Mwakyembe: Marufuku kumuliza Azory Gwanda alipo. Mbona viongozi wa Serikali hamuwaulizii? Waliokashifiwa na gazeti la Tanzanite waende Mahakamani

Waziri ameshindwa kuunganisha kauli ya Rais alipolizungumzia swala la Mo, aliposema watanzania sio wajinga.Hivi Mo alivyopotea kihuni kama vile alitaka tukae kimya?Msomi wa sheria kama Mwakyembe kusema watu waache kuzungumzia swala la Azory nadhani ameteleza kwa maoni yangu.Leo kapotea Azory,Ben, Kangoye yule wa kigoma,Lisu kapigwa risasi mchana leo Msomi wa sheria anasema tukae kimya, kweli uongozi ni koti subiri ulivue halafu mwanao apotee ndipo utajua umuhimu wa sauti
 
Lakini Mwananchi,Mtanzania,Mwanahalisi,Tanzania daima,hayo yanafungiwa na kupewa onyo kali,bila kwenda mahakamani!!!

Lakini Tanzanite waandike wanavyopenda,anayeona hatendewi haki aende mahakamani!!!

Basi sawaaaaa!!!
Namimi swala la Tanzanite naunga mkono. Mtu kama hatendewi haki na gazeti flani kwanini haendi mahakaman?Badala yake naye anakuja mitandaoni kutoa shutuma zake. Haki inatolewa mahakaman sio kwenye page za social networks.
 
Namimi swala la Tanzanite naunga mkono. Mtu kama hatendewi haki na gazeti flani kwanini haendi mahakaman?Badala yake naye anakuja mitandaoni kutoa shutuma zake. Haki inatolewa mahakaman sio kwenye page za social networks.

Serikali inapofungia magazeti huwa inaenda mahakamani?
 
..mbona magazeti ambayo ni pro-wapinzani yakikosea SEREKALI inachukua hatua?

..wananchi wanataka SEREKALI ichukue hatua kwa Tanzanite kama ilivyofanya huko nyuma kwa mwanahalisi, na magazeti mengine.
Serikali haiwezi kudhibitisha kama hiyo habari ni ya kweli au la anayetakiwa kulalamika ni anaejua amechafuliwa na habari za uongo. Serikali inafungia magazeti ambayo yameichafua serikali kwasababu yenyewe ndiyo iliyochafuliwa si mtu.
Kila mtu anayechafuliwa aige mfano wa Membe
 
Sasa hivi MTU unatakiwa ujilinde mwenyewe ,ukiona mazingira huyaelew, usitegemee wana usalama ,binafs sina imani nao ,
 
Mbona magazeti mengine yanafungiwa na serikali hayafungiwi na mahakama ! Ama kweli wakiwa kule akili zinapungua ....
 
Namimi swala la Tanzanite naunga mkono. Mtu kama hatendewi haki na gazeti flani kwanini haendi mahakaman?Badala yake naye anakuja mitandaoni kutoa shutuma zake. Haki inatolewa mahakaman sio kwenye page za social networks.
Mbona magazeti mengine yanafungiwa na serikali hayafungiwi na mahakama ! Akili ndogo...
 
alitia huruma sana alivobabuliwa ngozi huyu bwana ila tumuachia Mungu maana nae utawala wake wa kyela ndio umefika mwisho
 
Huu ni ulevi na kiburi kisicho kipimo. Wanamuulizia Azori kwa sababu anajulikana na anawawakilisha wote waliopotea.
 
Ulevi wa madaraka ni ulevi mbaya sana.
Mwakyembe anaeleza kila kitu bila kujijua ana ueleza umma habari kamili

Dr haelewi kuwa maisha ya mwanadamu hayapimwi katika makundi
Hakuna thamani ya maisha ya mwanadamu kwa kuyapima na kitu kingine

Nchi za wenzetu mtu mmoja 'ni taifa'. Marekani ina watu milioni 300 lakini maisha ya Otto Wombia kule Korea yalikuwa na thamani ya kuliingiza taifa hata kwenye mgogoro

Madaraka yanaondoa utu. Hivi Dr anaweza kusema tuache kupambana na kipindu pindu kwasababu wanaokufa nacho ni wengi!

Azori angekuwa mtoto wa dada yake, kaka au mdogo wake Mwakyembe angeweza kusimama na kuwaambia wakae kimya kwasababu watu wanapotea

Mbona alitoa chozi kifo cha mkewe hakuwa na ujasiri wa kukakamaa kwavile watu wanakufa kwa maradhi kila siku.

Ulevi wa madaraka hasa ya kunyooshewa kidole ni mbaya sana.
Unaweza kukufanya uonekane mkatili, usie na utu na roho ya ajabu sana

Kwanini Watz tumegeuka kuwa kama wanyama siku hizi?

Pascal Mayalla JokaKuu
 
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka watu wanaokashifiwa na magazeti wakalalamike mahakamani kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.



Dkt. Mwakyembe ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Pia Waziri Mwakyembe amesisitiza umuhimu wa waandishi wa Habari kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ili kulinda tunu za Taifa.

Katika hatua nyingine amesema kwamba pamoja na kwamba watu wengi wanataka kujua alipo Mwandishi Gwanda lazima waelewe kwamba eneo alilopotelea mwandishi huyo walipotea watu wengi wakiwamo viongozi wa Serikali. Kutokana na hali hiyo Waziri huyo amesema watu wasiendelee kufuatilia mahali alipo mwandishi huyo kwa kuwa hilo ni suala dhaifu.
 
Phd holder amechanganyikiwa n madaraka mpaka amesahau thamani y uhai wa binadamu. Kumbuka wtt wake n mkewe n familia kwa ujumla wako kwenye majonzi makubwa kw kupotea bwana Ezory. Tunaamini mh bado unamajonzi makubwa ya mke , kumbuka n familia yEzory nayo inaumia km uumiavyo wewe.
 
Kwa sheria zipi? Za dikteta wa Ikulu?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…