Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Mwalimu Nyerere: Hii Katiba ya Tanzania, tukimpata Rais asiye na busara anageuka kuwa Mungu

Angeanzisha mchakato wa kupata katiba mpya basi, mbona alikaa kimya? Ina maana J. K aliona mbali kuliko Nyerere hadi akathubutu kuanzisha huo mchakato japokuwa ulibuma? Na huu nao ni udhaifu mmoja wapo wa baba yetu wa Taifa kwa hiyo tuache tu katiba iliyopo iendelee hadi busara za mheshimiwa Rais zitakapoamua kuanzisha mchakato mwingine wa kupata katiba mpya
 
punguza povu acha kujitekenya jibu hoja hapo mkuu, me sijatukana popote, ...acha kunikusingizia mkuu...jibu maswali yangu..sikatai na wala sitakataa , kuwa yeye ni kiongozi wa nchi hii hilo liko wazi , swali langu ni hili je aliiacha na hivo vote unavosema tanzania hii? kama aliviacha je alimuachia nani wakati mzee mwinyi alitoa hutuba kuhainisha haya?


walokuwepo enzi za Nyerere wtashuhudia maneno yangu, NYERERE NI MWOKOZI na NABII wa Afrika na Tanganyika, mfano Yesu aliponya watu magonjwa yao, aliwasaidia wenye shida na Nyerere alilisha watu kwa aina yake, alilisha watu wengi kuliko Yesu, NYRERE enzi zake alijenga viwanda vya nguo vya Mwatex, Mutex, Urafiki, Sungura na Kilimanjaro, watu walipata ajira, walikula wakashiba, kwenye michezo Enzi za Mwalimu timu ya taifa ilikuwa moto wa kuotea mbali, wachezaji wengi wa timu ya taifa ya wakati huo walitokana na timu ya Pamba, enzi za Mwalimu kulikuwa na Shirika la Reli, Shirika la Posta, Benki ya NBC, TAZARA, ifuko ya hifadhi ya jamii, PPF na shirika la Akiba ya Wafanyakazi [National Provident Fund] leo hii ndo shirika la Hifadhi ya Jamii [NSSF], Enzi za Mwalimu kulikuwa na viwanda vya korosho kila sehemu kunakolimwa korosho, kulikuwapo viwanda vya kuzalisha zana za kilimo na uvuvi, viwanda vya sukari, kama Kilombelo I na Kilombelo II, Mtibwa, TPC, Mgodi wa Almas, viwanda vya tumbaku vya Tabora na Morogoro, Mamlaka za Tumbaku, Mkonge, Pamba, Kahawa, Korosho, Mamlaka ya chai, Nyerere huyu au MWOKOZI WA TANGANYIKA na AFRIKA alianzisha mashirika na makampuni ya umma kama kampuni ya Ngombe wa maziwa (DAFCO), kampuni ya ngombe wa nyama (NARCO) National Insurance Coperation, Shirika la Sukari (SUDECO) Shirika la Maendeleo (NDC) Shirika la Usagaji National Milling Coperation, Shirika la Umeme (TANESCO) Mamlaka ya Madawa, Board ya biashara ya ndani, Board ya biashara ya nje, Board ya Utalii, Shirika la ndege Tanzania (Air Tanzania) Benki ya Rasilimali (TIB) Benki Kuu (BOT) nk.

SWALI LA KWAMBA ALIMUACHIA NANI TUMUULIZE MZEE WA RUKSA.

Mkuu siku zote mtu mwenye maarifa, hekima na busara, anatamani kuwa na karama kama za Mwalimu, maana hekima, busara na maarifa aliyokuwa nayo Nyerere ni mwongozo tosha wakumwongoza binadamu kufikia maisha bora yenye mafanikio, Nyerere hakuwa malaika, jambo ambalo hata yeye mwenyewe alilifahamu ndo maana alikuwa akiwaasa watanzania kuachana na mapungufu yake yote, na tuchukue mema yote, km mmeshindwa au tumeshashindwa wananchi kudai KATIBA ni makosa yetu si ya Nyerere, km ulikuwa ukitegemea Nyerere akufanyie kila kitu umefeli, alifanya alipoweza kadri Mungu alivyomjalia , dunia na watanzania wanajua juhudi zake kwa nchi yake, TUACHE KULALAMA NYUMA YA KIBODI, MWACHENI MZEE WA WATU APUMZIKE
 
Mimi kuna siku niliwahi kumsifia yaani nikikumbuka natamani kubamiza kichwa change kwenye jiwe.Yaani mpaka tufike 2020 tutakonda tuwe kama ng'onda.

Tuendelee kuomba ili Mungu atende maajabu.
 
Bwana yule mtukufu anakataa jina lake kweli kazi tunayo labda tumwite shetani mwenzetu! Haha jamani mi ni malaika kwa maelezo yake na sipendi huo ushetani hata kidogo!
 
Mtakatifu mtakatifu ndio kiongozi wetu kwa sasa
 
wewe ni mwanadini uliyejaa ujinga wa kidini, MUNGU si DINI wala DINI si MUNGU, DINI ni mawazo ya wanadamu juu ya Mungu, Mungu hana mwanzo wala mwisho, DINI zina mwanzo na zina mwisho, zingine zilianzishwa na zishatoweka, lkn MUNGU anaishi, asili ya DINI zote ni UJINGA, na wewe umejaa ujinga wa DINI.

sasa hivi kuna mamilioni ya DINI lkn uovu ndo unazidi kupanda chati, hizo dini zinatusaidia nini? hakuna taifa teule duniani, ambalo MUNGU amelichagua, maandishi hayo ni unafiki wa wayahudi kujipalilia kujenga taifa lao ili liheshimike, mtumishi wa MUNGU au mteule wa Mungu ni mtu yeyote yule aliyechukia na kuachana na uovu, haijalishi ni myahudi, mzungu, mwarabu, Mhindu au mwafrika, ukisema IZIRAELI ni taifa teule hivi hakuna wasenge, wanyang'anyi, mafisadi, wakatili, wasagaji ktk IZIRAELI? km wapo na wao ni wateule?

Kwa kuwa umejaa ujinga wa DINI UNAOKWAMBIA KUWA Malaika, Manabii na Mitume ni watu wenye rangi nyeupe ndio sababu unokupelekea kuona kuwa NYRERE sio Nabii, darasa hili nakupa, Nabii au mtume ni mtu anayetoka kwa Mungu akiwa na ujumbe wa kimungu kwa watu wa wakati wake, kila binadamu ana mapungufu, ili kudhihirisha kuwa huyu ni mtume na nabii ni kutokana na mienendo na tabia yake, Nyerere hakuwa FISADI, WALA MALAYA KM DAUDI NA SELEMANI waliofilisi IZIRAELI, ikagawanyika IZIRAELI na SAMARIa, Nyerere ameongoza, ametuunganisha tukawa wamoja, waliokuja na kuanza kutuachanisha ni MZEE RUKSA aliyekuja na mawazo km yako kutaka nchi iwe ya kidini, hata kuandikisha nchi ikawa ya kidini (Organization of Islamic Cooperation, O.I.C) na umeona madhara yake, msimamo wa Nyerere kimungu ulikuwa sahihi, aliifanya nchi hii kuwa nchi ya AMANI na kuwa kimbilio la watu wote, baada ya kuondoka Nyerere madarakani, walofuatia walianza kuibadilisha nchi kuwa jehanam, kwanza ni laana kumtukana Nyerere.

kusema Nyererre aliwaondoa wakoloni kabla hawajatuendeleza hayo ni mawazo ya KIPUMBAVU, hivi wewe nyumbani utamsubiri mtu aje akujengee mji wako km mwanaume kweli? si kuolewa huko? halafu peleleza ujue chanzo au sababu zilizopelekea kuwapo kwa Muungano, acha maneno ya kwenye kahawa utaonekana kasuku, unadai Nyerere alishindwa kujenga misi ya elimu na Afya? usidakie maneno, ni hivi Nyerere aliendeleza ELIMU na AFYA vizuri, watu wote walisoma bure kuanzia Msingi hadi Chuo kikuu ambapo serikali za leo zimeshindwa kufanya, alitibu bure kuanzia ZAHANATI hadi Hosp za RUFAA pasi na malipo kwa wananchi wote, baada ya Nyerere kuondoka tumekuwa tukizalisha uozo, wezi, mafisadi, wapenda ngono ndio maana maisha yamekuwa hivi yalivyo kwa sababu tumezalisha watu wavivu wasio penda kufanya kazi km wewe,
sibishani na mpumbavu nikaonekana mwenda wazimu, hakuna iziraeli dunian, rudi shule kipapa we, inaonekana una damu za mababu akina Nyerere na mizimu yao ipo juu yako, rudi madrasa ufundishwe maana ya dini ukikosa nenda kipaimara, nenda kwa watu wa kitabu, au waliovuviwa na roho wa kweli watakuambia issa bin maryam na Muhammad nani katajwa zaidi kwenye kitabu chao, ndo maji ulojaza kwa kichwa yatakutoka.
Kuna habar za mungu unazijua ila ww monitress wa wapuzaaji, acha kuzifia maiti kipapa
 
sibishani na mpumbavu nikaonekana mwenda wazimu, hakuna iziraeli dunian, rudi shule kipapa we, inaonekana una damu za mababu akina Nyerere na mizimu yao ipo juu yako, rudi madrasa ufundishwe maana ya dini ukikosa nenda kipaimara, nenda kwa watu wa kitabu, au waliovuviwa na roho wa kweli watakuambia issa bin maryam na Muhammad nani katajwa zaidi kwenye kitabu chao, ndo maji ulojaza kwa kichwa yatakutoka.
Kuna habar za mungu unazijua ila ww monitress wa wapuzaaji, acha kuzifia maiti kipapa
Weka akilini mwako kwamba MUNGU SI MUISILAMU, WALA MHINDU, WALA MKRISTO, wanambia nikajifunze madrasa na kipa Imara, sina muda huo kwani DINI HAINA NAFASI MAISHANI MWANGU, mwenye nafasi kwa maisha yangu NI MUNGU PEKE YAKE, kwa sababu DINI ni tegemeo la watu wajina na wapumbavu, bali MUNGU NI TEGEMEO LA WATU WENYE BURASA, HEKIMA NA MAARIFA,

hivi wewe TANZANIA HII UMEIFANYIA NINI? UNANINI CHA KUJIVUNIA KTK NCHI YAKO? kazi yako ni matusi tu, CHUKI ZAKO KWA MWALIMU HAZITAKUFIKISHA POPOTE. Watanzania watakukumbuka kwa lipi ulilolifanya? Kwa hayo matusi?
 
Mtu akisha kufa hana chake...kama alijua hivo why aliitmia na kama alijua inamapngufu why hakuanzisha mkakati wa kuibadili...simpend kwa vikaul vyake basi tu..
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa hii katiba yetu, inampa mno madaraka makubwa sana, mwalimu alisema kuwa kama tukimpata Rais asiyekuwa na busara, kwa katiba hii Rais anageuka kuwa mungu, unakubaliana na kauli ya mwalimu Nyerere?
ambanisha video ya hotuba hiyo ili tuweze kuchangia
 
Weka akilini mwako kwamba MUNGU SI MUISILAMU, WALA MHINDU, WALA MKRISTO, wanambia nikajifunze madrasa na kipa Imara, sina muda huo kwani DINI HAINA NAFASI MAISHANI MWANGU, mwenye nafasi kwa maisha yangu NI MUNGU PEKE YAKE, kwa sababu DINI ni tegemeo la watu wajina na wapumbavu, bali MUNGU NI TEGEMEO LA WATU WENYE BURASA, HEKIMA NA MAARIFA,

hivi wewe TANZANIA HII UMEIFANYIA NINI? UNANINI CHA KUJIVUNIA KTK NCHI YAKO? kazi yako ni matusi tu, CHUKI ZAKO KWA MWALIMU HAZITAKUFIKISHA POPOTE. Watanzania watakukumbuka kwa lipi ulilolifanya? Kwa hayo matusi?
Same to you boy/girl, jiulize wewe pia umeifanyia nini Tanganyika, au ww agent wa Nyerere,
Nikufanyie nn nchi kwani yenyewe imenifanyia nin hujui nataabika peke yangu acha habar zako, sikulazmishi uwe muislam au mkiristu, whatever na huwez kumpenda Mungu husiemjua, kivip utampenda?
Tazama ishara hizi zitaambatana na waaminio, katafakar hapo ndo utajua namna ya kujenga hoja zako kwangu
 
Alijua katiba yetu ni mbovu na hakuchukua hatua Zozote kurekebisha hilo ni moja kati ya mengi tutakayo mlaumu nayo.

Kusema bila kutenda wakati uwezo wa kutenda unao haisaidii lolote.
Hilo kaliona baada ya kuachia madaraka lakin alipo kuwa ndani ya madaraka asingeweza kuliona
 
Umeona eeh!
Baba wa Taifa, Mwl. JK Nyerere(RIP) alikuwa mwenye hikma na busara sana! Aliliona hili mapema na bila hivo huyo mzee angelifia Ikulu kama angelitaka! Lakini aliamua kung'atuka mapema mwaka 1984!
Leo hii mijitu ya CCM yenye uroho wa madaraka imeamua kuifanya Tanzania ni mali yao na hawataki kusikia habari ya kubadilisha Katiba!
Mwaka juzi kwa maksudi kabisa waliwacheza shere Watanzania kwa kuona kwamba Katiba mpya ingelikuwa kifo cha CCM hivo wakavuruga mchakato wote!!!!!!
Leo Magufuli yuko Ikulu akitimiza utabiri wa Baba wa Taifa kwa kuitawala nchi kidikteta na kibabe akijifanya kama mungu mdogo kwa kuitumia Katiba hii ya kidikteta!!!!
Poleni sana Wabongo!
Huwa nawalaani sana wabunge wengi wa ccm maana bila ujinga wao tungekuwa na katiba inayo enda na wakati tulionao na amabayo ingelijengea heshima taifa na maendeleo kwa ujumla ,lakin kwa kwa ujinga wao wa mshikamano wakaendelea kulipoteza taifa gizani kabisa
 
Back
Top Bottom