Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa Mataifa mawili na si idadi ya watu. Kihalali mgao wowote ulitakiwa uwe 50/50

Nchi moja inakuwaje na serikali mbili bwashee?!
Ndiyo ilivyokuwa. Zanzibar na Tanganyika ziliungana na kuwa nchi moja yenye Serikali 2, ile ya JMT na SMZ (Katiba ya JMT inasema hivyo, siyo mimi)

Sasa hivi ,Katiba ya Zanzibar inadai Zanzibar ni "nchi" yenye serikali yake na "inapakana"na JMT;

Huku Katiba ya JMT inadai Tanzania ni "nchi" yenye Serikali mbili, na "Zanzibar ni moja ya eneo lake".
 
Kulipa pia 50/50
 
kijamii...zanzibar tumeingiliana nao zaidi ya 200yrs. Ni nini faida yake Kwa sasa?
 
kisiasa...pamoja tunaunda taifa kubwa
ulinzi imara wa taifa, ukubwa wa eneo ni uimara wa ulinzi? Watanganyika tumelogwa
 
N
Ni nini faida ya Muungano kwa mfanyakaxi wa umma, mkulima, mfugaji, mvuvi, Mchimbaji madini, au mfanya biashara wa bara?
 
Wanaoanzisha hii hoja huwa hawana akili. Kwenye kulipa mbona hamtumii formula ya 50/50?
 
Jo kuna wakati nadhani zinakutoka kidogo..sina hakika NADHANI
 
Mkuu ninakubaliana na kauli yako, ila huoni wazanzibar wanatuona mazuzu Sisi watanganyika?
Kuna maoni kinzani: Kuna maoni huku bara kwamba Tanganyika imepotea na kumezwa. Lakini upande wa visiwani wanadai Tanganyika ipo ila imevaa koti la Tanzania yaani Tanzania ndiyo Tanganyika yenyewe tofauti ni jina. Kwa hiyo, kisemwacho upande wa bara kinapingwa upande wa visiwani.

Bara ukisema tunawalisha visiwani, visiwani wanadai wangekuwa peke yao wangekuwa kama Dubai.

Sasa hapo zuzu ni nani, inategemea upo upande upi๐Ÿ˜„
 
Mazuzu ni sisi bara. Wewe unakwenda kuungana na maskini unatarajia nini kama Sio mlolongo wa maneno.
Kuungana ni kuungana kiuchumi Ili wananchi wafaidike na huo muungano,
 
Tunaungana na pemba. Sasa niambie pemba mnataka nini kule?wapemba wenyewe wameshaikimbia pemba wanaishi Oman.
 
Simple mathematics , kuuvunja Muungano ni kuiondoa CCM madarakani.
I
 
Nchi mbili ziliungana kuwa nchi moja. Baada ya hapo pato la taifa linapaswa kugawiwa sawa kwa raia wa nchi mpya Tanzania. Iwe ni pato la ndani, misaada au mikopo, kama sio kwaajili ya mradi fulani wa eneo fulani, basi pato hilo lapaswa kugawiwa sawa. Lakini pia nchi yaweza kukopa kwa ajili ya kujenga mradi Fulani eneo fulani tuu, eg. kujenga airport chato (๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€๐Ÿ˜€), kujenga hospitali Kigoma, kujenga barabara Kilimanjaro au kujenga bandari Pemba etc. Haiwezekani tukope say trillion 10 kuboresha elimu Tanzania, halafu tupeleke visiwani trillion 5 ambapo Kuna raia million moja na nusu tuu, na bara nayo ipate trillion 5 wakati idadi ya raia huku ni karibu million 60.
 

Huo si muungano ni uvamizi uliopewa Jina la muungano. Tanganyika chini ya utawala wa Laanatullahi Nyerere iliivamia Zanzibar Na kuuwa maelfu ya watu Na kuifanya Zanzibar ni koloni lake.
 
mkuu angalia tu usijedhani unajipendekeza kumbe ndionunazidi kuharibu.
 
Hizi Mada wanatoaga watu ambao Ni attention whores,, endeleeni kuziibua ibua tu,,,kuna siku mtakipata mnachokitafuta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ