Zanzibar 2020 Mwaka 2015, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo, mwaka huu wa 2020 watakuja na mbinu gani?

Zanzibar 2020 Mwaka 2015, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo, mwaka huu wa 2020 watakuja na mbinu gani?

Kwa Sjingo upande Maalim atatangazwa lakini Serikali yake haitaachiwa kufanya yale ambayo itataka kufanya hususani yaliyo kwenye muungano.
Unajua hata waingereza walikuwa wakifikiria hivyo hivyo kama Nyerere akiwa kiongozi hawatamuachia afanye mambo fulani fulani hivi. Pia na Mandela makaburu walifikiria hivyo. Ni akili za kikoloni tuu hizo, inafurahisha kuona Tanganyika iliokuwa ikijinata kupigania uhuru barani Afrika sasa imekuwa mkoloni na raia wake wengi wakifurahia. Tukumbushe mkuki kwa nguruwe!

Zanzibar ni nchi ina uhuru wa kujiamulia itakavyo, hakuna ukomo. Muungano sio wa kitakatifu lazima uwe na maslahi ya kiuchumi na wazanzibari. Narudia hoja kuu ni uchumi, kuna kila dalili tena za wazi kama uchumi wa Zanzibar umefifia au kufa kutokana na wakoloni wetu kutofahamu tofauti ya uchumi wa Zanzibar na ule wa Tanganyika. Hili tatizo linaenda deep hadi kwenye utungaji wa sera/economic-policies.

Mpelekeeni salamu huyo Dr.Mwinyi, nasikia anasema ameishi maisha ya kawaida kama wazanzibari wengine. Labda nimdokeze tuu, sie wengine hatuoni kama ni kawaida kila baada ya kilomita chache kupita road-blocks! Way far from what we consider it a normal life!
 
Wadau, hili ndio swali tunalopaswa kujiuliza kwa kuzingatia yaliyotokea mwaka 2015 ambapo matokeo ya uchaguzi yalifutwa na Bwana Jecha ambae ndio alikuwa kiongozi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC)....
Siku zote ccm hushinda zanzibar, tatizo ni pale ambapo wananchi wanaaminishwa kuwa et maalimu huwa anashinda. Hata mwaka huu ccm itashinda lakini kutakuwa na kelele zile zile ambazo hazimzuu punda kunywa maji
 
Kuna yale mazingaombwe ya kumtoa Sungura kwenye kofia. Tunasubiri CCM wafanye hayo.

Kama ningekuwa Dr Mwinyi ningechukua makamu wa kwanza wa Rais ili nishirikiane na kina Maalim.

Znz inategemea zaidi utalii, kwa Corona hii Holiday nyingi hakuna mwaka huu hadi 2022. Sasa kama ni kweli anataka kuijenga Zanzibar basi lazima ashirikiane na wenzake waombe msaada, wakatafute wawekezaji, wajenge kituo cha kibiashara n.k
Unajua hata waingereza walikuwa wakifikiria hivyo hivyo kama Nyerere akiwa kiongozi hawatamuachia afanye mambo fulani fulani hivi. Pia na Mandela makaburu walifikiria hivyo.!
 
CCM wametuona watz vilaza naomba Lissu aoneshe mfano kuwa mstari wa mbele kwenda kuvamia ikulu endapo haki haitatendekeka, nchi hii sio Mali ya CCM tumechoka na utopolo wao.
lISSU HAPATI HATA IDADI YA KURA ALIZOPATA MBOWE MWAKA 2005.POLENI
 
Wasipomtangaza, wamejipanga kufanya nini au muda ndio utajua nini kifanyike?
Inabidi hukusikia mpango wao wa mara hii? mbona wameweka wazi, siku ya kwanza wanapiga kura watu flani (ndio siku ya mipango ya wizi) na siku ya pili ndio jumla jamala.
 
Wadau, hili ndio swali tunalopaswa kujiuliza kwa kuzingatia yaliyotokea mwaka 2015 ambapo matokeo ya uchaguzi yalifutwa na Bwana Jecha ambae ndio alikuwa kiongozi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Binafsi na ni imani yangu tuko wengi tunaoamini kuwa hata mwaka huu Maalim Seif atashinda uchaguzi huko Zanzibar kama dalili zinavyoonyesha.

Swali hapa ni je, safari hii atatangazwa mshindi iwapo atashinda?

Wasipomtangaza, wamejipanga kufanya nini au muda ndio utajua nini kifanyike?

Na wapinzani safari hii walivyopania, watakubali kutotangazwa washindi iwapo watakuwa na uhakika wameshinda huko Visiwani na hata huku Bara?

Pengine swali gumu kuliko yote ni je, Maalim Seif akiingia Ikulu ya Zanzibar, ataacha kuitisha kura ya maoni Wazanzibar waamue hatima ya Muungano?

Tuombe uzima kuona Taifa hili likirekodi historia mpya mwaka huu kuhusiana na maswala ya uchaguzi Bara na Visiwani.
Wamepania kumpa mtu ushindi kwenye sahani. Kwasababu ni mrithi wa babayake.
 
Silaha kubwa ya CCM ni utu wa watanzania. Wanajua watanzania wapo tayari kunyanyaswa kuliko kumwaga damu.
Wakenya wanatuita sisi kuku kwa kuogopa..

Sent from my SM-G935W8 using JamiiForums mobile app
 
Mwaka huu wamepanga kukata majina ya wagombea maafufu ,wanaohisi watawaangusha CCM ,Lissu ,Membe ,Maalim majina yatakatwa na tume hawana sifa kwa mujibu maelekezo kutoka juu kwa yesu wa CCM.
 
Mwaka huu wamepanga kukata majina ya wagombea maafufu ,wanaohisi watawaangusha CCM ,Lissu ,Membe ,Maalim majina yatakatwa na tume hawana sifa kwa mujibu maelekezo kutoka juu kwa yesu wa CCM.
Waache kuweka Mpira kwapani,wakiwa wanakubalika sana waingie uwanjani watuonyeshe kukubalika kwao.
Kukataliwa kubaya...
 
Back
Top Bottom