TEAM 666
JF-Expert Member
- Dec 7, 2017
- 4,399
- 8,594
Taarifa za ndani ni kwamba bado Simba wanajadili mahitaji ya Chama kwa ajili ya mkataba mpya.
Inaelezwa kuwa nyota huyo anahitaji pesa ya usajili shilingi milioni 250 kwa mkataba wa miaka miwili na mshahara wa Shilingi milioni 16 kwa mwezi. Siyo uongo kuhusu Yanga kumtaka Chama.
Taarifa tulizonazo ni kwamba Yanga wametenga dau nono zaidi ya Simba lakini tatizo ni kwamba tayari Chama ana ofa kubwa zaidi Afrika Kusini na Uarabuni na iwapo atashindwana na Simba, hatamani kujiunga na timu yoyote ya Tanzania.
Lolote linaweza kutokea, lakini ni wazi kuwa Simba hawapo tayari hata kidogo kumpoteza Chama.
Zipo fununu kuwa dau walilotenga Yanga linafikia Milioni 300 na mshahara wa milioni 18 kwa mwezi, lakini ipo nadharia pia kwamba Yanga wanawachezea Simba mchezo ili watumie pesa nyingi zaidi ya walivyopanga katika dili hilo.
Inaelezwa kuwa nyota huyo anahitaji pesa ya usajili shilingi milioni 250 kwa mkataba wa miaka miwili na mshahara wa Shilingi milioni 16 kwa mwezi. Siyo uongo kuhusu Yanga kumtaka Chama.
Taarifa tulizonazo ni kwamba Yanga wametenga dau nono zaidi ya Simba lakini tatizo ni kwamba tayari Chama ana ofa kubwa zaidi Afrika Kusini na Uarabuni na iwapo atashindwana na Simba, hatamani kujiunga na timu yoyote ya Tanzania.
Lolote linaweza kutokea, lakini ni wazi kuwa Simba hawapo tayari hata kidogo kumpoteza Chama.
Zipo fununu kuwa dau walilotenga Yanga linafikia Milioni 300 na mshahara wa milioni 18 kwa mwezi, lakini ipo nadharia pia kwamba Yanga wanawachezea Simba mchezo ili watumie pesa nyingi zaidi ya walivyopanga katika dili hilo.