Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,191
- 677
mie muafaka nnautaka , ila hujiuliza muafaka kwa hali hii utawezekana?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zanzibar haitapatiwa muafaka mpaka CCM watakapo amua kuacha ujambazi wao.
source : http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/9/21/habari5.php#WANANCHI wa Zanzibar, wameanza kuwasilisha malalamiko yao Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, na miongoni mwa watu wa mwanzo kulalamikiwa ni Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansour Yussuf Himid.
Waziri Mansour amefunguliwa malalamiko hayo mbele ya tume hiyo, akituhumiwa kuvamia eneo la ardhi la Abdallah Ahmed Sharif (80), liliopo kando kando ya bahari ya Hindi, huko Buyu Wilaya ya Magharibi, Unguja.
Kamishna Mkaazi wa tume hiyo Zanzibar, Safia Masoud, alithibitisha kupokea malalamiko hayo na tayari tume hiyo imeanza kufanya uchambuzi na itahakikisha inawasiliana na waliolalamikiwa ili nao wasikilizwe kabla ya kutolewa maamuzi.
Katika barua ya malalamiko, ambayo Tanzania Daima ina nakala yake, mzee Sharif anasema amesikitishwa na kitendo cha Waziri Mansour kuvamia eneo lake la ekari 10 bila ya kuzingatia sheria za umiliki wa ardhi.
Alieleza kwamba kitendo hicho kimefanyika huku viongozi wengine ambao wametakiwa kuondoka kwa amri ya mahakama katika eneo hilo, wakiwa hawajatekeleza amri hiyo kwa zaidi ya miaka 17 tangu maamuzi hayo kutolewa na Mahakama ya Rufaa Tanzania, katika kesi iliyofunguliwa 1989.
Njama hii ya kuingilia haki yangu kikatiba inaendelezwa na Mheshimiwa Mansour Yussuf Himid kuchukua sehemu ya pwani ya shamba hili, alilalamika mzee Sharif.
Alisema kwamba baada ya kupokea taarifa ya shamba lake kuvamiwa na Waziri wa Ardhi, alikwenda kuthibitisha katika eneo hilo na kuchukua hatua ya kukutana naye ili kujua nani aliyemruhusu kuchukua eneo lake bila ya ridhaa yake.
Nilipoenda kuonana naye ofisini, aliniarifu kuwa yeye amethibitishiwa na uongozi wa wizara yake na wa CCM eneo la Shakani, hususan Khatib Abdallah Makame na Sheha wa eneo hilo, Yahya Matar na uongozi wa wilaya kuwa, sehemu hiyo ni ya serikali, alisema.
Sharif alisema kwamba kitendo hicho kinamvunja moyo kwa vile Waziri wa Ardhi alitakiwa kusimamia haki yake.
Katika shamba hilo, mbali na Waziri Mansour, pia viongozi kadhaa wameamriwa na mahakama waondolewe, na nyumba zao kubomolewa baada ya kushindwa katika kesi Mahakama ya Mkoa, Mahakama Kuu Zanzibar na baadaye Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Baadhi ya viongozi walioamriwa kuondoka na nyumba zao kubomolewa ni Mshauri wa Rais Karume Mambo ya Mazingira, Abdallah Rashid, aliyekuwa Mkuu wa Usalama wa Taifa Zanzibar, Mohammed Hija, mfanyabiashara maarufu Zanzibar, Edward Kissasi na aliyekuwa Meneja wa hoteli ya kitalii ya Reef.
maalim huyu hujui kuwa yy ni CCM damu?
mie utaifa kwanza halafu ndio mengine, zanzibar ni taifa lilokubali kuingia kwenye muungano kwa ridhaaa.
sasa ni juu ya chama chochote kinachotaka kuniconvice mimi ni kuja na suluhisho lamaana.
hivi huhisi kuwa inakera kila siku kupingana kwenye mambo madogo madogo.