Mwalimu gani mkali ushawahi kukutana nae katika maisha yako ya shule...!!!??

Mwalimu gani mkali ushawahi kukutana nae katika maisha yako ya shule...!!!??

Kweli watu Jamiiforum wengi wametoka bushi
 
Mwl machumbe na mwl mtatiro,shule ya mcng majimoto huko serengeti,zam yao wanafunz tulikua tunafka shulen sa 11 alfajiri ili kuwah kuhesab namba,kumbuka kule miaka hyo n pori lkn bora uamke usiku uliwe na fisi lakin usichelewe namba,unapgwa style moja inaitwa shka masikio,stiki kama 30 hapo mgongon,mkuu ilikua heri kuliwa na fisi kuliko kuchelewa namba.
 
Mwl.jacob cheyo 'A' pr school, mwl.malekela(R.I.P) itigi pr school,mwl.maduhu na mwl.dijenyenye mazoezi mwenge . respect to them kwa mboko.
 
Nyakabungo primary school pale Mwanza alikuwepo mwl Aron, pamoja na jirani yake mwl Banana.

Walikuwa wakisimama maeneo ya parade ground hata kama ni break time watoto wote wanaingia mitini na kurudi madarasani tena bila kusikia kengele ya pili.
kaka mwl banana jina lake la kwanza nan?
 
Pale S/M SAMORA MJIMWEMA alikuwa mwalimu JEMBE,huyu jamaa alikuwa anatufundisha hisabati darasa la 6-7,ilikuwa ukimzingua tu anagonga hadi vichwa.

O/level kulikuwa na MOHAMED UTALY,jamaa alikuwa anafundisha COMMERCE.anauliza swali na anakuchagua ujibu hata kama hukunyoosha kidole,ukipata unagongwa bakora kwamba ulikuwa unajua halafu hunyooshi kidole,

MAPUNDA D,(mbuni) huyu alikuwa mnoko balaa.

CHUO,kuna dingi mmoja alikuwa anaitwa MKUMBO alikuwa anafundisha FINANCIAL ACCOUNTING alikuwa anapenda kunyanyasa mabinti wakijichanganya tu amekula kichwa.

wapi MSAKY wa COMMUNICATION SKILLS?
shule ni noma arif.

aisee mwl. mohamed utaly nimemkubali mkuu duuh
 
Mwl machumbe na mwl mtatiro,shule ya mcng majimoto huko serengeti,zam yao wanafunz tulikua tunafka shulen sa 11 alfajiri ili kuwah kuhesab namba,kumbuka kule miaka hyo n pori lkn bora uamke usiku uliwe na fisi lakin usichelewe namba,unapgwa style moja inaitwa shka masikio,stiki kama 30 hapo mgongon,mkuu ilikua heri kuliwa na fisi kuliko kuchelewa namba.

daah mkuu hiyo shika maskio hata mimi ishawah kunikuta
 
wakuu,
katika almost shule zote hua hawakosekani wale walimu wa kali balaa ambaye ukiingia kwenye 18 zake ni lazima ueleze. kwa mfano mimi shule ya msingi lugalo niliposoma kulikua na Mwl.Chavala,Mwl.Kinyogori,Mwl.Bango,Mwl.Getwa,Mwl.Buchwa aisee hawa walimu sitawasahau kamwe. maticha,walikua wana mwaga stiki kama hawana akili nzuri aisee,
then makongo kulikua na Kisarika, Yeyeye,Malongori na Afande Miraji (thou hakua mwalimu). ebana kuna siku tulipata msala asembo baada ya kuimba vibaya wimbo wa taifa, huwezi amini marehemu Afande Miraji single-handedly alizungusha stiki shule nzima kwanzia form 1-6 pale asembo af akarudia raundi mbili. kuna jamaa kesho yake akaomba uhamisho baada ya kukamatwa tena na afande miraji hakwenda zamu akala stiki 15 za adabu. vp mwl gani ushakutana nae hadi leo huwezi msahau?

Mbonan wengi sasa si kichwa cha habari kinasema mmoja?
 
aisee mwalim Nsega kule Kasera Primary school na (mwalim Baruani RIP alikuwa mlemavu)wilaya ya Mkinga zamani ilikuwa wilaya ya Muheza, ni balaa ukichelewa hana adhabu mbadala ni fimbo tu, yaani hawa enzi hizo ukifanya kosa ujue unaenda na alama nyumbani halafu fimbo zao haziishi maumivu haraka
 
1988 to 1991, form 1B, form 2 to form4 group 4 electrical.... Halafu kula na kocha, ticha wa bweni la chabu huyo, halafu kulikuwa na Lihuruku a.k.a Mbungi, si mchezo

eeh wengine ndo tulikuwa tunzaliwa miaka hiyo.
Hakijaharibika kitu lakini school mate
 
Primary. Marehemu Mwl mndolwa ( mlimani primary)..alikuwa anatumia kushoto.

Sec..afande bwenge na wajadi ( jitegemee). Kuna siku Mwl wajadi alinikuta navuta sigara. Taratibu alinishika mkono mpaka discipline office, alinichapa fimbo nyingi sana hats idadi sikumbuki. Halafu kila akiona lazima aniite ananukumbusha tena kosa , nakunichapa tena.
Yaani nilikuwa nukimuona nakimbia saaana mpaka nulipomaliza shule.
 
Kuna mwalimu mmoja anaitwa Mshekangoto kama sijakosea, alisoma butimba ttc! Dada mmoja hivi!
Kwa alichonifanyia namuombea maisha magumu sana popote alipo! Maisha magumu sana!!
 
Mwl. Kipilipili Makumira Primary School
 
bado namkumbuka mwalimu wangu wa primary,the late Mwl. Mbunda .sina hamu na huyu Mwl vile alivyokuwa ananichukia na kuniadhibu kwa bakora pale ilipo bidi.secondary kwangu ilikuwa mdebwedo sana,i had no beef with teachers.
 
wewe kwenu wapi kama si bush????????????? unadhani hapo town ulipo sasa hivi ndio kwenu!!!!!!!!!!!!!!!!!

Sawa sawa mkuu hao ndio wanao jiita watoto wa mjin wana tanua wazee wao wana kufa njaa hko vijijin kwao
 
Nilisikia amefariki but niliwahi kumiona,then nikasikia tena amefariki,ilikuaje jamani du rip,

Yaah huyu jamaa alisha kufa Enzi zake Makongo ilikuwa makongo kweli sio siku hizi watoto wa mama kibaao
 
Pale S/M SAMORA MJIMWEMA alikuwa mwalimu JEMBE,huyu jamaa alikuwa anatufundisha hisabati darasa la 6-7,ilikuwa ukimzingua tu anagonga hadi vichwa.

O/level kulikuwa na MOHAMED UTALY,jamaa alikuwa anafundisha COMMERCE.anauliza swali na anakuchagua ujibu hata kama hukunyoosha kidole,ukipata unagongwa bakora kwamba ulikuwa unajua halafu hunyooshi kidole,

MAPUNDA D,(mbuni) huyu alikuwa mnoko balaa.

CHUO,kuna dingi mmoja alikuwa anaitwa MKUMBO alikuwa anafundisha FINANCIAL ACCOUNTING alikuwa anapenda kunyanyasa mabinti wakijichanganya tu amekula kichwa.

wapi MSAKY wa COMMUNICATION SKILLS?
shule ni noma arif.
Uliposema Samora, umenikumbusha Lizaboni, Kakululu Bar, Foloma... Maana wakati tunasoma hata dalili za samora hazikuwepo... lile eneo kulikuwa kuna kitu tunakiita ''' LUHANU'' kikwetu

 
Back
Top Bottom