Mwalimu gani mkali ushawahi kukutana nae katika maisha yako ya shule...!!!??

Kitoksya(RIP) Meta sec. Nilikua pale 2003-2005
Hivi Kitokesya alikuja kuwa mwalimu Meta? Namkumbuka akiwa Iyunga enzi hizo, ila yeye ukali wake ulikuwa ni kwa Form One tu, sijui kwa nini mwalimu yule alikuwa hawapendi bazoka
 
Kuna kitu kilikuwa kinaitwa Mwakalindile... Ifunda Technical Secondary. Tulizowea kumwita Brigedia...

Kijana kijana unaletha mchedho, lala tchini....brigedia alikuwa hana utani.nakumbuka kithembe chake....by the way labda mkuu hukumkuta kuna mtu ifunda alikuwa mkuu wa taaluma.tulikuwa tunamwita mkono wa chuma.alikuwa na kengeza kabla hajakuchapa sura yake tu chozi linatoka.rip mrema!!
 
Nestory Kaimukilwa a.k.a Sura mbaya wa kitendaguro! we hacha tu! alikuwa Rwamishenye Primary school (Kashabo)!
 
Kuna kitu kilikuwa kinaitwa Mwakalindile... Ifunda Technical Secondary. Tulizowea kumwita Brigedia...

Mwaka gani?
Me nlikuwa pale enzi ya Kigava.


Sie ni wa enzi za akina Kaguo, Mbungi (Kiswele), Kocha, Luhwago (Kaka)
 
Na hapa ndipo Tanzania ilikuwa na elimu safi.... Enzi hizo ukimuona mwalimu mtaani kwenu unakula kona!
 

Mbugi?
 
Mwl. Ndossi wa Muhimbili primary, uwiii. Hivi yupo wapi huyu mzee?
 
Mwl miloso, onespholi a.k.a pokati na LL hatari sana hawa viumbe pale NYAKATO BOYS BUKOBA
 
dahh Kigava alikuwa noma ukijipindua kwenye anga zake. Ila akiwa class utadhani sio yeye vile, anakuwa mtu poa sana.

Yaani waweza amini alieko darasani ni fotokopi kwa upole.
 

mkuu mm shule ya msingi kuna jamaa alikua anaitwa Njilima dah! Afu pale kibaha sec nikakutana na Mr Luhaga(aka Abacha) miaka ile ya 1998-2001 . Huyu akikutangulia hatua moja kwenye pindi la kemia huzami mazee
 

Shule Ya Msingi ni Mwalimu Nyagabona na Marehemu Mwalimu Wangu wa Darasa La Kwanza Mama Nunduma hapo Nikiwa Oysterbay Primary School Wakati Secondary School Sitamsahau Mwalimu Thomas Kavuye ama TK na Hayati Mwalimu Maina hapo Nikiwa Shighatini Secondary School na Nilipokuwa Nchini Uganda Bugema Adventist Sitomsahau Mwalimu Wangu na Kocha Wangu Pia Wa Mpira Wakati Nikiwa Beki na Kiungo Maarufu wa Timu Ya Shule Ya Bugema Adventist Hayati Mwalimu Thomas Olinga na ktk Tuition Sitomsahau Mwalimu Aliyenipiga Bakora Lakini Alinifundisha Hesabu na Alinijenga Mno Kitaaluma Hayati Mwalimu Njowoka Tukiwa Tuition Pale Uhuru Mchanganyiko na Tukahamia Shule Ya Msingi Ilala Boma. Ila Nawashukuru Sana Walimu Wangu Wote Walionifundisha Japo Sitosahau Viboko au Bakora Zao!!!!!!!!!
 
kuna mwl marehem kwa sasa ,Kombaha......alikua kiboko
 
Mwalimu ZEREMURA - huyu alikuwa hatari kwa viboko , alikuwa na scooter yake - kwa wanaomkumbuka
 
Ticha laurent mwanga primary alikua anafundisha hisabati huyu alikua kiboko ukikosa swali moja kiboko kimoja yaan ilikua kila ikifika kipind chake darasa lote kimya....!ticha mkisi jitegemee sec
 
Nilipokuwa Tambaza alikuwepo H/M Karumuna(Father K), huyu mzee alikuwa noma.RIP
. Nilipokuwa Tosamaganga nilimkuta H/M anaitwa Dudu. Huyu alikuwa anakuchapa fimbo+constant (constant=,fimbo 6)
. Alikuwepo pia mwalimu Soldier. Huyu usiposafisha meza d/h halafu yupo zamu anasafisha yeye, sasa subiri muziki wake akikupata
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…