Mwakyembe: Marufuku kumuliza Azory Gwanda alipo. Mbona viongozi wa Serikali hamuwaulizii? Waliokashifiwa na gazeti la Tanzanite waende Mahakamani

Mwakyembe: Marufuku kumuliza Azory Gwanda alipo. Mbona viongozi wa Serikali hamuwaulizii? Waliokashifiwa na gazeti la Tanzanite waende Mahakamani

Mbona wakitukanwa humu jukwaani huwa wanachukua hatua, au serikali huku jukwaani inaona tu ikitukanwa?
Umesema wakitutakanwa na hao unaowasema ni serikali. Je zito ni serikali?
 
Hao walio serikalini are they so special?
Mkuu serikali haiwajibiki kufuatilia swala la mtu mmoja mmoja bila ya muhusika kutoa taarifa. Ukiigusa serikali utachukukiwa hatua stahiki lkn sio serikali imuite mhariri kwanini umeandika Zito anatembea na mke wa marehem. Zito ni nani?Zito hana tofauti na wewe tindo au Misuli nk.Leo gazeti likiandika Tindo ni ana matatizo ya akili,sio jukum la serikali kulalamika. Tindo inatakiwa ukatoe taarifa kwenye mamlaka husika. Zito kaambiwa anatembea na mke wa marehem badala ya kushtaki anakimbilia tweeter au fb kutoa mikwara ya kuroga. Serikali ifanye nn?
 
Dr Mwakyembe ataka watu waache kuuliza alipo Azory Gwanda.

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amewashangaa watu wanaofuatilia mahali alipo mwandishi wa habari Azori Gwanda.

Dk Mwakyembe ameyasema hayo bungeni leo alipokuwa akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2019/20.

Amesema kwamba pamoja na kwamba watu wengi wanataka kujua alipo Gwanda lazima waelewe kwamba eneo alilopotelea mwandishi huyo walipotea watu wengi wakiwamo viongozi wa Serikali.

Kutokana na hali hiyo Waziri huyo amesema watu wasiendelee kufuatilia mahali alipo mwandishi huyo kwa kuwa hilo ni suala dhaifu.

Dk Mwakyembe aliyasema hayo bungeni leo alipokuwa alihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2018/20.

“ Pamoja na hayo Serikali itaendelea kudhibiti watu wanaokiuka utoaji wa maoni kwa kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka,”amesema Dk Mwakyembe.

Katika hatua nyingine Waziri huyo amewataka watu wanaokashifiwa na magazeti wakalalamike mahakamani kwa kuwa ndiko haki inakopatikana.

Source: Mtanzania Online
Katika watu wa hovyo,ni huyu jamaa,
Kwa majibu yake,anaweza kumkana hata mama yake mzazi,
Kwamba kwa vile ubakaji upo,mama yake akibakwa watu wasihoji kwa kuwa mbona wengi wanabakwa!
 
Karma is a bitch

Mwakyembe aangalie sana kauli zake, anafikiria familia ya Azory inajisikiaje unapokwamisha juhudi za kumpata mwenzao.
 
Eti mpaka leo watu 20 wametoa "Thanks" kwa alichokisema Mwakyembe. Hivi kasema point gani hapo. Ngoja ndugu yako apotee na uambiwe ufyate mkia, Jinsi utavyojisikia. Ma- CCM ndivyo Yalivyo.
 
Laiti angelikuwa ni ndugu yake ama mwanae sidhani kama angeliongea maneno haya,Ila maneno mtu unenayo ipo siku yatakugeukia mwenyewe
 
..mbona magazeti ambayo ni pro-wapinzani yakikosea SEREKALI inachukua hatua?

..wananchi wanataka SEREKALI ichukue hatua kwa Tanzanite kama ilivyofanya huko nyuma kwa mwanahalisi, na magazeti mengine.
Mkuki kwa nguruwe ...
 
kweli watu waache kuhoji maana ukisoma huu uzi utajua alipo kutokana na maneno ya mwakichungwa
 
Watanzania wanahofu zaidi na CCM kuliko hata hofu ya maisha na kifo!
 
Bwana Mwakyembe huyo Azron ana wazazi kama wewe huyo Azron and ndugu kama wewe nipende kukumbusha tuu hakun akitu inauma kama kumpoteza mwanao hujui yuko hai au ni mfu... Nikuambie tuu omba msamaha Azron Gwanda hakutoka kwenye mti ana familia ndugu na marafiki
Na aliacha mke mjamzito.
 
Back
Top Bottom