Mvua imetuvua nguo kama Taifa. Aibu hii

Mvua imetuvua nguo kama Taifa. Aibu hii

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Mvua imenyesha na hakika ardhi imepokea maji hadi imetota.

Wakazi wa mijini tumeshuhudia adha kubwa inayotokana na ubovu wa miundombinu ya kutiririsha maji.

MTWARA
Nyumba zaidi ya 17 zimezingirwa na maji (kwa mujibu wa taarifa ya habari ITV) na wananchi wanalalamikia ufunyu wa mitaro iliyojengwa kutiririsha maji ya mvua

DAR
Ni mafuriko kila kona.
Wakazi wa Mwananyamala wanalalamikia mwekezaji kufunga njia za maji na kusababisha maji kuelekea makazi yao

Maeneo ya Kisiwani wananchi watalala nje siku kadhaa ili maji yapungue majumbani kwao

Picha inayofuata inaonesha eneo la mjini kati chuo cha biashara CBE likiwa ipo ndani ya maji. Na bado tulivyo na akili za usahaulifu watu watapanga foleni kuipigia kura CCM.
FohDy3GWcAAQCko.jpeg.jpg


Hali ya kukosa mipango sahihi yenye tija kwa ncbi ni utamaduni uliosimikwa na serikali ya CCM ambapo wanapambana kushikilia dola kwa gharama yeyote ile huku wakifanya mambo ya hovyo kwenye kuisimamia serikali.

Pale eneo la soko la samaki ferry ambapo ni hatua chache kuelekea baharini, mvua ikinyesha hata ya dakika tano inajaza maji ambayo yanakosa muelekeo na kutuama barabarani ambapo ujenzi wa barabara na kituo cha mwendokasi havikuzingatia matoleo ya maji kuelekea baharini. kumbuka hapo ndipo ilipo Ikulu yetu. Aibu hii inatufanya tuonekane kituko duniani.

Mkuu wa Mkoa yupo bize kupambana na wamachinga badala ya kusimamia tija ya miradi ya serikali mkoani kwake.

Bungeni ni drama za kupmbea kura 2025 zinaendelea wskijifanya wana uchungu na nchi huku wakijua wazo kwsmba hatima yao ipo mikononi mwa kamafi za chama na siyo wananchi.

Tufike mahala tuwaache wateuane na watenguane lakini wakija kwetu tuwachuje na kuwakataa kuanzia Rais hadi mwenyekiti wa kitongoji
 
Tanzania hatuamini katika ukarabati. Ila Cha ajabu, ukifika muda wa uchaguzi, kuna kada wa ccm atakuja kuitumia hiyo kama hoja, ili apate kura.
NI makada kizazi cha 1970 hadi 1999 ndo wsnaohofia kuwapa kura upinzani wakiaminishwa wataleta vita.

Kitafutika kizazi hiko na CCM itategemea mitutu bila polisi
 
Wenye pesa wamejenga kwenye njia za maji kupita
 
Mvua imenyesha na hakika ardhi imepokea maji hadi imetota.

Wakazi wa mijini tumeshuhudia adha kubwa inayotokana na ubovu wa miundombinu ya kutiririsha maji...
Wayanyonye maji wakajaze mabwawa ya umeme! Tz inabidi tujipange kwa kweli, ukame unatutesa, mvua inatutesa, hujaweka magonjwa na ajali. Ni jambo gani tunaweza kulidhibiti?
 
Drainage systems zihimarishwe, hakuna aibu, after all Dar es Salaam is generally a swamp
Je akili hizi wanazipata baada ya mvua kuanza kunyesha au walipaswa kuzingatia drainage system during planning?

Je, hapo awali, mvua zikinyesha maji yalikuwa yanakwenda wapi?

Kwa sababu kadiri wanavyoongeza miundombinu bora ndivyo hali ya utiririshajj maji inakuwa shida.

Pale Jangwani. Ile barabara na daraja la Kajima waliwezaji kudhibiti mto msimbazi usisambaze maji na ukichukulia godown la Kajima lilikuwa pembezoni mwa mto? Leo tunatumia hela nyingi kutoa mchanga na tope mtoni mwaka mzima na bado mvua zikija zinatuzidi akili.

Tatizo ni wizi, ubadhirifu na hao TANROADS wanaangalia wanapata nini na siyo kinajengwa kiwango gani
 
Wayanyonye maji wakajaze mabwawa ya umeme! Tz inabidi tujipange kwa kweli, ukame unatutesa, mvua inatutesa, hujaweka maginhea na ajali. Ni jambo gani tunaweza kulidhibiti?
Tunachoweza kudhibiti ni maandamano pekee.

Vingibe ni hekaya za Abunuwssi
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Mvua imenyesha na hakika ardhi imepokea maji hadi imetota.

Wakazi wa mijini tumeshuhudia adha kubwa inayotokana na ubovu wa miundombinu ya kutiririsha maji...
Inakuwaje posta barabara ya Bibi titi iwe kama bwawa ? Watangaze tenda ya kufuga samaki wa vizimba na mimi ntaomba nifugie hapo CBE
 
Uongozi wa Nchi hii chini ya CCM ni tatizo kwa kweli
Na badala ya kushughulikia matatizo ya wsnanchi wapo bize kuwashughulikia na wwnaohoji na kukosoa.

Kuna mwalimu kule Mbeya anashikiliwa kwa kupiga picha za watoto wakikalia vumbi na matofali kwenye shule ambazo zinaelezwa hazina uhaba wa madawati kutokana na pesa za UVIKO

Shida sana
 
Back
Top Bottom