Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya Sekondari ya Serikali. Waliobahatika walijulikana kata nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

Infantry Soldier

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2012
Posts
15,892
Reaction score
16,476
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wote wa hapa JamiiForums.

Ndugu zangu watanzania;

Mwaka 1999 kurudi nyuma ilikuwa ngumu sana kuchaguliwa shule ya secondary ya serikali. Wachache waliobahatika walijulikana kata/tarafa nzima. Je, wewe ni mmoja wao?

TABORA BOYS SECONDARY SCHOOL
images (10).jpg


Juzi kuna mtoto wa jirani yangu alinifuata akaniambia brother ninaomba uniangalizie matokeo yangu ya darasa la saba. Mimi bila hiyana na smartphone yangu hii nikaingia katika website ya necta nikamuangalizia fresh tu. Dogo bwana alipata C flat masomo yoooote.

Nikajua ndio basi tena. Baada ya selection ya shule kutoka nikasikia huyu dogo amepangiwa shule moja ya kata mwendo kama wa dakika 20 kutoka hapa tunapokaa, ndio nikajisemea kimoyomoyo hakika dunia imebadilika kwa kasi sana.

Yaaani mtu anapata C flat bado anaenda secondary? Ninakumbuka dada yangu aliyeniachia ziwa, sasa hivi ni engineer, yeye ni moja kati ya wanafunzi 4 waliofaulu kwenda secondary shule ya serikali. Kumbuka enzi hizo kuchaguliwa tulikuwa tunaita kufaulu.

Yaaani wewe ukichaguliwa unaonekana umefaulu na wale ambao hawakuchaguliwa wanaonekana wamefeli ingawa kiuhalisia hawakuwa wamefeli ila shule zilikuwa ni chache mnoooo kiasi kwamba ni ngumu ku-accomodate wanafunzi wooote waliofaulu.

images (11).jpg


Dada yangu alifaulu wakati huo baba anafanya kazi Wilaya ya ******* Mkoa wa Mbeya. Watu walifurahi familia nzima, lilipikwa pilau kana kwamba kuna sherehe ya kipaimara. Ndugu waliokuwa wanaishi karibu walikuja kumpa pongezi dada utadhani labda amejifungua mtoto.

Dada alikuwa maarufu sana kwa maana akiwa anaenda shuleni basi ni yeye tu ndiye aliyekua anaonekana asubuhi amevaa sare wakati huo wenzake aliomaliza nao darasa la saba bado wamelala au wameenda shambani.

Mgeni aliyekuwa hapafahamu nyumbani akiwa anaulizia kwa mama fulani wenyeji wanaanza kudadisi kwa kuambiana "au yule mama mjaluo ambaye mwanae anasoma secondary". Kwenda secodary ya serikali ilikuwa ni umaarufu kama dereva kwa maana enzi zile hakuna gari ya automatic transmission.

Gari zote ni manual na anayeweza kuendesha ni mzee mmoja au wawili tu mtaa mzima. Wanafunzi wa secondary walikuwa maarufu kama madereva kutokana na uchache wao.

images (12).jpg


Matokeo yalikuwa yanasubiriwa kwa hamu na shauku kubwa sana kwa maana matokeo na selection zilikuwa zinakuja kwa pamoja tofauti na sasa hivi ambapo matokeo yanaanza kutoka na mwanafunzi au mzazi wake anaingia katika internet kisha baada ya mwezi mmoja mbele ndio selection inatangazwa.

Je, wewe ni mmoja ya wanafunzi wachache waliobahatika miaka ya 1990?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi. Je, hii ina ukweli wowote ndani yake?
Ni kweli ....kwa zamani shule za private secondary zilikua za wale ambao hawakufaulu sana kwenda shule za serikali
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi. Je, hii ina ukweli wowote ndani yake?
enzi zetu ukienda private wewe ni failure. shule private zilikuwa kwa ajili ya waliofail.
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi. Je, hii ina ukweli wowote ndani yake?
Mimi nilpomaliza shule mwaka huo shule nzima walifaulu watatu tu.
Basi wengine wetu wazazi waliokua na kauwezo kidogo wakatupeleka shule za private.
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
Ina ukweli

Shule kama 'special schools' za Serikali ndio zilikuwa zinatamba kabla ya ujio wa shule kama Feza, Marian, Kemebos nk

enzi hizo kwenda Ilboru ama Mzumbe ni lazima uwe 'cream' na zingine nyingi tu
 
Ukweli ni kuwa hapo zamani watu wengi wamekosa nafasi ya kusoma secondary school sio kwa sababu ya kutofaulu bali sababu ya uchache wa shule za sekondari.

Unakuta wilaya nzima kuna shule moja ya sekondari halafu shule za msingi zaidi ya120.Ilikuwa jambo la kawaida kukuta shule yote haijatoa hata mwanafunzi mmoja wa kujiunga kidato cha kwanza.

Kwa kweli aliyeleta shule za kata alifanya jambo la maana sana pamoja na changamoto zake. Kujivunia ule uzamani ambao uliwanyima wenzetu nafasi za kusoma na sababu kubwa ikiwa ni ukosefu wa shule za sekondari unakuwa sio uzalendo
 
Ukweli ni kuwa hapo zamani watu wengi wamekosa nafasi ya kusoma sio kwa sababu ya kutofaulu bali sababu ya uchache wa shule za sekondari.
Ukisoma vizuri bandiko langu kuu, hiki ndicho nilichokisema. Wengi sana walifaulu lakini wachache walichaguliwa kwenda secondary na walikuwa maarufu kijiji/kata nzima.
 
Nilianzia kuruka kichura kwenye hiyo round about hadi bwenini, ni mwendo wa viwanja viwili vya mpira wa miguu,begi na jembe nimejitwisha kichwani.

Nilivyo fika getini akanisamehe, akanirudisha tena nilipoanzia kuruka kichura kwa lengo la kujitambulisha.
Kweli maisha ni hatua.

IMG_20201228_190942.jpg
 
WAHENGA TU: Kuna mzee mmoja alisoma secondary miaka ya 1970s. Yeye binafsi aliwahi kuniambia kwamba enzi hizo waliokuwa wanasoma shule za secondary za serikali walikuwa wanaheshimika sana ukilinganisha na wale waliokuwa wanasoma shule za secondary za binafsi tofauti na hivi sasa ambapo wanafunzi wa private ndio wanaheshimika.

Je, kauli hii ina ukweli wowote ndani yake?
KABISA.
 
Nilianzia kuruka kichura kwenye hiyo round about hadi bwenini, ni mwendo wa viwanja viwili vya mpira wa miguu,begi na jembe nimejitwisha kichwani.
Nilivyo fika getini akanisamehe, akanirudisha tena nilipoanzia kuruka kichura kwa lengo la kujitambulisha.
Kweli maisha ni hatua... View attachment 1661688

Lugalo Secondary, mwaka gani hiyo boss?
 
Pamoja na ukweli kwamba zamani shule za private zilionekana kuwa ni za wale vilaza, lakini kuna kundi la hizo shule za private zilikuwa zinaheshimika sana; namaanisha SEMINARY. Hizi kitu zilinifanya nikaitosa Mazengo (kwa sasa St John University) nikaenda kukipiga kwa wazee wa kazi na sala.
 
Mkuu hii ishu iliishia 2004 kurudi nyuma

Kuanzia 2005 alipoingia Kikwete ni mwendo wa shule za kata hata Kama ulikuwa unapasua

Nakumbuka nilipomaliza darasa la Saba shule yetu tulikuwa 232

Ila tuliochaguliwa(kufaulu) tulikuwa 14 tu wavulana Tisa na wasichana 5

Aisee tulikuwa tunaonekana watabe sana na alwatan sana kitaa [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom