Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibar: Una faida gani na kwa manufaa ya nani?

Heshima kwako LAT

Mkuu ebu tupia macho na hiki kipande,choko choko zote unazosikia kutoka Zanzibar ni mafuta hawataki kugawana na ndugu zao wa Bara kichekesho ni uwepo wenyewe wa mafuta !.

Mafuta Zanzibar yataligawa taifa
 
Sisi wa bara hatutaki Muungano. Kwanini katiba ya zbar inasema zbar ni nichi? Wenyewe hawataki. Nasi hatutaki. Wanaupigia debe ni wabunge wa zbar akina hamad Rashid na majina yao bandia ndo wanaupigia debe. Ama wapemba wanaofaidi huku bara. Vinginevyo Tusidanganyane muungano ni hasara kwa bara.

Hata sisi tunaotaka muungano pia ni wabara japo tunaweza kutofautiana mikoa tunayotoka. Sasa kama Zanzibar wamekuwa na Raisi, Bunge na Mahakama katika kipindi chote cha muungano na wamekuwa na katiba yao si ingekuwa ni ajabu kama wangeshindwa kuitwa nchi.
 
ngongo ..... jambo usilolijua ni swasawa na giza .... kuuliza si ujinga bali ni kuelimika .... nisingelijua jambo hili kama nisinge soma bandiko lako na pia sikuishia hapo tu bali nikaendelea kuomba mwongozo wa ufafanuzi kutoka kwako na kusisitiza kwamba ni kwa manufaa ya wengi .... nashukuru kwa mara nyingine tena

Heshima kwako LAT,

Mkuu hii ndiyo raha ya JF.Ukisikia kelele za Maalimu Seif and Co ujue ni fitina za mafuta hawana karata nyingine zaidi ya mafuta utashangaa likifika suala la mafuta hakuna CUF wala CCM wote wanajitambulisha kwa uzanzibar balaa ni kwetu sisi huku bara hatuungani kupigania maslahi ya Tanzania bara tunakubali kugawanywa na uCCM na uCHADEMA.Ikafika mahali wabunge wa CCM,CHADEMA,UDP na nk wakasima pamoja bila kujali itikadi za vyama vyao ni na hakika Tanzania ingefaidika na madini yake,mgao wa umeme ungekuwa history,mafisadi bila kujali wanatoka chama gani wangeshughulikiwa na nk.
 
Muungano huu hauna faida yoyote kwa upande wa zanzibar unaishi kutokana na kikundi cha CCM kwa wazanzibar wenyewe muungano wanaushukulia kama ni ugonjwa mbaya wa Ebola na wanatafuta kila dawa kuuwa lakini hau- exist tena.

Kwanza muungano huu ni fake hakuna nchi hata moja duniani zilizo ungana bila kushirikishwa wanainchi wapande hizo mbilia.)
B.)Muungano huu wazanzibar wanaushukulia ni wakisiasa sio wa hiari

c.)Muungano umepoteza heshima na uaminifu pale nyerere alipokaa itisha bunge la tanganyika na kukaa na watanganyika wenzake na kuuvunja katiba ya tanganyika na tanganyika yenyewe bila kuwashirikisha wazanzibar wakati ni tanganyika ndio mshirika na zanzibar na sio tanzania.


Kwahiyo kwa upande wa zanzibar muungano umepoteza uhalali wake kwa hio ni batli na fake,na mabadiliko ya hivi karibuni ya baraza la uwakilishi zanzibar kupitisha kipengele cha kuwa zanzibar ni nchi ndio haya nimalipo ya kuvunja mkataba mama artcle of union na kujivisha koti la tanganyika kuwa tanzania ujanja mwingi mbele kizaa.
Sisi tunarudisha hadhi ya nchi yetu kama mwanza kabla ya muungano zanzibar ilikuwa nchi au mkoa jiulize hivyo? Kwahiyo katiba ya Zanzibar imerudisha uhalali wa nchi yake.
 
kama ni swala la muungano tanganyikia na visiwani wanatakiwa wote wanufaike-naona umeeleza jinsi wapemba wanavyonufaika huku tanganyika-inawezekana watanganyika hawanufaiki na kitu visiwani
kuliko huu muungano uwabebe wazanzibari-ni bora uvunjwe hata leo

Manufaa ya Kijamii na Kiuchumi yanatokana na jinsi wana-nchni husika wanavyochangamkia fursa na uwezo wao wakuona fursa, Wabara labda wanachelewa kuona fursa za kutumia zenj, sina uhakika.

Lamsingi ninaloona ni kuweka siasa mbele kuliko mambo ya uchumi na Mandeleo ya kijamii. Uki-evaluate Politically ni kweli haufai maana tena juzi nimesikia wanachoma baa za watu huko, sasa hayo yote ni kwa sababu vingozi wetu wanafanya siasa katika kila kona za Muungano huo.

Kama tukiacha siasa na kuishi kama nchni mbili, kuna fursa za Maendelo kwa pande zote mbili.
 
Lengo la muungano la Nyerere na watanganyika wenzake nikuimeza Zanzibar. Upole na ukarimu wa viongozi wetu wa CCM ndio ujinga na upumbavu wanavyo onekana na wenziwao wa ccm/bara.

Jee ikiwa sera ya ccm/smz ni serekali mbili kuelekea moja zanzibar ina nafasi gani ktk serekali ikiwa moja? (2-1 =1)?.

Mimi nahisi tumefika wakati tuwashuhulikie viongozi wetu wa ccm/smz kuwakata roho otherwase wataipeleka nchi pabaya na kuja kujuta na kukitia kizazi cha wazazibar machaka kwa ulafi wao na kuwa na akili finyu?.

Pinda,chadema, wote ni ndugu wa tanganyika na lao ni moja ktk kuimeza zanzibar kimpinu ikiwa pinda anataka kuipigu katiba ya z'bar nani aliomkataza kuirudisha katiba yao ya tanganyika kwa maslahi ya watanganyika? Mimi siamini kuwa katiba tulionayo ni ya muungano?.

Hii ni katiba ya tanganyika na kuna kila dalili kuwa ni yao hata simbul za nchi adam na hawa ni nembo ilokuwa ya watanganyika haikubadilika ni wazanzibar kutaka kupelekwa pata potea tu.

Mimi nasema tusiwe na muhali na ccm-smz kutulisha matapishi ya watanganyika imefika wakati kupiga kura ya maoni na kulizwa wananchi kuwa muungano uendelee au la. Kama upande moja utasema hautaki sio kitu cha kulazimishana.

Chadema kipindi kirefu wanasema kuwa mabadiliko ya katiba ya zanzibar yamevunja ilani ya katiba ya muungano kuwa lengo ni serekali 2 kuelekea 1.

Nyiyi watanganyika munawazimu munazani wazanzibar ni wepesi kumezwa ktk tumbo la tanganyika ambayo ni tanzania? Yaguju.

Kama zanzibar imevunja katiba ya muungano nyiyi mulipo vunja tanganyika na katiba yenu na mukavaa koti la tanzania hamukuvunja mkataba wa muungano? Katiba ya zanzibar 1984 imesha asirika zamani kwanza ni pale katiba inaposema ili uwe raisi wa zanzibar nilazima wazazi wako wawili baba na mama wawe ni wazaliwa wa zanzibar jee ?mzee kondom ali hassan mwinyi na mtu ni kwao abudu jumbe ni wazaliwa?

Kwa hio hapa nyerere alituvunjia katiba yetu kutuwekea watanganyika kututawala zanzibar wakati katiba yetu haikubali kuwa rais wa zanzibar kama sio mzaliwa wa zanzibar hii sio kuvunja katiba ya nchi yetu?

Mimi naona suala la muungano musilingaganie kuwa nilazima tuwe na zanzibar muna nchi yenu tuna yetu mukitaka kushanganya damu muwe wazuri njoni zanzibar tutawashuhulikia?. Mutapata vitoto vya rangi x2 na nyele laini
 
  • Hoja binafsi kwa wazalendo ipo mezani!
  • Operesheni megua muungano Zanzibar kuanza jimbo kwa jimbo!
Na: Malik Nabwa
Zamani mtoto akilia sana usiku tukimchombeza kwa nyimbo. Tukianza na nyimbo za kuchezea watoto kuanzia makwaya kwaya kamndindiliya, adi adi. Tukiona hanyamazi tunaimba nyimba za Samba. Kisha msewe, tarazia, kibandiko, boso, mbware, na kama mtoto bado hanyamazi tukimpiga ubeleko. Ndani ya mbeleko akiendelea kulia tukimuoshakwa maji maana tukidhani ana joto. Yakishindwa yote haya mtoto bado hasikii dawa na anaendelea kulia sasa tukimtisha kwa babu mduma. Zote hizi ni juhudi tu za kumreburebu mtoto anyamaze maana kilio ni ghasia na hunyima watu raha.

Na muungano wetu wa Tanzania ni mithai ya mtoto mlizi. Tumekwisha kila rai kuutaka Muungano huu ama uondoke, au basi angalau urekebishwe ili unufaishe sehemu zote mbili sawasawa lakini wapi?. Juhudi hizi zimeshindikana. Tulitaka muungano uangaliwe upya, tukaonekana tunabwabwaja tu. Tukataka tupunguziwe mambo ya Muungano yasio na faida bado kimya. Baya zaidi Raisi wetu aliepo madarakani kila jambo analoletewa na wasaidizi wake husema hilo ni la Muungano kwanza nalipitie bara huko ndio lijadiiwe hapa. Tumeona hivi karibuni jinsi mamilioni ya Brunei yalivyorudishwa hivi hivi kwa Rais kukataa nchi hiyo kuisaidia Zanzibar kama nchi akisisitiza kupitia Muunganoni kwanza. Kwa haya machache na mengine mnayoyajua na kuyaona kwa mato yenu ni dalili tosha kuwa njia mbadala ya kujinasua haipo.

Kumwaga damu haina haja na si katika njia nzuri ya kudai haki iwapo haina ulazima. Tulishajaribu ikashindikana mara moja hiyo. Lakini kwa sasa kuna njia mbadaa ya kuutumia umma wa Zanzibari kuitatua hili. Ninaposema nguvu ya umma sikusudii tuandamane, la hasha. Katika Operesheni Megua muungano visiwani hatukusudiii kabisa kuingia barabarabani. Bali tutatumia utaratibu sahihi wa sheria na katiba ya nchi na tukishikamana kiukwei basi tutafanikiwa muda si mrefu. Wazalendo wenzangu, kampeni MEGUA haina nia ya kuuvunja muungano. Neno MEGUA maana yake kuunyofoa nyofoa kidogokidogo mpaka tukajua moja. Kupata haki yetu au kuufanyia marekebisho Muungano huo ukawa wa manufaa zaidi kwa kila mmoja wetu. Ikishindikana hivyo tutaendelea kuumegua hadi tuumalize. Nyumba isiyo nguzo haisimami, na hii ndio falasafa ya Operesheni MEGUA. Na ili tuuangushe huu ni kuumegua nguzo zake muhimu.

Operesheni megua itaendeshwa na wazaendo wenyewe. Haitagharimu hata senti kumi lakini itahitajai umakini na kujitolea kulikotukuka. Operesheni hii itafanyika katika kila jimbo.Zanzibar ina majimbo hamsini na wawakilishi hamsini pia. Shida yetu juu ya hili sio wabunge bali ni Wawakilishi. Kwa vile katiba ya Zanzibar inaruhusu wananchi kupiga kura ya maoni juu ya kila mabadiliko ya katiba Operesheni MEGUA itakitumia kipengee hiki kukusanya maoni ya wananchi katika kila Jimbo kuhusu jambo moja moja la Muunagano ambalo wananchi hawalitaki. Tutaandaa barua rasmi (Muundo na kiambatisho kitawekwa hapa baada ya wazo hili kupitishwa na wazalendo) itakayaopelekwa kwa mwakilishili wa kila jimbo baada ya kupata ridhaa za wanajimbo na sahihi zao kuhusu kukubali au kukataa jambo Fulani la Muungano.

Baada ya maoni ya wananchi katika kila jimbo yakipata kuungwa mkono barua hiyo na dodoso yenye orodha ya wanajimbo walio wengi kutia saini kutokubali suali hilo kinachofuata hapo ni kumpa barua hiyo na dodoso Mwakilishi na kumtaka alifikishe wazo lile au hoja hile jumba la kutungia sheria huko Mbweni; yaani Baraza la wawakilishi. Zoezi hili litakuwa gumu lakini likisimaiwa vizuri linaweza kuleta athari kubwa sana katika jamii zetu. Itakapofikia hatua tukapata angalau majimbo 30 tu yakafanikisha zoezi hili na barua hizo kuwasilishwa mikononi mwa Wawakilishi huku baadhi ya kopi zikiwekwa kama kumbukumbu kwa taasisis za kiraia na zile za Kimataifa basi utakuwa tumefanya kazi kubwa. Kitakachobakia ni kwa Wawakilishi kusuka au kunyoa. Ni juu yao kuamua kuyafikisha maoni yetu kunakohusika au kuyakalia na kutoyafanyia kazi, ili kusubiri tuwaoneshe hasira zetu kwa kutowachagua au hata kuwaengua nyadhifa zao kwa kushindwa kutufikishia matakawa yetu kunakohusika.

Katika fomu hiyo tutaorodhesha baadhi ya mambo ya muungano ambayo kwa sasa lazima yaondolewe kama mambo ya Muungano na kuachwa kuwa chini ya nchi husika; Zanzibar na Tanganyika. Mambo kama vile TRA, bandari, Mafuta, NECTA, na Mambo ya Nje n.k yatakuwemo katika dodoso atakayoulizwa mwana jimbo na kutoa maoni yake.Lakini kabla ya huko ni nafasi yako mzalendo kutoa maoni yako juu ya hili.
Wazalendo, mnaonaje wazo hili? Linafaa? Tutaweza? Nasubiri maoni yenu. Sina mengi leo!
Wakatabahu
Nabwa
 
Asante ndugu Malik kwa mchango huu wako. Ama kwa kweli, asilia mia 70 ya wazanzibari hawataki muungano. Takwimu hizi zimetokana na utaratibu uliyofanyawa na NGO fulani hapa Zanzibar siku chache zilizopita. Wazanzibari wengi wamekwisha amua na maadamu Jamii Forums ipo hai, wakuu wengi wa bara wataipata habari hii. Wazanzibari wamechoshwa na Muungano.
 
Kazi imeanza, sasa tuuvunje muungano ama?
 
abdulahsaf,

Elimu ya umma haina mwisho, mimi nitaendelea kuwasaidia Wanzanzibar kujitambua na kuchanganua mambo.
Kama Mwinyi/ Aboud Jumbe ni Watanganyika: Abeid Aman Karume ni Mnyasa kwa taarifa yako. Sasa kama unawakataa Mwinyi na Jumbe ambao ni miongoni mwa Wanamapinduzi 12 waliohai unayakataa mapinduzi ya nchi yako.

Salim Ahmed Salim: Ndugu yangu acha unafiki, mwenyezi Mungu hapendi, kanisa halina mkono, ni habari zilizozushwa hivi karibuni, na kwa uduni wa kuelewa, kusoma na kutambua mambo Wznz wanaimba wimbo huu. FACTS: Wajumbe wote wa Halmashauri kuu NEC ya CCM walimkubali na kumtaka Salim A Salim. Walioleta fitna ni wajumbe wa ZNZ waliosema eti ni Hizhbou. Wakasema ana damu ya Uarabu, na alishiriki mauaji ya Karume. Fitna hizi ni kutoka kwa wazanzibar wenyewe. Hakuna Mbara anayejua Hizbou ni nani, ila waunguja na wapemba. Salim alikuwa waziri mkuu wa Tanganyika, na waziri wa Ulinzi. Usiwadhalilishe Wnz

Hakuna anayelazamisha muungano. Tanganyika tumechoka kulipia watu umeme wa bure, kuwalipia mishahara na kuendesha serikali ya muungano. Sisi hatuna faida na muungano.
Ombi letu: Fungeni virago muondoke bara mrudi kwenye nchi yenu. 700,000 mnafanya nini bara? Ondokeni mkadai nchi yenu mkiwa kwenu.

Muungano ukivunjika Tanganyika wana lose nini? waulizeni Wznz kwenye mablog na website maana nimeuliza hili swali mara zaidi ya 100 hakuna mZnz anayejibu.
Znz if you think education is expensive try ignorance.
 
Naheshimu mawazo yako. Na pengine ndoto yako. Ushauri mdogo tu kwamba hadi kufikia hapo unapopatabiri ingekuwa vizuri uendelee kuiheshimu hiyo bendera kwa sasa.Maana bado inatuwakilisha sote kimataifa.
 
I never knew how EXTREMISTS were before, until i stumbled upon this overwhemingly ignorant Zanzibari man! Next time use a BRAIN to do all the thinking, otherwise you'll be steering youself very wrong. If you guys withdraw then cool, good for us! Take my word, the 1st thing you guys will do is REDUCE THE CONSTITUENCIES (only two willl do u right)!
 
Kumbukeni hadi vyakula mnachukua bara, so if you decide to go mtatupunguzia mzigo sisi, we got nothing to loose zaidi ya longolongo zenu, kwanza sijui ni nani anayewang'ang'ania, pack your things and go!! hebu angalia kuna wabara wangapi Znz comparing to Bara? mbona hamna shukrani nyie, au mnaona tukinyamaza ni kwamba tunawapenda sana? think twice, sisi ni kitu gani tunacho-import toka Znz? ni hizo used electrical devices zinazouzwa na wapemba wenzenu kariakoo?? usitake kuniharibia chai yangu asbh asbh hiv
 
Zanzibar is a time bomb!.
Tena wenye akili, waushukuru Muungano vinginevyo baada ya Mapinduzi, wangeendelea kuchinjana mwanzo mwisho!.

Naifuatilia kwa keen interest hii GNU ya CCM na CUF, juzi nimetoka huko nikawa surprised, kumbe viongozi wa CUF ndani ya GNU wanatekeleza sera za CCM!.

CUF ni kama mtoto aliyekuwa akilia kwa makelele sana ndipo baba CCM akampa peremende ya GNU alambe anyamaze. CUF kalamba kanyamaza, nasubiria utamu wa peremende utakapoisha kama mwana ataendelea kunyamaza!.

Hata hao Wanzazibari wanaolalama humu kuhusu muungano hawajui watendalo kwa vile ni muungano ndio unaowapa fursa za kuyafanya wanayoyafanya kwa kukohoa na kelele nyingi, nje ya muungano hawa wange vanish into thin air (wangeshafungwa mawe shingoni na kutoswa baharini).

Wazanzibari wenye muono wa mbali, wanamshukuru Julius vinginevyo wangeachwa walivyo hawa, zamani pale pangekuwa ndio ngome ya Osama na Wamarekani wangevizamishia mbali kabisa visiwa hivi vifutike kwenye uso wa dunia! Thanks to Muungano.
 
Nguruvi3,
Mkuu umemaliza kila kitu, facts ni kwamba watngnyka hawata-lose chochote kwani hawana investments zozote zenj! Nadhani pia watanganyika waanzishe 'operation ondoa wapemba bara' yaani wote kuanzia ujiji-kigoma hadi kigamboni, kila kukicha tunakutana na malalamiko yao tuu ambayo hayaeleweki, vijana wanasema kama noma na iwe noma! Kila black kwao si mzaliwa bali mwarabu yes-this z slave inferiority ambayo imejengeka visiwani na wanataka kuihamishia bara! Al adawi wakubwa hawa
 
Elli,

Halafu mkuu tena haya ma used wanayouza ndo yanaua sna uchumi wa bara! Wanatumia dola ku-import hata vile ambavyo havina matumizi kwa watz, an they export nothing ili kuingiza foreign earning-wapemba woooote now warejee chokocho kwao huko wakajenge nchi yao na watngnyika wote warejee umatumbini kwao-na vijana wa kazi watakaa ready ku-confiscate kila chumo la migrants wa either side-wanabebwa then wananyoosha miguu!
 
Zanziber ,mnataka kujitenga?
hata leo jitengeniii, maana nyie ni mzigo atiii, mkija huku shule zawashinda
 
Wapemba na waunguja walipokaribia kutengana kumbe wachawi walikuwa watanganyika mmmmmmmmh hii mpya.
 
Back
Top Bottom