Muungano wa Tanganyika na Zanzibari ukivunjika,na ukatokea mgogoro, mgogoro huo utasuluhishwa na mahakama ipi au mkataba uko kimya juu ya hili?

Muungano wa Tanganyika na Zanzibari ukivunjika,na ukatokea mgogoro, mgogoro huo utasuluhishwa na mahakama ipi au mkataba uko kimya juu ya hili?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Ni wazi wananchi wa pande zote za Muungano huu hawaridhiki na huu Muungano na ni wanasiasa ndio wanaoung'ang'ania kwa masilahi yao, hivyo ni swala la muda Muungano huu kuja kuvunjika au kuzua mgogoro mkubwa.

Swali langu ni je, Muungano ukivunjika na ukatokea mgogoro labda katika kugawana yaliyopatikana ndani ya Muungano(mfano ni ndege za ATCL), mgogoro huo utasuluhishwa na mahakama ipi?

Au hata hivi sasa ukatokea mgogoro wa kimasilahi huku kila upande ukidai kuwa na haki, mgogoro huo utasuluhishwa wapi?

Kwa maneno mengine, Mkataba wa Muungano unasema nini kuhusu mambo haya maana hata kizazi kijacho kinaweza kuja kukataa huu muungano.

Muungano huu utazamwe upya kwani lolote linaweza kuja kutokea huko mbeleni na tukumbuke msemo huu wa wazungu: "better late than never".
 
Back
Top Bottom