Mwabukusi: Waziri hana Mamlaka ya kufuta Kijiji na asili ya Watu wa Ngorongoro

Mwabukusi: Waziri hana Mamlaka ya kufuta Kijiji na asili ya Watu wa Ngorongoro

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi

Mwabukusi amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamta wabakaji na kuwafikisha Mahakamani. Amesema kuwafikisha mahaksmani ni hatua ya kwanza, ametaka Polisi imfikishe Mahakamani aliyewatuma pia. Pia amewata Polisi kumuachia na kumuweka wazi mwanamke alipata madhira ili haki yake ipatikane ikiwrmo kupewa msaada wa kisheria..

Stsy tuned

=====

20 Agosti, 2024

TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU WITO WA WANANCHI WA NGORONGORO NA MAENEO MENGINE KUTAKA KUHESHIMIWA KWA HAKI ZAO

Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii kwa njia ya video iliyosambaa kwenye mitandao hiyo ikionyesha maandamano yaliyofanywa mnamo tarehe 18 mwezi Agosti, 2024 na mamia ya Wananchi wa Ngorongoro wakidai kuheshimiwa kwa haki zao. Katika maandamano yao miongoni mwa mambo mengine, Wananchi hao wamesikika wakilalamikia kuondolewa kwenye maeneo yao kinyume na utaratibu bila wao kuridhia pamoja na kuondolewa kwa huduma zote za kijamii kama vile shule, huduma za afya pamoja na maji. Kutokuwepo kwa huduma hizi muhimu kumepelekea Wananchi hao kuendelea kuishi katika mazingira magumu.

Tamko la Umoja wa Mataifa Juu ya Haki za Watu wa Asili la Mwaka 2007 limeeleza wazi katika ibara ya 10 kwamba watu wa asili hawataondolewa kwa nguvu kutoka kwenye ardhi au maeneo yao, uhamisho wowote wa watu wa asili hauwezi kufanyika bila idhini yao huru

Kwa mujibu wa ibara ya 24 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, kila mtu anayo haki ya kumiliki mali na haki ya hifadhi ya mali yake aliyonayo. Haki ya kumiliki mali ni moja ya haki ya msingi ya binadamu. Ibara 24 (2) imeeleza wazi kwamba mtu yoyote hatonyang’anywa mali yake isipokuwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria ikiwepo ulipwaji wa fidia stahiki.

TLS inatoa rai kwa Serikali kuonyesha nia yake ya dhati kwa kurudisha huduma zote za kijamii kwa Wanachi wa Ngorongoro kwa kuwa ni haki yao. Pia, vituo vya kujiandikisha kwa ajili ya kupigia kura ambavyo Wanachi wa Ngorongoro wanalalamika kwamba havipo katika maeneo yao virudishwe ili wapate kuitumia haki yao ya kikatiba ya kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa uliopangwa kufanyika mwezi Novemba mwaka 2024 pamoja na Uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka 2025.

Baraza la Uongozi la TLS limeona jambo hili la Ngorongoro na maeneo mengine linahitaji ufuatiliaji wa kina zaidi na kwa sababu hiyo, Baraza limeamua kuunda kamati maalum itakayofuatilia jambo hili kwa ukaribu ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na Idara, Wizara na vyombo vyote vinavohusika na suala la Ngorongoro ili kujua ukweli zaidi na kuhakikisha misingi ya sheria za nchi yetu inafuatwa.

Kamati iliyoundwa inajumuisha wajumbe wafuatao:

*Dr. Rugemeleza Nshala
*Tike Mwambipile
*Bumi Mwaisaka
*Laetitia Petro Ntagazwa na
*Paul Kisabo.

Miongoni mwa mambo mengine kamati itafanya mambo yafuatayo:

*Kufanya mashauriano na taasisi mbalimbali pamoja na kutembelea baadhi ya maeneo yenye migogoro ili kujua uhalisia wa migogoro husika.

*Kufanya Mapitio ya Sera ,Sheria na Mazoea pamoja na kuzichambua kuhusiana na umiliki wa Ardhi kwa Wazawa pamoja na shughuli za uwekezaji na Uhifadhi na kubaini uzingativu wa Haki za Msingi za Raia katika maeneo husika kwa kuzingatia Katiba, Sera na Sheria za Nchi.

*Kuandaa kongamano (Symposium) la Kitaifa kuhusiana na namna bora ya kufanya maendeleo kwa kuzingatia na kulinda haki za Wazawa katika Ardhi zao za Asili pamoja na haki zao za Kijamii, Kiuchumi na Kiutamaduni katika maeneo yanayofikiwa na shughuli za uwekezaji.

*Kubaini mashauri au hatua zote ambazo zimechukuliwa na walalamikaji pamoja na walalamikiwa kisheria na kiutaratibu katika kuhakikisha uzingativu wa sheria na kubaini majina ya watu ambao kweli wameridhia kuondoka kwa hiyari kwenye maeneo yao na ambao hawakuridhia kuondoka kwa hiyari kwa sababu ya wao kuamua kubaki katika eneo lao la asili Ngorongoro.

*Kubaini na kulishauri Baraza la Uongozi la Chama Cha Mawakili wa Tanganyika juu ya hatua zakuchua ili kupata ufumbuzi wa kudumu kuhusu swala la migogoro ya Ardhi inayosababishwa na mipango ya uwekezaji au uhifadhi.

Kamati inatarajiwa kumaliza kazi tajwa ndani ya muda wa kipindi cha siku 30.

TLS inawaomba Wanachama, Wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa Sheria kutoa ushirikiano kwa Kamati maalum iliyoundwa ili TLS kwa mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act Cap. 307) iweze kutimiza wajibu wake wa kuishauri Serikali na Kulinda haki za Wananchi kwa lengo la kupata suluhisho la kudumu.

Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)

Boniface A.K Mwabukusi

Rais
 
Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi
Naam kumekucha kweli
 
Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi
Samia amedhamiria kuikabidhi Tanganyika yote kwa wajomba zake waarabu
 
Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) Boniface Mwabukusi, amesema Waziri hana Mamlaka ya Kufuta Vijiji vya Ngorongoro

Ameyasema hayo leo 20/08/2024 Mkoani Dar Es Salaam alipokuwa anaongea na Waandishi wa habari. Amesema kama TLS wanaaangalia cha kufanya. "Wale wananchi wa Ngorongoro hawapaswi kupuuzwa, Warudishiwe huduma Muhimu pia Warudishiwe vituo cha kupigia Kura. Ni lazima tujue chanzo cha Tatizo Ngorongoro ni nini?". Amesema Mwabukusi

Mwabukusi amelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwakamta wabakaji na kuwafikisha Mahakamani. Amesema kuwafikisha mahaksmani ni hatua ya kwanza, ametaka Polisi imfikishe Mahakamani aliyewatuma pia. Pia amewata Polisi kumuachia na kumuweka wazi mwanamke alipata madhira ili haki yake ipatikane ikiwrmo kupewa msaada wa kisheria..

Stsy tuned
Sasa ndo TLS imempata Rais siyo wale wapigaji akina Hosea, Fatma Karume
 
Tuna bahati Mwabukusi kukalia ofisi ile
Haiwezekani Watanzania wawe wakimbizi katika nchi yao wenyewe.
Wamasai wana haki ya kuishi ngorongoro, kujaribu kuwafukuza ni kukaribisha hatari ya violent resistance
KUENDELEA KUKAA NA KUHARIBU UHAI WA HIFADHI HAIKUBALIKI,WAMASAI WALIO WENGI WAMEONDOKA KWA HIYARI YAO NA KWENDA MSOMERA,SASA HAO MNAOWAPIGIA KIFUA WAENDELEE KUBAKIA HAPO NI WA KUWAINGIZA KWENYE SHIDA TUH.
 
KUENDELEA KUKAA NA KUHARIBU UHAI WA HIFADHI HAIKUBALIKI,WAMASAI WALIO WENGI WAMEONDOKA KWA HIYARI YAO NA KWENDA MSOMERA,SASA HAO MNAOWAPIGIA KIFUA WAENDELEE KUBAKIA HAPO NI WA KUWAINGIZA KWENYE SHIDA TUH.
Unanikumbusha staili ya waisrael kuwahangaisha hangaisha wapalestina kila kukicha huko Ghaza. Leo utasikia hamienini Khani Yunis, kesho utasikia ondokeni Khani Yunis rudini Rafah, keshokutwa wanaambiwa ondokeni Rafah mrudi Khani Yunis.

Mbona waliojenga mahoteli huko ngorongoro hawaambiwi wakayejenge Msomera?
 
Kwani wewe unajiona timamu!
NDIYO MTULIE SASA,MMEPIGA KELELE WEEEE,MARA BANDARI IMEUZWAA BANDARI IMEUZWA,IMEUZWA WAPI BANDARI??

NA MKAENDA HADI KUSHITAKI VATICAN ETI NCHI INAUZWA KWA WAARABU,SASA HAT MKISEMA VATICAN ITASIAIDIA NINI,VATICAN WANA HELA??HELA ZENYEWE WANATEGEMEA HADI WAUZE MISALBA,SASA ALIEKUAMBIA MISALABA NI DEAL NANI??

ACHENI CHOKO CHOKO MLETEWE MAENDELEO,NA MKILETA FUJO MNAKULA VIBAO VYA USO TUH.
 
Unanikumbusha staili ya waisrael kuwahangaisha hangaisha wapalestina kila kukicha huko Ghaza. Leo utasikia hamienini Khani Yunis, kesho utasikia ondokeni Khani Yunis rudini Rafah, keshokutwa wanaambiwa ondokeni Rafah mrudi Khani Yunis.

Mbona waliojenga mahoteli huko ngorongoro hawaambiwi wakayejenge Msomera?
MAHOTELI YANAHARIBU VIPI MAZINGIRA??HAO WAFUGAJI WAMEKUWA WENGI NA MIFUGO YAO KILA SIKU INAZIDI KUKUA,MALISHO YA MIFUGO YAO NI HAPO HAPO MBUGANI,SHUGHULI ZAO ZA KIBINADAMU KAMA KUKATA KUNI,MITI NA KUCHOMA MOTO MISITU NI HAPO HAPO MBUGANI,SASA UNATAKA WAACHWE HAPO HADI LINI??NA SISI TUNATEGEMEA SERENGETI NA NGORO NGORO KUTUINGIZIA FEDHA ZA KIGENI KWA UTALII??

KWANINI LAKINI CHADEMA HAMTUMII AKILI MAFALA NYINYI??
 
MBONA MAGUFULI ALIIKABIDHI VATICAN KWA BABU ZENU NA SISI HATUKUSEMA KITU??
Ukijadili kila kitu kwa mrengo wa kidini unakuwa mpumba na juha kabisa.

Samia ni kweli ana wajomba zake kama ilivyo kwa Wazanzibar wengi walivyo na mafungamano na Oman.

Labda kama hujui Zanzibar ilikuwa ni sehemu ya Oman na makazi ya Sultan kama unavyoona Comoro ya Mayotte ni wilaya ya Ufaransa.

Wewe hata ujipendekeze vipi kwa Waarabu wewe siyo Mwarabu ni Mmakonde tu.
 
Mtu mmoja tunampa mzigo wa kupigania haki ya Watanzania wote. Atachoka haraka. Watanzania hatubebeki, wala hatuna uchungu wa Rasilimali tulizopewa bure na Mungu. Hakukosea kuweka vyote hapa.

Tuvilinde, hawa wanasiasa ni wa kupita anajineemesha yeye na watu wake. Baada ya miaka 10 hayupo madarakani but Tz bado ipo. Je ni sawa kila sehemu iuzwe au kuingia mikataba na hatuoni faida ya hizo hela?

Bado tunakopa na walipaji nisisi. Hatuhoji chochote, ni ili mradi kunakucha. Wao wanatumia huo udhaifu wa kufanya watakalo hakuna wa kuwauliza wala kuwazuia. Watanzania hebu tuamke huo usingizi wa pono jamani.
 
MwanaCCM kwa jina Kijana Mzalendo akasirishwa na vitendo vya chama dola kongwe kufanya mambo kinyume na ilani yake ya uchaguzi, katiba ya chama na pia kinyume na katiba ya nchi. Huku akirejea ilani ya uchaguzi wa CCM, katiba ya chama cha CCM na katiba ya nchi anajiuliza serikali ya CCM imetoa wapi mamlaka ya kufukuza watu Ngorongoro ...


View: https://m.youtube.com/watch?v=SROilRA8SdQ
 
Mtu mmoja tunampa mzigo wa kupigania haki ya Watanzania wote. Atachoka haraka. Watanzania hatubebeki, wala hatuna uchungu wa Rasilimali tulizopewa bure na Mungu. Hakukosea kuweka vyote hapa.

Tuvilinde, hawa wanasiasa ni wa kupita anajineemesha yeye na watu wake. Baada ya miaka 10 hayupo madarakani but Tz bado ipo. Je ni sawa kila sehemu iuzwe au kuingia mikataba na hatuoni faida ya hizo hela?

Bado tunakopa na walipaji nisisi. Hatuhoji chochote, ni ili mradi kunakucha. Wao wanatumia huo udhaifu wa kufanya watakalo hakuna wa kuwauliza wala kuwazuia. Watanzania hebu tuamke huo usingizi wa pono jamani.
Ni ngumu sana kuwabeba watanzania, wanaotegemea kuwa mtu mmoja ndio atawaletea mabadiliko halaf wao wanakuwa busy na umbea, uchawa, uzinzi… huyo mtu mmoja akianguka wanambebesha lawama
 
Back
Top Bottom