Mvulana huyu kashangaza wengi siku ya jana kisa...

Mvulana huyu kashangaza wengi siku ya jana kisa...

Pamoja sana wanajf.

Jana 21/10/2018 maeneo ya wilaya ya Ilemela - Mwanza, kuna mvulana au niseme dogo mmoja hivi alishangaza wengi, na hata wengine kuishia kucheka (nikiwemo Nahuja mie).

Tulikuta foleni kubwa ya magari eneo ambalo hata siku moja halina historia ya msongamano wa magari. Watu wakawa wanajiuliza kuna nini, wengine wakaenda mbali zaidi na kuhisi labda kuna ajali.

Baada ya kushuka kwenye magari tuone kuna nini huko mbele kinachosababisha foleni ndefu, oooooops! tukamshuhudia dogo anagalagala katikati ya barabara hali ambayo imefanya magari yashindwe kuendelea na safari.

Wengine wakasikika wakisema, "amekuwa kichaa". Lakini cha ajabu kukawa na vijana wengine pembeni mwa barabara ambao ni rika moja na yule aliyekuwa anagalagala barabarani walikuwa wanacheka sana,hadi machozi na makamasi yanawatoka.

Tukawauliza, vipi huyu wenzenu amekuwaje? wakatujibu kuwa, "ALIBET NA AMESHINDA KIASI CHA TSHS.1,850,000/=" Kijana mwingine akaongezea "JAMAA ALIBET MKEKA MKUBWA"...

Mfyuuuuuuu, watu tukafoka foka hapo, basi akanyanyuliwa wakamuweka pembeni mwa barabara magari yakaendelea na safari.

Maskini mtoto angeweza kugongwa hata na gari million moja ikamgharimu maisha yake ambayo yana thamani kuzidi kiasi cha pesa zote zilizopo hapa duniani! Munaona sasa maisha yetu yalivyo magumu halafu watu wamejitoa muhanga kutuondoa kwenye hali kama hii halafu wanatokea watu wa kuwa wanawakwamisha! Mimi kwa kweli mtu yeyote anayefanya tofauti na matakwa ya viongozi wa nchi hii haitatokea siku hata moja huko mbele nikaja kumwelewa. Kwenye zama zile za ubinafsishaji, angalau nasi tulitakiwa sasa tumfanye angalau hata Mzee Mengi kumkaribia Dangote!te!
 
Kwani kupata mil 1.8 lazima uweke timu nyingi?

Kama alibeti ngumu kumeza?

Umejuaje kama mkeka ulikuwa mkubwa?

Unaweza kujifanya unajua kumbe haujui, anayejua ni mshindaji tu.
Upo sahihi kabisa

ila nimezingatia maelezo ya mleta taarifa juu ya huyo mvulana


kama aliweka ngumu kumeza basi narudi pale pale kwenye kiasi cha pesa alichoweka hakizidi 2000/=


Hata kama ni ngumu kumeza odds ya kila game tuseme ni 2.00+ basi game hazipungui 8 kwenda juu
 
Maskini mtoto angeweza kugongwa hata na gari million moja ikamgharimu maisha yake ambayo yana thamani kuzidi kiasi cha pesa zote zilizopo hapa duniani! Munaona sasa maisha yetu yalivyo magumu halafu watu wamejitoa muhanga kutuondoa kwenye hali kama hii halafu wanatokea watu wa kuwa wanawakwamisha! Mimi kwa kweli mtu yeyote anayefanya tofauti na matakwa ya viongozi wa nchi hii haitatokea siku hata moja huko mbele nikaja kumwelewa. Kwenye zama zile za ubinafsishaji, angalau nasi tulitakiwa sasa tumfanye angalau hata Mzee Mengi kumkaribia Dangote!te!
Umeongea maneno yenye ujumbe mzito sana mkuu. Ahsante sana
 
Upo sahihi kabisa

ila nimezingatia maelezo ya mleta taarifa juu ya huyo mvulana


kama aliweka ngumu kumeza basi narudi pale pale kwenye kiasi cha pesa alichoweka hakizidi 2000/=


Hata kama ni ngumu kumeza odds ya kila game tuseme ni 2.00+ basi game hazipungui 8 kwenda juu

Mara nyingi haswa ngumu oddz za kushiba 26.00,33.....
 
Back
Top Bottom