Mwalimu Maganga, Katibu Mkuu CWT aliyekataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya arudishwa kwenye Ualimu

Na hiyo ndo ya kufikiria sana kwanini..Na jibu ni moja tu lengo ni kumuathiri kisaikolojia na kumtengenezea mazingira katika kituo kipya ili ashindwe kuhimili kazi
Binadamu sisi baadhi yetu ni wapumbavu sana especially Tanzanians,hata kama una cheo gani kiumbe mtu wote mnategemea pumzi msiyojua inatoka wapi kwanini kukomoana.

Kwani ni lazima sana kutishana eti kwa sababu mtu alitumia uhuru wake?alishajiona mapema hiyo nafasi hatoshi hakutaka kuitia serikali hasara ya kuapishwa kisha kesho atolewe yote hii ni busara alitumia mbona hili halionekani kwa hao wanaotaka kumkomoa?

Wao wataishi milele eti???
 
Waalimu wanachama wa CWT - Chama cha Waalimu Tanzania waonyeshe solidarity na waandamane kupinga viongozi wao kuburuzwa na watawala.
Unadhani wait hawataki fulsa? Kufa kufaana bwana.
 
Pesa sio kisuuza roho!

Huyu bwana ameshinda sana, ndio maana unaona hawa wengine wanavyohangaika kutaka kumdhalilisha. Wanafanya ligi sasa, kiuhalisia wao ndio wanaumia.

Bora kusimamia kile unachokiamini
 
Wa kwetu wanakunywa pombe, sauti nzuri itatoka wapi?
 
Kumbe yupo town,Temeke!!
Mungu anampenda sana....
 
Alikataa TEUZI.. ya MKULU?

ALAFU Waalimu sijui wana AKILI gani, wengi akili zao ni FUPI FUPI.

Ni mjinga pekee ambaye anaweza kukataa Uteuzi wa kutoka Ualimu kwenda Ukuu wa WILAYA.

Huyo alikuwa na TARGET zake na bahati nzuri kajaa kwenye MFUMO.
 
Siyo kila mtu anaweza kuwa mkuu wa wilaya. Ni kazi ambayo unatakiwa uipende ili kutumikia wananchi wa kawaida - mizengwe ni mingi sana kwenye kazi hizo za kisiasa. Ni bora kukataa kuliko kutimuliwa na kupata mfadhaiko wa akili.
 
Mantiki ya taarifa za mwajiriwa kuwekwa hadharani ni zipi?

Alipaswa apewe barua yake kisha aripoti kazini. Kubandikwa kwenye mbao za matangazo ni upuuzi usio na maana.

Mbona kabla ya hapo, vibali vyake havikuwa wazi?

Pathetic!.
Ndiyo watawala wako hao. Siku zote wanatumia njia za aina hii ili kutengeneza mazingira ya kuogopwa.

Ningekuwa mimi ndiyo huyo Mganga, nisingeripoti hiyo tarehe 1 Oktoba. Halafu wakinifukuza kazi yao, poa tu.
 
Siyo kila mtu anaweza kuwa mkuu wa wilaya. Ni kazi ambayo unatakiwa uipende ili kutumikia wananchi wa kawaida - mizengwe ni mingi sana kwenye kazi hizo za kisiasa. Ni bora kukataa kuliko kutimuliwa na kupata mfadhaiko wa akili.
Kwa unamaanisha vetting ya mweshimiwa Rais haikuwa sAwa kumchagua
 
Ualimu ni wito mkuu ukilitambua hilo hautopata tabu katika ualimu.
Huu ubosi ni madaraka tu ni yana mwisho ila ualimu mpaka anakufa ni mwalimu.
 
Ndiyo watawala wako hao. Siku zote wanatumia njia za aina hii ili kutengeneza mazingira ya kuogopwa.

Ningekuwa mimi ndiyo huyo Mganga, nisingeripoti hiyo tarehe 1 Oktoba. Halafu wakinifukuza kazi yao, poa tu.
Ni kama kuna kitabu kimoja nimetoka kukisoma mchana kwamba matatizo huwa yanatengenezwa nawao kisha wanapoyatatua mbele za wananchi wapate misifa
 
Huyo ni shujaa.
Historia itamkubuka.

Heshima na kinafiki zina ukomo.

Lakini kuna heshima ya kujijengea kwa misimamo binafsi huishi
 
Huu hapa 🤣🤣 nahisi alidanganywa na wtu akasahau nyadhifa aliyo nayo ni nyadhifa ya Kuhitaji Kibali kwa mteuzi wa mtu aliyeteuliwa na yule ambaye yeye amemgomea uteuzi wake (Yaani kifupi aliyemuonyesha dharau)
Hata DC ni yale yale tu; even worse. Bora hata hiyo ya michakato ya kiutumishi kuliko maamuzi ya mtu mmoja ambaye ana hiari ya kukubali au kukataa ushauri wowote.
 
Alikataa TEUZI.. ya MKULU?

ALAFU Waalimu sijui wana AKILI gani, wengi akili zao ni FUPI FUPI.

Ni mjinga pekee ambaye anaweza kukataa Uteuzi wa kutoka Ualimu kwenda Ukuu wa WILAYA.

Huyo alikuwa na TARGET zake na bahati nzuri kajaa kwenye MFUMO.
Umeshaambiwa uache upumbavu. Hivi kukataa uteuzi unaonekana huna akili? Kila mtu ana namna yake ya kuishi na inayompa furaha.
 
Umeshaambiwa uache upumbavu. Hivi kukataa uteuzi unaonekana huna akili? Kila mtu ana namna yake ya kuishi na inayompa furaha.
Sawa. Ndio kasharudi kuwa MWALIMU.

Na hapo asubiri kuhamishwa.. na mtu wa hivyo unampeleka kule kule kwenye wilaya aliyoikataa unampeleka anakuwa MWALIMU.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…