Mwaka huu kufuturisha kumetumika kisiasa kuliko kiimani; matajiri na wanasiasa wamejifanya ifta kama kongamano; tupate mwongozo next time

Mwaka huu kufuturisha kumetumika kisiasa kuliko kiimani; matajiri na wanasiasa wamejifanya ifta kama kongamano; tupate mwongozo next time

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Nimeona agenda ya kuftarisha imepamba Moto kila Kona huku majina ya viongozi yakitumika....kila kiongozi akiftarisha anamtaja mwenye nchi unajiuliza hizi fedha wametoa wapi? Je NI kweli wametumwa na wanayemtaja? Au uchawa unawasumbua Hadi kwenye Imani?

Lakini pia ifta ilipaswa iwe Kwa maskini na wale wasio na chakula au futari lakini unashangaa wote wanaoonekana kwenye TV wanajiweza na wameacha misosi kwao. Najiuliza hii inatafsiri gani kidini? Hakuna kiongozi aliyefuturisha ambaye tumemwona akiwa na maskini mitaani wote wanakula kwenye hekalu na kumbi Nono.

Mwisho najiuliza ni lazima ukiwalisha watu chakula uite vyombo vya habari? Wakuu WA wilaya na Mikoa pamoja na wabunge mmefanya siasa kwenye ibada ya mwaka huu; najiuliza mwakani kuelekea uchaguzi mtafanya vihoja gani mwezi mtukufu?

Kuna baadhi ya watu wamefanya mwezi mtukufu uonekane kama mwezi wakuonyesha nguvu ya kisiasa na kiuchumi kwenye kulisha matajiri........mlijisahau mkawaacha walengwa ambao ni wasio na vyakula......mmetumia muda mwingi kualikana Kwa hadhi zenu kwenye jamii.....siyo Jambo jema limewakera wengi
 
Sehemu nyingi imetumika kama sehemu ya kupiga hela. Kwenye taasisi za umma, wakuu wa mikoa na wilaya.

Bila shaka December pia tutashuhudia kadi nyingi za christmas na january kalenda za kutosha kutoka kwenye hizo taasisi.
 
Nimeona agenda ya kuftarisha imepamba Moto kila Kona huku majina ya viongozi yakitumika....kila kiongozi akiftarisha anamtaja mwenye nchi unajiuliza hizi fedha wametoa wapi? Je NI kweli wametumwa na wanayemtaja? Au uchawa unawasumbua Hadi kwenye Imani?

Lakini pia ifta ilipaswa iwe Kwa maskini na wale wasio na chakula au futari lakini unashangaa wote wanaoonekana kwenye TV wanajiweza na wameacha misosi kwao. Najiuliza hii inatafsiri gani kidini? Hakuna kiongozi aliyefuturisha ambaye tumemwona akiwa na maskini mitaani wote wanakula kwenye hekalu na kumbi Nono.

Mwisho najiuliza ni lazima ukiwalisha watu chakula uite vyombo vya habari? Wakuu WA wilaya na Mikoa pamoja na wabunge mmefanya siasa kwenye ibada ya mwaka huu; najiuliza mwakani kuelekea uchaguzi mtafanya vihoja gani mwezi mtukufu?

Kuna baadhi ya watu wamefanya mwezi mtukufu uonekane kama mwezi wakuonyesha nguvu ya kisiasa na kiuchumi kwenye kulisha matajiri........mlijisahau mkawaacha walengwa ambao ni wasio na vyakula......mmetumia muda mwingi kualikana Kwa hadhi zenu kwenye jamii.....siyo Jambo jema limewakera wengi
Huku kwenye futari ndiko ziko kura.
 
Huwezi kupata mwongozo mzee BAKWATA ni taasis ya serikali mufti wq Tanzania ni mtu aliyesoma elimu ya upande mmoja tyu. Dini. Unamkumbuka pr. Mtulya?
 
Kadri ya miaka inavyo kwenda ndivyo ujinga wa viongozi wa bara la kiza wanakuwa wajinga wa kiwango Cha SGR.

Ikulu imekuwa kama kijiwe Cha kahawa na alikasusu
 
Kwani wakati wao wanatafuta utajiri uliwasaidia? Mpk utake kuwapangia namna ya kutoa/ kutumia mijihela yao?
 
Back
Top Bottom