Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kero zake: Je, tuuvunje?
kichuguu,jembajemba,mtumwitu,mkandara,
Habari ya Karume kum-consult Nyerere wakati wa mazungumzo ya Uhuru naweza kuita ni "smoking gun." Sasa ndiyo maana nimepumzika huu mjadala, nikijaribu kupitia upya, na kuchunguza tena, uelewa wangu kuhusu kipande hiki cha historia ya ZNZ.
 
kichuguu,jembajemba,mtumwitu,mkandara,
Habari ya Karume kum-consult Nyerere wakati wa mazungumzo ya Uhuru naweza kuita ni "smoking gun." Sasa ndiyo maana nimepumzika huu mjadala, nikijaribu kupitia upya, na kuchunguza tena, uelewa wangu kuhusu kipande hiki cha historia ya ZNZ.

............ Now you are talking
 
stonetown i find your post very educative..kama unaweza kutupa na link ya ile ripoti ya HASHIM MBITTA kwenye pdf itakuwa safi...mimi nahisi hii dhana ya MAPINDUZI DAIMA! inaendelea kutumika kw a manufaa ya wachache..kwanza unaweza kunitajia wajumbe wa baraza la mapinduzi wa leo[masultani wapya]..na ni wangapi kati ya hao waloshika panga??!
 
Stonetown,
Tunavyoambiwa lengo la mapinduzi ilikuwa kumuondosha mtawala mweupe ambaye alikuwa akifanya ubaguzi na kutowapa haki wengi tunambiwa haki ilikuwa ikipatikana kwa wachache lakini hadi hii leo ubaguzi upo tena unauma zaidi kwa kuwa anayetubagua ni mweusi mwenzetu. na miaka zaidi ya 40 sasa haki inapatikana kwa wacheche ambao wana madaraka yaani wakubwa na familia zao ndio
wanaonufaika hivi sasa.

Kama hujafanya utafiti hiyo ndio ndoto ya waafrika wote!.. tulipopata Uhuru wetu sote tulifikiria hivyo kwa hiyo sio Zanzibar peke yake. Nitarudia kusema kwamba mapinduzi yoyote yanayoshirikisha chuki baina ya watu huja na maovu mengi. na sii kweli kabisa kwamba ni Baraza la Mapinduzi waliokuwa wakiwachukia wenzake ila ni chuki ya pande mbili inayoweza kuleta matokeo mabaya. Ndio maana ukaambiwa unapopigwa kofi geuka na ondoka kama huna Ubavu ama hutaki shari!..
Laukama mapinduzi yale yangeshindikana basi viongozi wote wa Baraza la Mapinduzi na ndugu zao wote wangekiona cha mtema kuni na wao wangekuwa wakilalamika hivi hivi, ndio maana sipendelei kabisa Mapinduzi ya kutumia mitulinga.

Njembanjemba,
Nadhani huko nyuma nimeeleza vizuri sana kutokuwepo kwa usawa wa ktk chaguzi zetu na kusema kweli tatizo kubwa la Kisiasa nchi Zanzibar limeletwa na kurudishwa kwa vyama vya Upinzani, yaani tumurusisha uhasama ule wa mwanzo ambao ulifikia Mapinduzi! Yawezekana kabisa wakati wa vyama vingi nchini humo haukuwa tayari kama ilivyo bara ambako bado watu wanafikiria kuwa Nyerere yuu hai kiasi kwamba unapokuwa na mtazamo tofauti ktk mrengo basi wewe ni adui wa nchi.

Sina budi kumpongeza JK kuweza kustahimili mikiki ya sasa hivi hasa ktk magazeti na pengine kuacha wananchi watumie nafasi kama hizi kujieleza. Hofu yangu sio JK na nina hakika sii yeye mwenye nguvu nchini ila ni CCM na hilo baraza la Mapinduzi. kwa hiyo zikusanyeni nguvu zenu sio kwa uhasama bali ktk njia iliyonyoooka kama vile unavyosoma Surat L'Fatah!
Tatizo lenu mnawapa CCM kisa sababu ya kutumia maguvu kwani wakitangaza Uchaguzi tu nyie mnaanza kusema damu zitamwagwa! mara msione Polisi mawe!.. vigenge vya kihuni ndivyo viunavyowapa hawa jamaa kila sababu. Tumiieni chama chenu kuweka mikutano ya amani na kutoweka tofauti zenu za rangi ama Upemba! msiwe wajinga kama ndege kurushiwa mtama mkafikiri ndio mnapendwa sana. Wenzenu wana njaa na njaa hii haiwezi kuondoka hadi Kiyama kwani shibe ya binadamu huenda kwa masaa!.. na ndinyo ilivyo tamaa ya Utajiri!..
 
Stonetown,



Njembanjemba,
Nadhani huko nyuma nimeeleza vizuri sana kutokuwepo kwa usawa wa ktk chaguzi zetu na kusema kweli tatizo kubwa la Kisiasa nchi Zanzibar limeletwa na kurudishwa kwa vyama vya Upinzani, yaani tumurusisha uhasama ule wa mwanzo ambao ulifikia Mapinduzi! Yawezekana kabisa wakati wa vyama vingi nchini humo haukuwa tayari kama ilivyo bara ambako bado watu wanafikiria kuwa Nyerere yuu hai kiasi kwamba unapokuwa na mtazamo tofauti ktk mrengo basi wewe ni adui wa nchi.

Sina budi kumpongeza JK kuweza kustahimili mikiki ya sasa hivi hasa ktk magazeti na pengine kuacha wananchi watumie nafasi kama hizi kujieleza. Hofu yangu sio JK na nina hakika sii yeye mwenye nguvu nchini ila ni CCM na hilo baraza la Mapinduzi. kwa hiyo zikusanyeni nguvu zenu sio kwa uhasama bali ktk njia iliyonyoooka kama vile unavyosoma Surat L'Fatah!
Tatizo lenu mnawapa CCM kisa sababu ya kutumia maguvu kwani wakitangaza Uchaguzi tu nyie mnaanza kusema damu zitamwagwa! mara msione Polisi mawe!.. vigenge vya kihuni ndivyo viunavyowapa hawa jamaa kila sababu. Tumiieni chama chenu kuweka mikutano ya amani na kutoweka tofauti zenu za rangi ama Upemba! msiwe wajinga kama ndege kurushiwa mtama mkafikiri ndio mnapendwa sana. Wenzenu wana njaa na njaa hii haiwezi kuondoka hadi Kiyama kwani shibe ya binadamu huenda kwa masaa!.. na ndinyo ilivyo tamaa ya Utajiri!..


Mkandara,

nasema tena Kaka Mkandara, wewe siasa za Zanzibar hujazielewa uzuri bado. wewe ungelikuja Zanzibar wakati wa uchaguzu ukafanya utafiti uliokuwa fair kabisa ndipo utakapojua ukweli wa mambo, kuwa nani ni muhuni kati ya CUF na CCM?. Sasa wale watu wa Pemba waliouliwa na CCM mwaka 2001 walikuwa wahuni? kama ni uhuni unafanywa ya CCM kwa kuwaandaa vijana wa janjawidi kushambulia wafuasi wa CUF tena wanawafata mpaka majumbani kwao kuwapa kipigo. Askari Zanzibar ni tawi la CCM na ndio wanaowalinda hao janjawidi wafanye wanavyotaka.

CCM washatamka wazi kuwa hawatatoka madarakani kwa makaratasi ya kura na hii sio siri wanasema mchana kuwa wao wamepindua yaani Mapinduzi daima.


Tumiieni chama chenu kuweka mikutano ya amani na kutoweka tofauti zenu za rangi

Hii ya tofauti za rangi mkuu umeipata wapi? au unaposema rangi unamaanisha nini? chama cha CUF ni masultani au? au unaweza kuonyesha mgawiko wa rangi ambao umo kwenye chama cha CUF?

Chama ambacho kinadumisha Amani Zanzibar kati ya CUF na CCM basi ni CUF, ingelikuwa nchi nyengine basi sasa hivi Zanzibar ingelikuwa haikaliki kwa jinsi ya mambo ambayo CUF inafanyiwa na CCM ikiwemo kunyang'aywa ushindi wake.
 
Under_age,
Kuna sehemu nimekuuliza kama sii wewe basi itakuwa Njembanjemba kama una rangi?... ilikuwa utani lakini sasa ngoja nikupe ukweli.
sidhani kama kuna umuhimu wa kujua rangi yangu katika hii mada.ila kama utaihitajia nambie nitakutumia PM, ila tukianza kuulizana rangi hapa ukumbini nadhani tutapoteza lengo la kutaka kuwaunganisha waliotengana.
ama kuhusu siasa ya zanzibar ,nitaungana na jemba jemba kwamba bado mkandara ni mgeni saaaaaaana wa siasa ya zanzibar , na ningekueleza mifano mingi, ila napenda niwaunganishe wazanzibari kwa kampeni ya nyumba kwa nyumba ,kuliko kudhihirisha utengano wetu hapa ukumbini. ila kama utapendelea nikupe mifano kadhaa wa kadhaa ya siasa ya zanzibar basi nijulishe na nita ku PM.kama unafikiri wazanzibari wa sasa wanabaguana kwa rangi, basi umekwenda mchomoo, hilo neno warabu na sultani linatumika kwa kampeni tuuu lisikusumbue.
jemba jemba,kichuguu,mzalendohalis,stonetown,mtumwitu, na wengineo , ahsanteni na kwa pamoja ,basi ipo siku tutafanikiwa.dhulma zimezidi kila kona ya ulimwengu,ila tujitahidini kwa ajili ya vizazi vijavyo,kama hatukufaidi sisi watafaidi watoto wetu.
ni mdogo wenu underage.
 
Kuhusu mauaji ya Karume, kweli yalikuwa ni ya kulipiza kisasi. Kijana mmoja aliyekuwa ASP aliuliwa na baba yake ambaye hakuwa ASP katika mapinduzi yale pia. Baada ya kijana huyo kupata kamisheni ya jeshi na kuwa Luteni ndipo akaamua kulipiza kisasi.


..jamaa alikuwa akifanya zamu za ulinzi huko jumbani mwa karume.

..siku akilewa au namna nyingi alikuwa anaapa kurudisha kisasi.

..karume akaelezwa lakini akapuuza.yadaiwa maneno yake yalikuwa hivi "aagh!hanithi huyo hawezi fanya hivyooo!"

..sasa siku ilipofika akavuta trigger!
 
Under_age,

Mjomba yaonyesha hata hunielewi kabisa nachozungumza. Ebu rudia mada zangu nyuma kisha jaribu kutafakari zaidi ya kunukuu!...

Kuhusu rangi yako niliuliza pale tulipokuwa tukizungumzia maswala la Mapinduzi na maafa yaliyotokea kiasi kwamba tukapoteza dira na kuwa ni swala kati ya waarabu na weusi.
Ndio sababu hasa ya kuuliza wewe rangi gani maanake tusije kuwa tunazungumza kwa rangi hapa badala ya Mapinduzi na maafa yake.

Tena nashukuru sana unaposema kwamba Zanzibar leo hii watu hawatazamani kwa rangi zao... hii ni alama kubwa sana na mafanikio ya Mapinduzi yale. Na kama umewahi nisoma mara nyingi mimi sipendi kabisa tunapo jadili kitu kwa kuzitazama nafsi zetu, rangi zetu, jinsia zetu bali hupenda kujadili issue zinazotuhusu sote kwa ujumla.

Hizo siasa za Zanzibar, huna haja ya kunitumia kama ni zinatoka Al noor maanake huzisoma na kwa bahati nzuri marafiki zangu wengi Wazanzibara na Wangazija na kwa kiasi kikubwa naiona Zanzibar kwa sura zote mbili.
Nitarudia kusema kwamba Wazanzibar siku zote wamekuwa nyuma kuelewa mbinu za CCM na mara nyingi anawapiga mabao ya penalt!.. kucheza mwacheza nyie , chenga mwawala lakini mshindi ni CCM kwa sababu mitego yote anayoiweka nyie kuingia kama ndege aloona mtama!..
Sasa nadhani turudi kwenye mada yenyewe maanake tumetoka ktk Mapinduzi na kuzungumzia haya ya leo kwa kisingizio cha Mapinduzi. Na kama utakumbuka niliwauliza swali moja! Bila mapinduzi yale unaweza kufikiria Zanzibar ya leo ingekuwaje?... wakati nchi zote zilizodai uhuru wa Bandia wakati ule zilianzisha mfumo wa Apartheid!.. Sultan ndiye aliyevikwa taji ya head of state!.. kweli hiyo Zanzibar ingekuwa tofauti na Rhodesia?.. Kama ni swala la Hizbu kuwa chama chenye weusi nilisema hata chama cha Ian Smith kilikuwa na weusi. Tanzania leo hii tuna viongozi weusi na wengi wao walikuwa against Mkoloni kwa Unyonyaji wao. Leo hii hawa wazee viongozi wetu ndio wanyonyaji wakubwa!..Hivyo basi hakuna guarantee yoyote ambayo inatuonyesha kuwa viongozi wa Hizbu wangekuwa tofauti na CCM/ASP. Hizi hadithi za kujaribu kujenga Umoja tumeziona ktk tawala zote za kiafrika na kwa bahati mbaya ndizo zimetugawa zaidi sisi wenyewe kuliko Mkoloni ambaye aliwakumbatia macheif wetu kutuweka sawa kama taifa moja la Tanganyika ama Zanzibar. Leo hii tunagawanyika ndani sisi wenyewe bila kujali rangi zetu ila mipaka iliyowekwa na Mkoloni kutumika kama ndio pindo la ardhi.

Kifupi ndugu yangu mimi siamini kiongozi yeyote yule ambaye anasimamia kundi la watu na wengine walobaki wanakaribishwa wakipenda ati nafasi yao ipo!
 
nasikitika sana watu wanao zungumzia mapinduzi ya kishenzi yalio tokea zanzibar ambayo ilikuwa ni dhulma na unyama mkubwa sana walio uliwa watu bure bila sababu ambao hawahusiki kiti wanao husiki waliwanyenyekea na kuondoka bila ya kuguswa na kulindwa waliuliwa watu bila sababu watoto wachanga kupigwa na vigogo vya mnazi na wengine kuchomwa moto kwenye matanuri leo hamyaoni hayo wengi wa walio fanya hivyo wapo nawasikitikia walivyo tegemea sivyo ilivyo kuwa napenda nikuelezeeni kisa cha kweli ambacho mungu anashuhudia mmoja ya watu walio husika kwenye mauaji ya tarehe 12jan ambae alikuwa akijisifu kwa kuwaua watu na kuwazini ilifikawakati akawa anaomba madukani kisa chenyewe ni hivi mimi nilikuwa fundi kuchonga nilienda kufanya kazi ya kutengeza makabati mchangani unguja maeneo ya mbuyuni kuna siku alikuja mzee mmoja kazi yake kuomba madukani apewe pesa sasa siku hiyo alipita kuomba pesa katika duka la mama mmoja kachanganya baba mwarabu na mama mswahil yule mzee akaomba asaidiwe pesa yule mama akamjibu wewe si mzee fulani yulemzee akajibu ndio mwanangu unanikumbuka akasema ndio nakujua na sitokusahau maisha yangu yule mama akamwambia yule mzee unataka nini nikusaidie yule mzee akasema mwanangu sina pesa za chakula hali yangu masikini yule mama akamjibu njoo kila ukiwa huna pesa mimi nitakusaidia wala usikhof akampa kwa siku zile 85 kama shs 5000 yule mzee akafurahi sana akashukuru na kujifanya kama yule mama kamea akaondoka yule mama hakusema kitu ikachukua kipindi nilibahatika tena kwenda kwa yule mama kumfanyia kazi zake kwani ilikuwa karibu na eid haji yule mzee akaja tena akapewa tena pesa sikujua kiasi gani lakini pale dukani yupo mzee mwengn huwa anauza duka la yule mama sasa hali ilikuwa hivi yule mzee anae uza duka akamuuliza yule mama mwenye duka vipi huyu mzee unamkumbuka wapi baada ya kuondoka yule ombaomba mzee wa mapinduzi akamwambia huyu siku ya mapinduzi aliniuliababa yangu na kumzini mama yangu baada ya kumuua leo nasikitika kuona hali yake iko hivianapita akiomba na ndio maana nikamwambia sitokusahau maisha yule mama hakusema kwa ubaya na alimwambia ukiwa na shida njoo nitakusaidia sasa yule mzee anae muuziaduka kusikia vile akajua yule ombaomba hajafika hata darajani akamfata akamwambia wewe huna hata haya yule unopita kumuomba pesa umemuulia baba yake na kumzinia mama yake ulipo muua basi yule mzee alianguka na kufa palepale yeye alisahau kama alifanya vile na aliona watu hawakumbuki hayo ndio malipo ya wale wanao jifanya eti ni wana mapinduzi viko visa vingi tu ndio ukaona hadi leo wanaogopa kukubali ukweli na wanazidi kutiachuki na husda miongoni mwa watu walio wajinga kusingizia eti warabu watakuja kutawala jamani dunia ya sasa kuna mtu anae taka kumtawala mwenzake warabu leo ndio wenye mali na sisi tunakwenda kuomba kwao huyu mtu anae jigamba amefanya nini katika kusaidia maendeleo ya nchi isipokuwa yeye anapeleka watoto wake ulaya kusoma ili waje kuwatawala maskini ya mungu bora hao wakoloni weupe kuliko wakoloni weusi naona shida imezidi mara 100 kuliko hapo nyuma
 
mimi kwa upande wangu naona hakuna mafuta ila ni porojo tu na kama yangekuwapo naona yangechimbwa zamani inchi inazidi kufa na kunufaika ni wachache tu walio wengi wanakufa na njaa wanangojea ifiki siku ya uchaguzi wawauo wenziwe ili apate tonge mimi binafsi siamini kama yapo mafuta labda naamini upo ukimwi tu huo ndio unotosha kuleta maendeleo ya vifo hakuna maji je?mafuta tusiwe tunajidanganya yakiwepo ni vizuri ndio tuombavyo leo yawepo mafuta ungeona america atakavyo lete fitna zake mimi sina uhakika na suala hilo
 
jamani hayo mambo makubwa kwani nyerere hakujua kama zanzibar ni ndogo tangu lini mtu mzima akafanya urafiki na mtoto si anataska kumuharibu mimi napenda kudumisjha muungano kitakacho patikana kigawiwe 50/50 sio huyu achukue asilimia 60 huyu 40 huo ni muungano au uzushi bora watu wagawane mbao
 
mimi siamini kama muungano huu ulivyo kama utadumu iko siku tu naamini utavunjika ipo siku na watu wa bara wataanza kupiga kelele japo wamelala na kunywa mataptapu itakuwabalaa siku hiyo
 
Inawezekana mwaka 1964 wakati muungano huu unaasisiwa, mpangilio ule ulionekana kuwa sahihi kwa vile waasisi walikuwa hawana uzoefu na uendeshaji wa nchi. Nyerere alikuwa na miaka mitatu tu madarakani wakati Karume alikuwa na miezi mitatu tu. Baada ya kuishi katika muungano huo kwa zaidi ya miaka 40, tumejifunza mapungufu mengi katika muundo huo. Ingekuwa ni vizuri sana tukayarekebisha mapungufu hayo ya muungano ili kuuimarisha. Tatizo lililofanywa na viongozi wetu ni kuchukulia kuwa makubaliano ya mwaka 1964 yaliyofanyika katika muda usiozidi siku mia moja tu huku yakiongozwa na watu wasiiokuwa na uzoefu wowote wakati ule eti hayana na kasoro yoyote: hayo ni makosa makubwa sana
 
Kwa nilivyowahi sikia mimi ni kuwa muungano huu Karume aliutaka kwa muda wa miaka 10 tu - sasa huu muungano wa kupeana muda maalumu sijui muungano gani?
 
Under_age,

Tena nashukuru sana unaposema kwamba Zanzibar leo hii watu hawatazamani kwa rangi zao... hii ni alama kubwa sana na mafanikio ya Mapinduzi yale. Na kama umewahi nisoma mara nyingi mimi sipendi kabisa tunapo jadili kitu kwa kuzitazama nafsi zetu, rangi zetu, jinsia zetu bali hupenda kujadili issue zinazotuhusu sote kwa ujumla.

Mkandara,

Huo ubaguzi wa rangi haujawahi kukuwepo Zanzibar kabla wala baada ya Mapinduzi - Ubaguzi wa rangi haujawahi kukuwepo Zanzibar kwa hiyo sio alama kubwa ya Mafanikio ya Mapinduzi yale.Hata hao wafalme ambao waliwahi kutawala Zanzibar kwa kuwaangaia tu huwezi kusema ni waarabu rabda kwa vilemba na majoho yao ndio utaweza kuwaita waarabu lakini sio rangi na nywele zao.


Barghash%20and%20advisors.jpg

hawa ndio waflme wenyewe - huwezi kuwatofautisha rangi zao na wazanzibari (wanzanzibari ni watu waliochangaya damu sana, so huwezi kuwabagua kwa rangi zao)


Tippu.jpg
Na huyu nae alikuwa mweusi kwa maana ya weusi haswa

Zanzibar kulikuwa na ubaguzi wa kikabila ambao uliletwa na Mkoloni Muingereza ili iwe rahisi kwake kuwatawala wananchi wa Zanzibar. Kulikuwa hata na maskuli ya kikabila yaani wangazija walikuwa na skuli zao, wahindi pia walikuwa na skuli zao, waarabu nao walikuwa na skuli zao waafrika walikuwa na skuli zao

Na ubaguzi mkubwa ni ule ulianzishwa na CCM kwa kuwafukuza kazi wale wafanyakazi wenye asili ya Pemba na kuwanyima haki zao nyengine

kwa hiyo mimi naona mafanikio ya Mapinduzi kwa upande wa rangi hayapo hata kidogo zaidi wao ndio wanaawabagua watu kwa jinsi ya rangi zao, yaani wakimuona mtu mweupe tu wao humwita muarabu (HIZBU) yalimkuta Dr. Salim
 
Kwa nilivyowahi sikia mimi ni kuwa muungano huu Karume aliutaka kwa muda wa miaka 10 tu - sasa huu muungano wa kupeana muda maalumu sijui muungano gani?

Hii nilikuwa sijaisikia, kama ni hivyo basi aliuwawa miaka miwili kabla hajatimiza azima yake ya kumaliza muungano huo katika miaka kumi.

Kuna stori niliyosma siku za nyuma sana kuwa baada ya mapinduzi na Babu kushirikiana na Karume, Marekani ilikuwa na wasiwasi kuwa uhusiano wa Babu na China ungesababisha Zanzibar iwe nchi ya kikomunisti kutokana na kuwa Babu alikuwa msomi zaidi ya Karume na angeweza kufanya maamuzi mengi. Kwa vile wakati huo Nyerere alikuwa hajajitangaza kuwa mjamaa, basi wakashinikiza Zanzibar iungane na Tanganyika ili kunyutralize makali ya Babu katika siasa za Zanzibar. Hata hivyo Babu alipofika kwenye serikali ya Nyerere akashibana Nyerere kuhusu uchumi wa kijamaa kiasi kuwa Nyerere alimfanya kuwa Waziri wa Mipango na Uchumi. Ingawa walitofautiana sana kwenye approach, lengo lao lilikuwa moja. Kama waziri wa mipango, Babu akatumia connection yake na China kufikia makubaliano ya kujenga Tazara, na kiwanda cha nguo cha Urafiki. Kwa hiyo wamarekani walioshinikiza muungano ule kwa kumwogopa Babu na ukomunist wakawa bado hawakufanikiwa malengo yao.
 
Hii nilikuwa sijaisikia, kama ni hivyo basi aliuwawa miaka miwili kabla hajatimiza azima yake ya kumaliza muungano huo katika miaka kumi.

Mwl Kichunguu,

There was also a period when the government stopped importation of food and encouraged self reliance. Some allege that the govermnent used foreign currency to import large arsenals of weapon in preparation for the eventual pull out of Nyerere's support. It is claimed that the union was originally planned for only 10 years and was to end in 1974.


source: http://www.zanzinet.org/zanzibar/history/historia.html#kifokarume
 
Ukiwasikiliza wazanzibari utachanganyikiwa.madai yao ni zaidi ya laki moja hasa ukikaa kwenye vijiwe vya kahawa.Mpaka sadani wanadai iko zanzibar ndio maana hata kwenye TV hawaonyeshi hali ya hewa ya huku bara lakini sadani wanaionyesha.Kero za muungano kero za muungano hakuna kero yeyote.Hayo mafuta hayajapatikana wanataka kupwewa mgao wa dhahabu ya shinyanga.je yakipatikana.jamani tujaribu kuwa wakweli zanzibar watu si zaidi ya milioni moja.baadhi wengi wao wanaishi huku bara mpaka vijini huko hakuna anayemzui mzanzibari katika shughuli yeyote.wengine wameajiriwa bara kama vile ni wabara.fedha za kigeni wanatumia za bara kununua mahitaji yao nje lakini wao hawana export kubwa yote haya hawaoni.lakini ukisikiliza manung'uniko yao utadhani bila zanzibar bara hakuna kitu kumbe ni kinyume chake.mimi ninaona hakuna haja kuwa na nci mbili zanzibar iwe ni mkoa/mikoa.
 
Ukiwasikiliza wazanzibari utachanganyikiwa.madai yao ni zaidi ya laki moja hasa ukikaa kwenye vijiwe vya kahawa.Mpaka sadani wanadai iko zanzibar ndio maana hata kwenye TV hawaonyeshi hali ya hewa ya huku bara lakini sadani wanaionyesha.Kero za muungano kero za muungano hakuna kero yeyote.Hayo mafuta hayajapatikana wanataka kupwewa mgao wa dhahabu ya shinyanga.je yakipatikana.jamani tujaribu kuwa wakweli zanzibar watu si zaidi ya milioni moja.baadhi wengi wao wanaishi huku bara mpaka vijini huko hakuna anayemzui mzanzibari katika shughuli yeyote.wengine wameajiriwa bara kama vile ni wabara.fedha za kigeni wanatumia za bara kununua mahitaji yao nje lakini wao hawana export kubwa yote haya hawaoni.lakini ukisikiliza manung'uniko yao utadhani bila zanzibar bara hakuna kitu kumbe ni kinyume chake.mimi ninaona hakuna haja kuwa na nci mbili zanzibar iwe ni mkoa/mikoa.


wacha kubwabwaja wewe
 
Back
Top Bottom