Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Your English shows clearly how much you hate our real enemy!
 
Majibu anayo nani?

Inakuwaje wakuu kama kina Lukosi wanauliza maswali haya?

Kama ipo, Nani mwenye siri ya muungan huu? Kina Mwanakijiji wanaochambua mambo wanaandika meengi na tuanayajadili, lakini hakuna jawabu la uhakika hadi leo? Au wanaoujua (wakiwemo CCM) wanaogopa kusema ukweli, tuwasaidie?

 
Kwa watetezi wa muungano kutoka Zanzibar wao wana kila sababu za msingi kuutetea muungano kwani wana fursa nyingi tu huku Tanganyika kwani Mzanzibar anaweza kumiliki ardhi sehemu yoyote ile ya Tanganyika, anaweza kuchagua au kuchaguliwa popote pale ikiwa ana vigezo na mambo mengine mengi tu yanayohusu haki za kiraia. Sasa nataka kujuwa nyinyi watetez wa muungano huu kutoka Tanganyika mnaodai kwamba muungano una faida kwetu sisi Watanganyika naomba kujua unatufaidisha na nini ikiwa Mtanganyika haruhusiwi...
 
...kumiliki ardhi huko Zanzibar, hana ruhusa hata kuchagua au kuchaguliwa, ubaguzi unaofanywa na wazenj kwa watanganyika waishio huko (ushahidi ninao kwani nina ndugu zangu huko). Narudia tena nifahamisheni faida tuzipatazo watu wa Tanganyika kupitia muungano huu wa kinafiki. TANGANYIKA KWANZA MUUNGANO BAADAE!
 
hakuna hasara, wala faida kwa muungano kuvunjika, sasa kuna umuhimu gani wa huu muungano kuwepo, Kwa faida ya nani.
leo hii baada ya kujadili katiba kwa niaba ya mtanzania maskini, katiba imekuwa no muungano mara serikali 3 na 2, Kwa manufaa ya nani, nini faida ya serikali 3 au 2 Kwa mtanzania masikini. acha muungano uvunjike kila mtu awe na serikali yake mambo yaendelee... leo hii wanasiasa wameiteka katiba, hawazungumzii tena yale ya maana kwa mtanzania masikini ila utasikia ooooh muungano, mara serikali tatu upumbavu mtupu.. TUAMKE WATANZANIA TUJIKOMBOE WENYEWE, TUSITEGEMEE KUKOMBOLEWA NAWANASIASA, TUWAKATAE ANZA SASA ULIPO GAP LA UMASIKINI NI KUBWA.

changia ili tujikomboe... tujengane kihoja na mawazo yaliotukuka.
 
Muungano wa serikali tatu una faida kuu za kiusalama. kubwa ni kwamba kwa hali ya kisiasa zanzibar kuna uwezekano mkubwa kutokuwa na stable government na baadae kutuletea shida bure
 
zile haki zote za kiraia kwa warioba zina faida kwa znz zaidi, maana haki ya kumiliki ardhi nani ataacha kiwanja dar au pwani akamiliki unguja ambako ni bei juu zaidi? nani ataacha vyuo au hospitali tanganyika aende kutibiwa unguja? labda awe yuko huko huko visiwani. na visiwani ajira kuu ni upishi na uhudumu kwenye mahotel na ulinzi sasa hapo kuna nini?
 
na kwakuwa cuf ni pemba na ccm ni unguja maeneo mengi watasumbuana sana, inaweza kuwa kama somalia.ikawa badala ya kujenga uchumi tunapeleka majeshi kulinda magaidi
 
Mkuu kwanza heshima yako, pili pole na kazi, tatu Shusha Munkari. Muungano ukivunjika zitapatikana nchi Mbili (1.Tanzania bara a.k.a Tanganyika; 2. Zanzibar): Baada ya hapo dhambi hiyo itawagawa Wazanzibar kwenye makundi mawili (WazanziBARA na WazanziBARI); Hawataishia hapo watasema Sisi ni Wapemba na Hawa ni Waunguja (Nchi mbili tena hapo UNGUJA na PEMBA). Kwahiyo Mkuu ili Unguja iwe salama (Watafanya kama Crimea walivyopiga kura kuomba kujiunga Rusia) wataomba kujiunga tena na Tanzania bara (Tanganyika). Dhambi hii itatusumbua sana.
 
Vunjilia mbali muungano waanze match ya zenj vs pemba
 
Muungano wetu unatikiswa kwa hoja ya serkali 3, lakini tukiwa na serikali 2 Tutadumu kwa miaka 50 mingine.

Naombeni tuunge two government system reformed.
 
Muungano wetu unatikiswa kwa hoja ya serkali 3, lakini tukiwa na serikali 2 Tutadumu kwa miaka 50 mingine.

Naombeni tuunge mkono two government system reformed. Muungano wetu uendelee kudumu.
 
Kwakuwa wazanzibar ndo wako mstari wa mbele kutaka kuvunja muungano ilihali wakijua wao ndo watakua waanga wa kwanza kudhulika kwa kuzidi kubaguana pemba na unguja, wazanzibar na wazanzibara... ni sawa na mtoto kulilia wembe...

Me nasema bora tuwape visiwa vyao ili watupunguzie makelele yao make washakua kama mbu za usiku wa manane zikoseshavyo usingizi.... achana nao wakachinjane huko baharini...

Tumechoshwa na kelele za vijukuu vya sultani.
 
Te!te!te!te!mbona mikelele imekuwa mingi humu jamvini?hiyo mikelele yenu mlikuwa mukaipige kwenye kaburi la nyerere coz ndie aliesababisha upotevu wa tanganyika,zanzibar haihusiki na upotevu wa tanganyika kama vipi fufueni tanganyika yenu kwanza ndipo mupige hiyo mikelele.
 
Muungano wetu unatikiswa kwa hoja ya serkali 3, lakini tukiwa na serikali 2 Tutadumu kwa miaka 50 mingine.

Naombeni tuunge two government system reformed.

Mbona tangu 2010 muungano ulishavunjikaaa???
 
Nadhani mleta hoja umeuleta uzi huu kwa jazba .

Kama msingi wa jukwaa ulivyo,tunatakiwa kujenga hoja na siyo jazba

Unaposema muungano uvunjike halafu nini .

Funguka kwa hoja nzito
 

Nakushanga bro kuwa hadi leo unamuabudu nyerere!badilika.
 
Watu wanaunganisha nchi mbili au zaidi wewe wasema huutaki muungano.Tafakari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…