Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
sasa tunaelekea pazuri, maana tumefika kujiuliza nani mkoloni wa kiarabu na nani mwananchi au muwatwin, na sasa tutaona kwa nini mapinduzi si kudai uhuru tu kama inavyodaiwa bali kuna mengi yaliyojificha.

tuendeleeni kuyatafuta
 
sasa tunaelekea pazuri, maana tumefika kujiuliza nani mkoloni wa kiarabu na nani mwananchi au muwatwin, na sasa tutaona kwa nini mapinduzi si kudai uhuru tu kama inavyodaiwa bali kuna mengi yaliyojificha.

tuendeleeni kuyatafuta
...........tusaidie basi, naona kama unajua mengi lakini umeamua kuyaweka kibindoni na kutuacha tuchakarike kuyatafua.
 
Okelo hakutajwa kabisa katika kumbukumbu za historia ya Zanzibar revolution. Leo hii Karume ndiye wengi wanamuelewa kama ndiye kiongozi aliyefanikisha mapinduzi yale. Documentary hii inaonyesha watu wengi waliuawa kule Zanzibar, je ni nani walikuwa wanafanya mauaji hayo? Wananchi wengi walionekana kukimbilia baharini ili kupata usafiri wowote kujaribu kunusuru maisha yao lakini wengi wao miili yao ilionekana kuelea baharini siku ya pili yake.

Tabia ya udanganyifu ambayo tunaiona hii leo ilianza tangu zamani, na kwenye hii documentary hata hilo jina la Karume halikusikika kabisa hii ni ishara ambayo inaashiria matatizo ya Zanzibar ambayo hadi leo yanausakama muungano. Utakumbuka vile vile wazanzibari wengi waliunga mkono uanzishwaji wa CCM na kufuta TANU na ASP kwa malengo ya kijikwamua katika uovu ambao ndio nguzo kuu ya fuku fuku la matatizo ya Zanzibar. Karume alifahamu bila muungano asingeweza kudumu kwa muda mrefu ndio sababu alikimbilia kuungana na Tanganyika haraka haraka ili ajilinde na wale waliojua mapungufu yake na kuondoa shaka ya kuvamia na maharamia wa wakati ule.

Jan 1964 watutsi takriban 18 000 waliuawa (genocide) na waliobaki walinusurika kwa kukimbilia Uganda, Je ni hawa ambao sasa hivi wameamua kulipiza kisasi? Je Kagame na Museveni hawana ukabila wa wale waliouawa? Chimbuko la matatizo ya Rwanda linashabihiana na mauaji haya. Je kuna vigezo gani vilitumika kuhakikisha hayawezi kutokea tena? Historia inatusuta kwani hii inaonekana ni circle ambayo itaendelea kwa muda. Sisi Tanzania tunaweka mechanism gani kuhakikisha matatizo kama ya Rwanda hayawezi kuja kutokea Tanzania.

Tabia ya viongozi wa Tanzania hivi sasa haitofautiani na tabia ya wazungu walioonyeshwa kwenye hii documentary:

1. Wazungu walikuwa wanawaua waafrika kama ndege.

(i) Viongozi wetu wanaua maisha ya WTZ kwa kuiba pesa za walipa kodi na kuzifuja kama zao.

2. Wazungu waliweza kuamrisha kuwazika watoto wa shule kwenye makaburi wakiwa hai.

(ii) Viongozi wetu wanawanyima karo vijana wa Tanzania kule Ukraine hadi watoe chau chau utafikiri hizo pesa wanatoa mifukoni mwao.

3. Ukiangalia kwa makini hii documentary utaona ujinga ambao ulitawala raia wa wakati ule, yaani ngozi nyeupe ndio super.

(iii) Hivyo hivyo ndivyo JK na EL wanavyofanya hivi sasa kwa wale waliowapa dhamana ya kuongoza. Wananajisikia ufahari zaidi wanapokuwa na marafiki wazungu na wa kiarabu ambao wanajifanya ni wawekezaji kwenye mikataba mibovu ya kuwahujumu wananchi wanaolipa kodi.

Wabunge wanaambiwa wasiulize wanyamaze kama maji yaliyo mtungini.
 
Revolution in Zanzibar by field Marshall John Okello...nakumbuka kusoma kitabu hicho miaka ya 70 na kinaeleza jinsi huyu Bwana alivyoongoza mapinduzi kisha kwa kujiona si mwenyeji wa huko akamtafuta Karume na kumkabidhi dola ingawa alikuwa kwanza akimuwaza Abdul Rahmaan Babu kama mtu anayefaa.Waarabu waliingiliwa majumbani mwao wakauliwa na wengi wakaikimbia nchi.Ni kwa kuwa wengi walikuwa wanachama chama kilichokuwa madarakani cha HIZBU..au ZNP kilichoungana na ZPPP.ASP walikuwa ni chama cha upinzani.Vyama vyote vilikuwwa vya kizanzibari.

Mauaji ya Zanzibar hayakuwa tofauti na yale ya Rwanda.Haijajulikana hadi leo John Okelo alitumwa na nani na alikuwa akitekeleza mpango huo kwa kutumwa na nani.Lakini Zanzibar ilishuhudia mauaji ya watu wengine zaidi baada ya mapinduzi kama yale ya Kassim Hanga,Othaman Sharif na watu wengine wengi wasiokuwa na majina.Historia ya matukio haya iligeuzwa na kuwa ukombozi wa mwafrika aliyekuwa katika utumwa wa kiarabu.Wazanzibari wenyewe wanajua kuwa hakukuwapo utumwa tena wakati wa tukio la mapinduzi.Joto la siasa lilikuwwa kubwa na watu wengine mbali walitumia fursa hiyo kumwaga damu kwa kutumia vigezo vya utumwa.Usultani kama ulivyokuwapo Rwanda na Burundi ni kitu ambacho kilikuwapo.Waarabu wa Zanzibar hawakuwa wavamizi wa kigeni waliotaka kushika madaraka kwa nguvu.Watu wenye asili ya Kiarabu walikuwa afadhali kidogo kuliko wale wenye asili ya Shirazi na asili ya Bara lakini ni kama vile Wachina wa Malaysia.Huwezi kuwaua ili uweze kumiliki walichonacho.

Anyway mimi naona tusamehe yaliyopita lakini kama kuna watu wanataka kufanya utafiti wa nini kilichotokea kuna watu wengi Zanzibar wenye umri mkubwa wanaweza kupatikana na kutoa picha ya matukio ya mwaka 1964 na baada ya hapo.
 
tuvuteni subra ,nina hakika iko siku siri itafichuka na ukweli utabainika ,na siku yenyewe ni pale tanzania itakapopata kiongozi atakaejali ukweli na uwazi wa kila jambo la kwenye historia(yakiwemo ,muungano,mapinduzi ya zanzibar,kuunganishwa tanu na asp n.k), na kwa upande wa zanzibar nao pale watakapofikia wakati wakajiamini kuuhoji muungano katika serikali ya muungano.na wananchi wa tanzania nao wakasimama kidete kudai nyaraka kwa kila kilichopita katika historia. itakuwa lini? mungu ndie anaejua zaidi ,ila kwa sasa kunahitajika umoja katika taifa ili kutetea haki ya wanaonyanyaswa na dhulma zinazoendelea,tukiamua kwa pamoja tutaweza.
 
Kassimu Hanga alinyongwa kwa madai ya makosa fulani kama ya uhahini vile. Taarifa zake hazijulikani sawasawa, ila alikuwa amekimbia nchi kipindi kimoja na Kambona. Yeye hakukaa sana ugenini, akaamua kurudi nyumbani ndipo akanyongwa.

Mwenye taarifa kamili kuhusu Kassim Hanga atutolee
 
hiki kitabu niliwahi kukisoma zamani lakini naona kwangu sasa hakifunguki sijui tatizo ni nini lakini ni moja ya kitabu ambacho kina majibu mengi ya hili tunalolizungumza na wakati huo huo kuibua mijadala mingi.

nnategemea tutajitahidi kwa sote kuutafuta ukweli juu ya yote yaliojiri
http://www.fortunecity.com/victorian/abbey/313/ukweli.html

UKWELI NI HUU (KUUSUTA UWONGO)

Aman Thani Fairooz

Dibaji
Kitabu Hichi
Ukweli Ni Huu (Kuusuta Uwongo)
Utukufu Na Neema Ya Zanzibar
Zanzibar Na Ubaguzi Kabla Ya Mavamizi
Ubaguzi Umeanzishwa Zanzibar Wakati Wa Serikali Yenye Kujiita Ya "Mapinduzi"
Elimu Na Matibabu Bure!

Taalimu
Matibabu
Hali Za Maisha
Neema Zilikuwepo
Kuanza Harakati Za Siasa
Sheikh Ali Muhsin Kwenda Nchi Za Ulaya Ikiwemo Na Uingereza Kupigania Uchaguzi Wa "Common Roll" (Mtu Mmoja Kura Moja).
Kuasisiwa Hizbul-Wattan (Zanzibar Nationalist Party)
Wakoloni Dhidi Ya Hizbu, Uhuru Na Umoja Wa Zanzibar
Makao Makuu Ya Hizbu
Hizbu Kumleta Zanzibar Seyyid Abdul-Rahman (Babu)
Natija Ya Safari Ya Sheikh Ali Muhsin
Wakoloni Na Nyerere Ndio Waasisi Wa Afro-Shirazi
Uchaguzi Wa Mwanzo Juni 1957
Kwanini Sheikh Ali Muhsin Aliamua Kusimama N'gambo Badala Ya Majumba Ya Mawe?
Kwenye Shari Huzaliwa Kheri
Kukuwa Kwa Harakati Za Siasa
Ati Husemwa Kuwa Hizbu Imefeli!
Kugawanyika Kwa Afro-Shirazi
Kuasisiwa Kwa Zanzibar And Pemba Peoples' Party (ZPPP)
Tume Ya Sir Hillary Blood
Uchaguzi Wa Pili, Januari 1961
Uchaguzi Wa Tatu Juni 1961
Ushirikiano Wa ZNP/ZPPP
Kutokufaulu Mazungumzo Ya Mwanzo Ya Katiba Ya Uhuru
Afro-Shirazi Iliandaa Machafuko Siku Ya Uchaguzi
Muungano Wa ZNP/ZPPP, Waunda Serikali
Kutokufaulu Mazungumzo Ya Mwanzo Ya Katiba Ya Uhuru
Babu Kutoka Katika Hizbu
Dhamiri Za Babu
Kufungwa Gerezani Kwa Seyyid Abdul-Rahman Babu
Kutolewa Gerezani Babu
Babu Na Fisadi Yake Ya Mwisho
Kipi Kilicho Mpelekea Babu Kuchukua Khatua Kama Hizo
Uchaguzi Wa Julai 1963
Nyerere Anasema Wakoloni Walipendelea Kuiacha Serikali Ya Zanzibar Mikononi Mwa Hizbu
Mkutano Wa Katiba Ya Uhuru.
Uhuru Wa Zanzibar
Sherehe Za Uhuru
Yaitwayo "Mapinduzi"
Kuuliwa Kwa Muhsin, Suleiman Na Ahmed
Kifo Cha Ali Mzee Mbalia
"Skolashipu" Za Misri
Yaliyo Nifika Nafsi Yangu Na Hayo Yenye Kuitwa "Mapinduzi"
Maafa Ya Gerezani
Kufungwa Kifungo Cha Miaka 10 Gerezani
Kiasi Cha Kazi Alichokuwa Akifanyishwa Mfungwa
Maovu Waliyotendewa "Wafungwa Wa Kisiasa"
Kutolewa Gerezani
Nakimbilia Dar-Es-Salaam
Mahabusi Wadhulumiwa Wa Mwalimu Nyerere
Mateso Ya "Kwa Ba Mkwe"
Maisha Ya Gereza Langoni
Nyakati Za Kufanyishwa Kazi "Wafungwa Wa Sisasa"
Ufungwa Wa Karume Ni Zaidi Ya Utumwa
Kurejeshewa Uhuru Wetu
Kuuliwa Wananchi Msikitini
Kuuliwa Kwa Wananchi Wengine
Namna Walivyo Uliwa
Wafungwa Waliyokufa Gerezani
(1) Mzee Mohammed Mbaba
(2) Maalim Harun Ustadh
(3) Idi Hassan
(4) Ramadhan Ibrahim Saadalla
Wameuliwa Vifungoni
Wafungwa Wengine Wauliwa
"Wafungwa Wa Siasa" Bado Waendelea Kuuliwa
Aliyonizungumziya Twala
Yalomfika Othman Shariff
Kuteswa Na Kuuliwa Othman Shariff
Kufungwa Na Kuuliwa Saleh Saadalla
Karume Kuanza Kumbadilikia Twala
Mwisho Wa Twala
Makomred Wamechangia Maafa Yaliopo Nchini
Kwanini Mwalimu Nyerere Alikataa Kuwapeleka Zanzibar Watuhumiwa Wa Kesi Ya Ukhaini?
Siri Hii Ni Kubwa Sana!!
Serikali Ya Mavamizi Ya Zanzibar Bado Imo Na Ubaguzi Wake
Nilitakiwa Nitoke Nchini
Namna Nilivyoondoka Kuukimbia Wattani Wangu
Kuleta Ahli Zangu Dubai
Mengineyo Kwa Ufupi
Mwalimu Na Uislamu
Mwalimu Na Utumwa
Porojo La Mitaani
Demokrasi Ya Vyama Vingi (Multi-Party Democracy)
Vipi Kuifikilia Demokrasi
Shukrani

DIBAJI
Namshukuru Mwenye Enzi Mungu Mwenye Wingi wa Rehema Kubwa na Ndogo kuniwezesha kuandika kijitabu hiki ambacho nimejaribu kiasi nilichoweza kuyaeleza yale yaliyotokea katika Nchi yetu, Zanzibar. Na yaliyonitokelea mimi mwenyewe na yaliyowatokelea Wananchi wenzangu kutokana na hayo yenye kuitwa, "Mapinduzi" yaliyofanyika katika Visiwa vyetu mnamo taarikh 12 Januari, 1964. Haya ninayoyaandika ni kiasi ya hayo niyajuayo mimi tu; hapana shaka yapo mengi ambayo sikupata kuyajuwa. Bali nataraji watatokea wenzangu nao, wakayaeleza waliyotendewa au waliyoyaona yakitendwa.

Nafanya haya si kwa makusudio yoyote mengine zaidi ya kutaka kueleza ukweli wa yaliyotendeka katika Nchi yetu ili Wananchi wenzangu (na ndugu zetu wa Tanganyika, bali na ulimwengu, pia) na khasa wale waliokuwa wadogo, na wale ambao hawajaja duniani wakati huo waweze kuyafahamu japo kwa uchache yaliyotendeka katika Nchi yao kwa hayo yenyekuitwa "Mapinduzi". Ikiwa katika kuyaelezea haya, kutahitajia kumtaja mtu au watu kwa njia yoyote, itakuwa nafanya hivyo kwa kutokana na maudhui ninayo izungumza wala si kwa ajili ya kusengenya au kukejeli au kudharau au kwa kutia illa za namna fulani, hashaa! Bali kwa vile dhamiri ya kukiandika kijitabu hiki ni kuelezea ukweli wa mambo yalivyokuwa, basi sitochelea kulieleza lolote madhali kwa kufanya hivyo ndio itakuwa natimiliza lengo nililolikusudia, nalo ni kuueleza ukweli. Kutokana na hayo, nachukuwa nafsi yangu mas-uliya yote yatayotokea katika maandishi haya.

Muhimu, nawaomba wasomaji wangu wajishughulishe zaidi na hayo niliyokusudia kuyaeleza, kwani hayo hayana shaka yoyote, ni kweli tupu. Na nawaomba wasijishughulishe na makosa madogo madogo, kama vile ya upigaji chapa, makosa ya lugha au juu ya utaratibu wa uwandishi.
Ikiwa litatokea suala lolote, au ikiwa lolote halitafahamika, basi wakurejelewa ni mimi. Inshallah, nitajaribu kama nitavyoweza kutanzua kila lililotanzika na ikiwa nitashindwa, basi sitoona taabu kutaka msamaha. Mwenye kukamilika kwa yote ni Mwenye Enzi Mungu.

Tunamuomba Mwenye Enzi Mungu ajaaliye haya tunayoyaeleza yapate kusomwa, kuzingatiwa na kufahamika na ipatikane faida ndani yake kwa kutumiwa kwa kheri. Kubwa ya kheri hizo ni kusahihisha palipo haribika, kuiondosha haramu, kuomba toba na kutenda mema, kwani mema huondowa mabaya. Mwenye Enzi Mungu atupe taufiq, Amin.

Aman Thani Fairooz
P.O. Box 10836
Telephone 04-850802
Dubai United Arab Emirates
Januari, 1995


KITABU HICHI
Kidogo-basi, Chungu-tamu.
Kwa hakika Kitabu hichi ni kidogo basi. Lakini, kama alivyosema muandishi kuwa kaandika kwa ufupi, bali ufupi wa kutosheleza faida yake. Yoyote atakaye kisoma kitabu hichi kwa kutaka kufahamu na bila ya mawazo yake kudhibitiwa na kupenda au kuchukiya, basi hapana shaka atapata faida. Atafahamu jinsi wananchi wa Zanzibar walivyokuwa katika harakati zao za kuwania uhuru wa nchi yao kutokana na ukoloni wa Muingereza. Harakati ambazo zalianza kabla ya miaka ya 1940. Pia ataweza kufahamu ni nani walioanzisha harakati hizo, namna zilivyopata kuungwa mkono na wananchi na namna zilivyokuwa zikiendeleya. Pia atapata kufahamu jinsi ya pingamizi zilivyokuwa. Atafahamu pingamizi hizo zilivyoanzia, nani aliyezianzisha na kuzipalilia na kuzikuza.

Atafahamu natija yake! Pia atafahamu vipi wananchi chini ya uwongozi wa vyama vyao ZNP/ZPPP walivyokuwa wakizikabili pingamizi hizo. Na zaidi atafahamu juhudi za waongozi wa ZNP/ZPPP katika kutaka mafahamiano na ushirikiano na wananchi wenziao - ASP - na nini ulikuwa muelekeo wa waongozi wa ASP, muelekeo ambao mara nyingi ulikuwa ukiathirika kwa uwongozi na fikra zilizokuwa zikipangwa na kuletwa kutoka nje ya nchi. Chungu-tamu. Kweli ni chungu! Lakini ni wajibu isemwe na kubainishwa. Uchungu uliyomo ndani ya kitabu hichi ni kuona jinsi wananchi walivyohangaika kwa jasho, mali na hata damu zao kwa kuwania uhuru wao kutokana na ukoloni wa Muingereza, lakini kwa sababu ya husda, chuki na ufisadi uhuru huo haukuachiwa kuishi zaidi ya siku thalathini! Isitoshe, sio kuwa uhuru huo ulipotezwa kwa kutumiliwa njiya za usalama, sivyo, bali kwa fujo! Fujo ambalo natija yake ni kupotezwa Dola ya Zanzibar, roho za wananchi, heshima ya binaadamu, mali za watu na mwisho kuwachwa wananchi kuishi ndani ya haramu.

Utamu - japo kwa hakika sio utamu - ni kwa vile kuweza wananchi kupata kuufahamu UKWELI ambao kwa muda wa zaidi ya miaka thalathini umekuwa ukifunikwa kwa UWONGO. Lakini, kama yalivyo maumbile, kweli daima huibuka.

Tunamshukuru Mwenye Enzi Mungu kwa kudhihiri kitabu hichi na kuweza kuufahamisha umma, bali na ulimwengu, maafa yaliofikishiwa Zanzibar, Nchi na Wananchi.

Msomaji, na pengine hata asimuliwaye haya, huenda akasema, yaaleiti yalielezwa haya kiasi cha miaka ishirini liyopita, au kabla ya hapo. Hivyo ni kweli! Lakini kila kitu kwa majaaliwa, na kuchelewa kwengine kuna kheri zake kama kwengine kunavyo shari zake. Kheri katika kuchelewa kudhihiri kitabu hichi ni kuwa vijana waliokuwa wadogo wakati wa maafa ya Zanzibar leo ni watu wazima, wenye uwezo wa kufikiri, kuamua na kutenda. Kwa hivyo wanahitajia kuujuwa Ukweli.

Wao si kwa ajili ya Kuusuta Uwongo, hashaa!! Bali ni kwa ajili ya kuujuwa ukweli, kisha iwe ni mafunzo kutokana na yaliotendeka. Watasoma, na Inshallah watayafahamu na kuyatumia. Na haya ndio khasa makusudio na faida ya kitabu hichi. Kutumia kwao huko kwanza iwe ni kwa kuepusha yasitendeke tena maafa yaliyotendwa, kufuatilia hilo - au yote mawili sambamba - ni kwa kufanyakazi katika kujenga palipo bomolewa. Kubomowa daima ni rahisi kuliko kujenga, kujenga kunataka umoja na ushirikano wa kila mmoja wetu. Kwa hivyo ni waajibu wa kila mmoja wetu kushirikiana, bega kwa bega, kwa nia na nguvu moja kufanyakazi kuirejesha Zanzibar. Kwanza, kuirejesha katika ramani ya ulimwengu ili iwe na jina na pahala pake kuwa ni Dola kaamili na iliyo huru. Kisha, bali ndio la muhimu, kuirejesha katika neema zake.

Hichi ni kitabu cha kusomwa na kila Mzanzibari, bali na ndugu zetu wa Tanganyika, pia.
Abdulla Ali (Baba)

UKWELI NI HUU (KUUSUTA UWONGO)
Nimelichagua jina hili la UKWELI NI HUU KUUSUTA UWONGO, baada ya kuyasikia na kuyasoma me ngi ya uwongo na hata yakafika kusomeshwa watoto wetu katika maskuli ya Zanzibar kukhusu hayo yenye kuitwa "MAPINDUZI" yaliyofanyika katika visiwa vyetu vya Zanzibar mnamo taarikh 12 Januari 1964.

Kabla ya kuingia katika hayo, ningependa ku-waambia wasomaji wangu wote kuwa mimi si mjuzi hata kidogo wa fani hii ya uandishi; tena ni mbovu sana katika "spellings" na ka-tika "nahau" za Kiswahili cha kisasa. Pia nawaomba radhi kwa Kiswahili changu cha kizamani
Bali, kutokana na huo uzushi na kupotezwa kwa makusudi ukweli wa hayo yaliofanyika kukhusu hayo yenye kuitwa "mapinduzi" nimeo-na sina budi illa ni kujitolea hivyo hivyo juu ya upungufu wangu katika fani hii ya uandishi. Lakini ukweli lazima niudhihirishe ili vichipukizi vyetu viweze kuyaelewa vilivyo yaliyotendeka katika nchi yao. Kwani wengi walikuwa wadogo na wengine walikuwa hata hawajazaliwa katika wakati huo.

Ilivyokuwa Kiswahili ni lugha yangu ya kuzaliwa, basi ninaiandika kama ni-navyoisema. Si shughuliki na "kua au kuwa, aliniambia au aliniambiya, ameuawa au ameuw-awa kenda au kaenda, amekwenda au ameenda". Hayo kwa wataalamu wa lugha ni mambo muhimu lakini kwa mimi nakutakeni msamaha juu ya hayo. Muhimu ya kuyaangaliya na kuyazingatiya ni yale nikusudiayo kuyaeleza, kwani hayo ndio muhimu na ndio ya kweli tupu isi-yokuwa na dosari hata chembe.

La mwanzo nitakalo kuombeni mlifahamu uzuri ni ile hakika ku-wa hayo yaliyofanyika katika visiwa vyetu taarikh 12 Januari 1964, hayakuwa "MAPINDUZI" wala hayafai hata kidogo kuitwa 'mapinduzi' kwa maana asili ya neno. Bali kwa maana zote yalikuwa khasa ni "MAVAMIZI", yaani kwa Kiingereza - "INVASION".

Mapinduzi lazima yapangwe, yaongozwe na yatekelezwe na wananchi wenyewe kwa maslaha ya nchi na wananchi wake. Sasa tukiangalia hayo yaliotendeka Zanzibar, yali-pangwa, yaliongozwa na yalitekelezwa na WAGENI kutoka nchi za nje za jirani zetu. (Ni wao wala si wananchi ndio waliochukua ngawira kubwa kubwa).

Haya yanathibitika zaidi kwa vile kuwa huyo jamadari aliyeyaongoza hayo 'mavamizi' ni John Okello na wa chini yake waliku-wa Injini na Mfaranyaki. Nani kati ya hao aliyeku-wa kitovu chake kimezikwa visiwani? Okello amezaliwa na amekulia kwao Uganda, Injini amezaliwa na amekuliya kwao Kenya na Mfaranyaki amezaliwa na amekuliya kwao Tanganyika. Wote hao walikuja Zanzibar wakiwa watu wazima na shughuli zao, wamekuja kutafuta kibarua na kukimbia kodi za kichwa katika nchi zao.

Liangalie hilo waliloliita "Baraza la Mapinduzi". Utaona sehemu kubwa ya wanachama wa Baraza hilo walikuwa si Wazanzibari, laa kwa kuzaliwa wala kwa kuchukua Tajnisi (Kuandikisha Uraia). John Okello, Khamis Darweshi, Seif Bakari, Said Natepe, Said Washoto, Muhammed Mfaume, Edington Kisasi, Mohammed Abdalla Kaujore. Ukiwaacha wengineo ambao nao vile vile walikuwa si wananchi wa Zanzibar kwa kuzaliwa, bali wao walikuja Zanzibar wakiwa katika migongo ya wazee wao na waliendelea kuishi humo visiwani kwa maisha yao yote. Na wakachukuliwa kama ni Wazanzibari.
 
MtuMwitu,

Ingawa ninapenda sana kujua hali halisi iliyotokea wakati wa Mapinduzi yale kwa nia njema kabisa, naona hicho kitabu ulicholeta kinasimulia kwa udini kikidai kuwa Nyerere hakupenda waislamu. Swala hili tuliwahi kulijadili sana huko nyuma na wala sipendi lichafue mada hii ambayo nia yangu ni kuanika ukweli kuhusu mapinduzi yale bila kuweka propoaganda zozote.

Ingawa sijasoma kijitabu chote, na nitakisoma kwa vile kinatoa background nzuri sana ambayo sijawahi kuipata, madai ya Nyerere kuchukia waislamu siyaoni yanavyohusika na mapinduzi haya kwa vile kuna waislamu wengi waliotokea Zanzibar ambao Nyerere aliwapa madaraka makubwa tu, kwa mfano Abdulrahamn Babu, Salim Ahmed Salim, Abdallah Natepe, Ali Hassan Mwinyi, Col Mahfudh, Brig. Yusuf Himid na wengine wengi tu. Na kuhusu uarabu, utakumbuka kuwa Abudulrahman Babu alikuwa ni kati ya mawaziri waliopendwa sana na Nyerere kabla ya kupewa pressure kutokea huko huko Zanzibar kuwa amwengue serikalini.

Tafadhali tuache propaganda za kidini na kisiasa tutafute ukweli wa mapinduzi yale. Nina na wasiwasi kuwa Nyerere anaweza kuwa alihusika kwa namna fulani lakini si kwa sababu za udini.

Mwandishi kanikumbisha mfuasi mmoja wa Okello aliyekuwa akiitwa Mfaranyaki; huyu naye aliishia wapi? Jambo jingine naona kamwa mwandishi anachukulia kuwa mapinduzi yale yote yalifanywa na watu wa kuja tu siyo kuwa yaliongozwa na Okello ambaye alikuwa wa kuja bali pia walioshiriki wote walikuwa ni wa kuja tu. Je walitumwa na nani kwenda kufanya mapinduzi hayo? Nitasoma kijitabu lakini kama kuna mwenye jibu au ufafanuzi zaidi atutolee hapa.
 
mtumwitu,
nimekisoma hicho kitabu na kinaeleza mengi kuhusu jamaa "waliopotea" ZNZ. mwandishi badala ya ku-stick to the facts, anajaribu kuchomekeza ajenda binafsi na kumhusisha Nyerere kwenye matatizo/migogoro ya WaZNZ.
 
Kichuguu,
Hata mie ila picha ya Okello kuonana na Mwalimu baada tu ya Mapinduzi- na jinsi alivyokuwa natembea kwa kujiamuni-iliashiria Malimu alijua kitu kabla. Ila naona haiongelewi.
Ila kwa sasa ni miaka 40- tusonge mbele na tujadili namna ya kuleta umoja na utengamano wa visiwani na kuimarisha Muungano.
 
kichuguu,
sijui nilisoma wapi, lakini nakumbuka ZNZ iliwahi kuwa na hadhi ya Arab Republic, or Sultanate. Serikali ya ZNZ iliyopewa Uhuru ilikuwa ikitambulishwa kwa jina gani? May be I am wrong.

Hilo suala la Udini hata mimi nimeliona, na nashukuru kwa tahadhari uliyoitoa. Linaweza likaharibu mjadala huu.

All in all, naamini kulikuwa na matatizo ya kimsingi yaliyolazimisha Mapinduzi ZNZ. Ukatili na mauaji yaliyotokea baada ya hapo nadhani ndiyo yanayatia doa Mapinduzi yale.
 
nnaamini hicho kitabu yapo mengi ya kujifunza na yako ya kuacha, pia yapo ambayo yanaibua mijadala mipya lengo hasa tunataka tufike kule ukweli ulipo.

nnaomba kama kwake mtu kitafunguka chote anitumie maana nilikisoma zamani na sasa hakifunguki chote.

mapinduzi haya yana utete mkubwa sana, ila tunahitaji kuvumiliana na kutafuta ukweli kwa kufanya utafiti.

mie nnapenda sana tusahau yaliopita japo machungu ili kujenga wakati tulionao na wa mbeleni.

lkn ukweli hali zanzibar imechafuliwa sana na mapinduzi yale
 
Kichuguu,
Hata mie ila picha ya Okello kuonana na Mwalimu baada tu ya Mapinduzi- na jinsi alivyokuwa natembea kwa kujiamuni-iliashiria Malimu alijua kitu kabla. Ila naona haiongelewi.
Ila kwa sasa ni miaka 40- tusonge mbele na tujadili namna ya kuleta umoja na utengamano wa visiwani na kuimarisha Muungano.

Usiku wa kuamkia mapinduzi, Nyerere aliarifiwa; Babu alikwenda Dar usiku huo kuonana na Nyerere kwa kutumia mtumbwi peke yake. Okello alikwenda kuonana na Nyerere baada ya kama siku nne hivi tangu usiku wa mapinduzi. Wakati huo mambo yote yalikuwa yameshajulikana na alikuwa ameshamsimika Karume kuwa Rais wa Zanzibar, ndiyo maana alikuwa na confidence vile.


Katika siasa za Zanzibar, Nyerere alikuwa upande wa ASP, lakini swala hili la kutumia nguvu sidhani kuwa lilikuwa kichwani mwake, najua kuwa walimstukiza sana. Ni around kipindi hicho hicho cha mapinduzi ya Zanzibar ndipo na yeye alikumbana na msukosuko wa yale maasi ya mwaka 1964.
 
nnaamini hicho kitabu yapo mengi ya kujifunza na yako ya kuacha, pia yapo ambayo yanaibua mijadala mipya lengo hasa tunataka tufike kule ukweli ulipo.

nnaomba kama kwake mtu kitafunguka chote anitumie maana nilikisoma zamani na sasa hakifunguki chote.

mapinduzi haya yana utete mkubwa sana, ila tunahitaji kuvumiliana na kutafuta ukweli kwa kufanya utafiti.

mie nnapenda sana tusahau yaliopita japo machungu ili kujenga wakati tulionao na wa mbeleni.

lkn ukweli hali zanzibar imechafuliwa sana na mapinduzi yale


Nakubaliana na wewe, yamo mengi ya kujifunza na vile vile yamo ya propaganda. Kama hutakipata mpaka katika masaa kumi yajayo nitumie PM nitakutengezea PDF nikutumie kwa vile kiko katika html nodes inabidi ukisome online tu.
 
sawa kaka yangu ntajaribu tena kukifungua na ikishindikana nitakujuilisha, mola akuzidishie moyo wa imani na huruma kwa watanzania wenzio
 
Kile kijitabu alichotuambai Mtumwitu hiki hapa. Nimekopi zile webpages na kufanya typesetting kwa kutumia software ya kizamani kidogo iitwayo Tex.

Sikuweza kurekebisha characters za kufungua usemi, kwa hiyo utaona kuwa alama zote za kufungua usemi zinafanana na zile za kufunga usemi. Ingenichukua muda kuzitafuta zote na kuzirekebisha, nadhani msomaji ataelewa.

Kuna chapter moja haipatikani, hii ni Chapter ya 15 iliyokuwa inamhusu mwandishi mwenyewe kwa hivyo nadhani aliondoa.

Kuna chapter mbili hivi au tatu hivi nimeziungansiha na kuwa Chapter moja ya 17 nikaiita "Kuuliwa kwa Wananchi." Nimeziunganisha kwa vile zilikuwa zinaongelea jambo lilelile, mpangilio wa kitabu haukubadilika.

Kwa jumla sikubadilisha maandishi mengine yote ya mwandishi isipokuwa labda marekebisho mawili au matatu ya typos katika quote zilizokuwa zimeandikwa kwa kiingereza kwenye ukurasa wa 32.

Nimekiweka hapa kwa ajili ya kurahisisha usomaji wetu tu. Nimewasiliana na mwandishi wake kwa e-mail lakini naona hajanijibu. Pamoja na kuwa hakina copyright protection yoyote, kuna haja ya kuheshimu effort ya mwandishi original. Kwa hiyo yeyote atakayekitumia asisahau ku-acknoweldge mwandishi original na original source ya kitabu pale http://www.fortunecity.com/victorian/abbey/313/
 

Attachments

Kile kijitabu alichotuambai Mtumwitu hiki hapa. Nimekopi zile webpages na kufanya typesetting kwa kutumia software ya kizamani kidogo iitwayo Tex.

Sikuweza kurekebisha characters za kufungua usemi, kwa hiyo utaona kuwa alama zote za kufungua usemi zinafanana na zile za kufunga usemi. Ingenichukua muda kuzitafuta zote na kuzirekebisha, nadhani msomaji ataelewa.

Kuna chapter moja haipatikani, hii ni Chapter ya 15 iliyokuwa inamhusu mwandishi mwenyewe kwa hivyo nadhani aliondoa.

Kuna chapter mbili hivi au tatu hivi nimeziungansiha na kuwa Chapter moja ya 17 nikaiita "Kuuliwa kwa Wananchi." Nimeziunganisha kwa vile zilikuwa zinaongelea jambo lilelile, mpangilio wa kitabu haukubadilika.

Kwa jumla sikubadilisha maandishi mengine yote ya mwandishi isipokuwa labda marekebisho mawili au matatu ya typos katika quote zilizokuwa zimeandikwa kwa kiingereza kwenye ukurasa wa 32.

Nimekiweka hapa kwa ajili ya kurahisisha usomaji wetu tu. Nimewasiliana na mwandishi wake kwa e-mail lakini naona hajanijibu. Pamoja na kuwa hakina copyright protection yoyote, kuna haja ya kuheshimu effort ya mwandishi original. Kwa hiyo yeyote atakayekitumia asisahau ku-acknoweldge mwandishi original na original source ya kitabu pale [B]http://www.fortunecity.com/victorian/abbey/313/[/B]


Mzee Kichunguu,
Mkuu hichi kitabu Kitatusaidia sana kufahamu nini kilijiri katika hayo Mapinduzi, kwani sisi wengine tunayasikia juu juu tu.

Lakini hiyo link hapo juu kwangu mimi haifunguki sijui kwa nini?
 
Msitake kudanganywa na hawa jamaa! kama Uislaam, na sisi pia waislaam vilevile, wasituwekee usiku hapa.

Mapinduzi ya Zanzibar yalikuwa muhimu iwe ni Okello ama ASP kwa sababu huwezi kumtaja Okello bila baraza la mapinduzi ambao walichukua Utawala. Okello aisngeweza kuota ndoto zake na kujua kuna mtu kama karume, ASP huko Zanzibar....acheni zuga!

Je, Nyerere alihusika?...Nyerere alihusika ktk Uhuru wa nchi zote za kiafrika baada ya Uhuru wa Tanganyika, kwa hiyo isije kuwa kisingizio...na wapo wa Zanzibar waliojihusisha kikamilifu ktk mapinduzi ya nchi za kiafrika. Je, Abrahman Babu aliwasili lini Zanzibar baada ya mapinduzi! na taarifa hizi alizipata vipi?...ni siku ngapi za usafiri wakati ule toka Cuba hadi Zanzibar!.. haya ni maswali madogo madogo tu ambayo ukijaza dots utapata jawabu.
Hao wafuasi wa Hizbu chama tawala wakati ule wengi wao walikuwa wakijiona kuwa wao ni waarabu, tena basi hadi leo hii wapo watu weusi ntilinti Zanzibar wanaosema kuwa wao ni Waarabu sio Waafrika!.nashangaa humu kuna watu mnataka kubadilisha lugha kuwasemea watu ambao hawauthamini kabisa Uafrika.

Mauaji ya Zanzibar hayawezi kuwa sawa na ya Rwanda hata kidogo!..labda kuna mtazamo tofauti hapa, na wala sielewi ktk kipimo gani hasa! Hawa watu walikuwa chini ya Utawala wa Sultan, hiyo demokrasia ya kuvizia haiwezi kusimama kabisa kwani hata Ian Smith alifanya uchaguzi huko Zimbabwe na hata akina Botha huko South Afrika...hii ilikuwa mbinu za watawala baada ya kuona kuwa mapinduzi Afrika yamechachamaa!..mbinu ambayo haikuwa zuga waafrika.

Na kama kweli hawa watu wafuasi wa Hizbu walikuwa Waafrika mbona wengi wamekwenda chukua Uraia Oman miaka ya 80 wakati Sultan wa Oman alipokubali kuwapokea Wazanzibar wenye asili ya huko. Haya si ndio alokataa Idd Amin na wahindi wa Uganda! hao watutsi na Wahutu hawana nchi ya kukimbilia ni raia wa Rwanda tofauti yao ni kabila tu sio asili mbili za bara tofauti. Kwa hiyo mkinipa mfano wa wazungu huko Zimbabwe na South nitakubalianana nanyi lakini sio rwanda hata kidogo.

Wote waliokuwa chini ya Hizbu, walikuwa viongozi chini ya Utawala wa Sultan wa OMAN. Swala sio rangi zao ama tunashangaa kuona weusi ktk serikali ya Hizbu! - ebu tujiulize:- hapakuwepo na Wahindi na waarabu ktk serikali ya mseto ya CCM baada ya mapinduzi?. hata huko majuu wapo watu wa mataifa mengine wameshika madaraka ya juu serikalini na wanajitambulisha kama raia wa nchi hizo. Pia wazee wetu walipokwenda pigana Burma walijulikana na askari wa Mkoloni, na waliuawa kama adui na sio kwa rangi zao kuwa tofauti na za master wao!

Tusitake kubabaisha issue hapa na kuanza nyoosha vidole kuhusu Mapinduzi. Washiraz walinyanyaswa karne kwa karne na wengi kuuawa sijasikia hata mtu mmoja akizugumzia zahma walizokuwa wakizipata hawa jamaa zetu chini ya Sultan. Saana utasikia mazuri ya Sultan ambaye kwa uzuri wake alikuja pinduliwa!

Ati leo tunataka hata kusifia tarehe na miaka ya kuacha Utumwa!... utumwa ulikwisha kama biashara lakini sio Utumwa ndani ya nchi hiyo na bado ahadi leo tunaziona athari zake. na watalii wanapokuja zanzibar msije fikiria kabisa kuwa ni sifa kuona yale mapango na makanisa ya utumwa!...sympathy tributes!

Kisha basi hakuna kipimo chochote kinachoweza kunambia kuwa mtumwa aliyepelekwa Marekani alikuwa na hali mbaya kuliko mtumwa wa ndani pale Zanzibar. tena basi nachelea kusema bora wao waliovuka bahari wamekuja kuwa na kizazi bora zaidi yetu.

Nakubaliana kama mtu atazungumzia maonezi yanayotokea leo Zanzibar chini ya uongozi huu lakini sio kuchanganya tawala hapa kama vile maonezi haya yanachagua rangi za watu. Ni maonezi ya kawaida kabisa ktk tawala zote hata sisi bara tunayapata vile vile ila kwa uzito tofauti kwa sababu Bara hakuna watu wenye msimamo mkali kama wa Wazanzibari, na pia hatujafikia kuzua husda kwa viongozi wetu kama ilivyofanyika Zanzibar...
Nitamalizia kusema kwamba kama baba yako, mama yako na wengine wote walikuwa waarabu na wewe kizazi cha leo bao unafikiria kuwa ni mwarabu hilo halinisumbui ila unapodai kuwa Hizbu ndio chama kilichokuwa mwakilishi halali wa watu wa Zanzibar hapo mjomba sinta afiki kabisa.
Mtaniuwia radhi kwa yote lakini imenibidi niseme yangu!

Maasalaam....
 
Bwana Mkandara umefanya utafiti? au unaropokwa tu ? samahani kama nitakuwa nimekukwaza
 
Back
Top Bottom