Mwakalebela aiomba msamaha na kuisifia TFF ya Karia, aiweka njia panda Yanga

Mwakalebela aiomba msamaha na kuisifia TFF ya Karia, aiweka njia panda Yanga

Lupweko

JF-Expert Member
Joined
Mar 26, 2009
Posts
23,566
Reaction score
24,891
Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, ndugu Fredrick Mwakalebela ambaye amefungiwa kutojihusisha na masuala ya soka nchini kwa kipindi cha miaka mitano pamoja na kutozwa faini ya sh. milioni saba, amekiri kufanya makosa na kuiomba radhi TFF kwa yale aliyotamka hadi yakapelekea kupewa adhabu hiyo.

Mwanamichezo huyo amekiri kwamba hata adabu aliyopewa ilizingatia kanuni, na kwamba kila kosa aliloadhibiwa lilitajwa sambamba na adhabu ya kikanuni inayohusika. Mwakalebela amezungumza hayo wakati akifanyiwa mahojiano na mwandishi maarufu wa habari za michezo nchini, Saleh Ally maarufu kama Saleh Jembe wa Global TV

Hatua hii ya Mwakalebela inaweza kutafsiriwa kama kuiweka njia panda klabu yake ya Yanga ambayo iliwahi kutoa taarifa kwa umma kuelezea dhamira yake ya kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya TFF kwani kwa kufanya hivyo, klabu itakuwa ikiwasilisha malalamiko kwa niaba ya mtuhumiwa ambaye ameshakiri kufanya makosa na kuomba radhi, tena akienda mbali zaidi kwa kuisifia TFF kwa hatua kubwa iliyopiga katika kuupaisha mpira wa miguu katika nchi yetu.


 
Jamaa anajua uchaguzi wa TFF ni mwezi wa nane anataka akajaribu bahati yake, ameshachungulia fursa.
 
inashangaza sana mwakalebela kuchelewa kugundua kwamba pale yanga kuna wenzake hawataki yeye na bumbuli waendelee na vyeo hivyo..walijifanya wanampigania huko Tff kumbe moyoni wanataka apotelee mbali hukooo
Walimchomekea na yeye akaingia kichwa kichwa bila kujua.
 
Akishalewa mataputapu huwa mropokaji sana
JamiiForums1571731236.jpg
 
Morrison katengeneza goli tusubiri kesho Mwakalebela atakuja na ile single yake ya CAS
FB_IMG_1612867223083.jpg
 
Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, ndugu Fredrick Mwakalebela ambaye amefungiwa kutojihusisha na masuala ya soka nchini kwa kipindi cha miaka mitano pamoja na kutozwa faini ya sh. milioni saba, amekiri kufanya makosa na kuiomba radhi TFF kwa yale aliyotamka hadi yakapelekea kupewa adhabu hiyo.

Mwanamichezo huyo amekiri kwamba hata adabu aliyopewa ilizingatia kanuni, na kwamba kila kosa aliloadhibiwa lilitajwa sambamba na adhabu ya kikanuni inayohusika. Mwakalebela amezungumza hayo wakati akifanyiwa mahojiano na mwandishi maarufu wa habari za michezo nchini, Saleh Ally maarufu kama Saleh Jembe wa Global TV

Hatua hii ya Mwakalebela inaweza kutafsiriwa kama kuiweka njia panda klabu yake ya Yanga ambayo iliwahi kutoa taarifa kwa umma kuelezea dhamira yake ya kukata rufaa dhidi ya maamuzi ya TFF kwani kwa kufanya hivyo, klabu itakuwa ikiwasilisha malalamiko kwa niaba ya mtuhumiwa ambaye ameshakiri kufanya makosa na kuomba radhi, tena akienda mbali zaidi kwa kuisifia TFF kwa hatua kubwa iliyopiga katika kuupaisha mpira wa miguu katika nchi yetu.



Kosa watakalofanya TFF ni kumsamehe, kesho wa simba nae ataropoka halafu ataomba msamaha
 
Back
Top Bottom