Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

Mwalimu wa Madrasa apandishwa Kizimbani kwa tuhuma za kuwachapa fimbo (Ukatili) wanafunzi wa madrasa

Mwalimu wa Madrasa, Musa Bashiru Musa (24) ambaye kipande cha picha jongefu (video) kilisambaa katika mitandao ya kijamii kikimuonyesha akiwapiga fimbo za mikononi wanafunzi wake, amepandishwa kizimbani kujibu tuhuma zake.

Musa ambaye ni mkazi wa Mbagala Kiburugwa, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke na kusomewa mashtaka mawili ya kuwafanyia ukatili watoto wa madrasa, kinyume cha sheria.

Mwalimu huyo amefikishwa mahakamani hapo leo Jumatano, Februari 19, 2025 na kusomewa mashtaka yake na Wakili wa Serikali Mwandamizi, Rabia Ramadhani akisaidiana na Nicas Kihemba, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Vick Mwaikambo.

Wapewe waislamu hii kesi....wajihukumu wenyewe...
 
Mimi hata nikimuona mtu anamchapa Punda wake huwa namuonya na kumwambia huyu ndio anakufanya uende chooni na wanao kama unao, halafu unampiga akiwa kabeba mzigo mzito.
Kweli fimbo sio sababu ya kufundisha na sioni sababu zozote za kupiga
Wanangu siwachapi na wana nidhamu sana kwa sababu nawafundisha

Hawaibi wala kutukana na shuleni wako vizuri pia, wakija nyumbani wanajua wajibu wao, homework kwanza, mengine yanafuata

Kuna watu wanafikiri kupiga ni nidhamu ila utakuta wauwaji wengi ukiwahoji makuzi yao watakuambia tulikuwa tunapigwa mpaka mangumi ya kichwani

Kama wanafuatilia hivyo basi mashule wanapiga mpaka mtoto anakufa
 
Wanazo wanafanya part-time tu tena bure,but huyo mwalimu kwa kweli amekosea thus watoto wengine uchukia madrasa
Halafu mbona huyo ustaadhi anapiga watoto wa kike kwa hasira na nguvu kubwa kuliko watoto wa kiume kwa nini?

Yaani hako kenye hijabu nyeusi alikuwa na hasira nako kama nini na alikapiga kwa nguvu hasa kuliko wa kiume alikatongoza kakamkataa au?
 
Kama hamtaki watoto wenu wagiswe muwe mnakaa nao nyumbani mnawafundisha , haiwezekani mtoto afanye makosa aangaliwe tu.
Katili mwingine huyu hapa. Kwanza unaelewa neno mtoto? Yaani watoto ndiyo mmeona ni wa kuchapwa tu? Nyinyi ndiyo huwafanyia watoto ukatili.

Mtoto kama kafanya makosa, ongea naye, fimbo haijawahi kuwa suluhisho, ndiyo maana tuna watoto watukutu, watoto wa mitaani waliokimbia vipigo majumbani na mateso. Hata hivyo mtoto wangu kafanya mafundisho, hakuwahi nilalamikia kuchwapwa.
 
Mnaomtetea huyo mwalimu wa madrasa, je kama ndiyo tabia yake huwachapa kila mara? Watu wamemchoka ndiyo sababu wakamrekodi mtajuaje?

Kijana wa miaka 24, ila hana huruma na mtoto mdogo wa kike analia, anaendelea kumchapa na hapo mwishoni kamchapa mwilini. Huo ni ukatili, mtoto/watoto wakikosea njia si kupiga ongea nao na kuwakataza Mabaya.

Hivi mtoto mmoja angekuwa mgonjwa na alipochapwa hapo akanyooka mngesema hayo? Tujaribu kuongea na watoto zaidi ya kuwachapa. Mtoto wangu sijawahi mchapa, ila anasifiwa kila anapokuwepo kuwa ana nidhamu sana analelewa vizuri kinidhamu. Nimemuweka karibu, kirafiki na kuongea naye zaidi.
Watanzania tulivyo wanafiki wanakusifikia unajua kulea na unakuja kujigamba?

Ukute wanakuchora 🤣🤣🤣
 
Kwa hiyo mwanao akipigwa au angepigwa namna hiyo, ungeridhia kabisa?

Be honest.
Binti yangu nienda kupiga shuleni mwenyewe fimbo 6. Nisingefabya hivyo asingemaliza shule alianza kwa kumugomea mwl kqenye parade taifa. Nisitoe story zaidi. Qatoto wafundishwe wachapwe ,ila kwa upendo. Period
 
Watanzania tulivyo wanafiki wanakusifikia unajua kulea na unakuja kujigamba?

Ukute wanakuchora 🤣🤣🤣
Ndiyo akili yako ilipoishia? Au kuna nyingine? Labda aina yako na unafiki wako. Nasisi tunaoishi naye hatumuoni? Walimu wake, yaani watu wote ni wanafiki hadi sisi wenyewe?
Acha roho mbaya ndugu, safisha roho hiyo ili mambo yaende.

Mwenzako ndiyo hivyo mtoto wangu ana nidhamu sana na namshukuru Mungu kwa hili. Hicho ulichosema hakibadilishi kuwa yeye ana nidhamu. Pole lea mtoto kwenye maadili halafu sukutua hiyo roho kaka.
 
Mufti wa Zanzibar na Mbagala Tena !??....
Kaandika kabisa na kutaja akionya ma ustaadhi wa Zanzibar kuwa wasifanye kama huyo wa Mbagala Dar es Salaam

Katoa waraka kabisha kuwa huyo maalim wa Mbagala Dar es Salaam anachafua na kuharibu taswira ya uislamu


Nashindwa ku attach tamko lake mwenye uwezo aweke humu
 
Binti yangu nienda kupiga shuleni mwenyewe fimbo 6. Nisingefabya hivyo asingemaliza shule alianza kwa kumugomea mwl kqenye parade taifa. Nisitoe story zaidi. Qatoto wafundishwe wachapwe ,ila kwa upendo. Period
Hapo ni wewe ulimpiga.

Ndio maana ulikuwa na Amani.

Vipi uone mtu baki anampiga mwanao mwenye umri kama wa hawa watoto?

Je utaona ni sawa tu?
 
Mimi hata nikimuona mtu anamchapa Punda wake huwa namuonya na kumwambia huyu ndio anakufanya uende chooni na wanao kama unao, halafu unampiga akiwa kabeba mzigo mzito.
Kweli fimbo sio sababu ya kufundisha na sioni sababu zozote za kupiga
Wanangu siwachapi na wana nidhamu sana kwa sababu nawafundisha

Hawaibi wala kutukana na shuleni wako vizuri pia, wakija nyumbani wanajua wajibu wao, homework kwanza, mengine yanafuata

Kuna watu wanafikiri kupiga ni nidhamu ila utakuta wauwaji wengi ukiwahoji makuzi yao watakuambia tulikuwa tunapigwa mpaka mangumi ya kichwani

Kama wanafuatilia hivyo basi mashule wanapiga mpaka mtoto anakufa

Ndiyo akili yako ilipoishia? Au kuna nyingine? Labda aina yako na unafiki wako. Nasisi tunaoishi naye hatumuoni? Walimu wake, yaani watu wote ni wanafiki hadi sisi wenyewe?
Acha roho mbaya ndugu, safisha roho hiyo ili mambo yaende.

Mwenzako ndiyo hivyo mtoto wangu ana nidhamu sana na namshukuru Mungu kwa hili. Hicho ulichosema hakibadilishi kuwa yeye ana nidhamu. Pole lea mtoto kwenye maadili halafu sukutua hiyo roho kaka.
Food for thought. Watanzania unatujua hatukuambii ukweli mpaka mambo yaharibike ndio tunaanza kunyoosha vidole.

Wewe hatuwezi kuikubali rating ya nidhamu ya mtoto wako mwenyewe kwasababu you can not objective. Kila mzazi anaona mtoto wake hana shida.

Hongera umepata mtoto ukiongea anasikiliza.

Haya mambo yana bell curve. There are extremes at both ends. Sasa kama wako yuko kushoto kuna wengine wako kulia mwa hiyo curve, hawasikii maneno ila wanarespond to bodily pain. Usitake system yako i apply kwao.

Nimekupa changamoto kidogo tu bingwa wa malezi umenivamia personally kuwa nina roho mbaya. Kwema huko? Unaweza kweli ukaongea na mtoto mtukutu akakuelewa kama challenge yangu tu umeshindwa kuipangua kiutu uzima?
 
Back
Top Bottom