Mwajiri anapokataa kukuthibitisha kazini bila sababu ya msingi nini kifanyike?

Mwajiriwa ana haki ya kuthibitishwa kazin baada ya miezi 12 lakin si lazima. Mwajir anaweza kumuongezea muda wa matazamio ambao kisheria NI miez 6.

Unapaswa kusubir ipite hiyo miezi 6 ambapo ni lazima mtapewa barua za kuthibitishwa au kusitishwa mkataba.
 
Je, muajiri anapokataa kukuthibitisha baada ya miezi 12 kupita, si inapaswa akupe taarifa kwa maandishi kuwa ni sababu ipi imefanya asikuthibitishe kazini?
 
kwa mujibu wa sheria ,muda wa majaribio au probation inapaswa isizidi kipindi cha miezi 12 na baada ya hapo itabidi mwajiri andike barua ya kukuthibitisha kazini au kukuruhusu kuondoka ,japo katika taasisi za serikali mara nyingi barua ya kuthibitishwa inaweza toka hata baada ya 1mwaka.
 
Asante mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…