Mwami Theresa Ntare VI wa Heru - Chifu wa kwanza mwanamke

Mwami Theresa Ntare VI wa Heru - Chifu wa kwanza mwanamke

Mme wa mwami ntare ni George Ntare siyo msukuma aisee.

Mkuu, Kilaga amejibu vema, Mwami Theresa Ntare alioana na George Shinganya, Ntare ni baba wa Mwami Theresa. Alitumia Jina la familia yake (wazazi) ambao ndio wenye asili ya uchifu kwa Waha wa Heru Juu.

Vv
 
Nimevutiwa sana kujua Historia ya mwanamke shupavu ambaye alikuwa ni mtawala wa kutoka katika kabila la waha wa Jamii ya kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu.

View attachment 338139

Ambapo zama zile jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake, Mwanamama huyu aliweza kuwa Kiongozi wa Jamii ya Heru huko Kasulu. Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni mkuu wa machifu akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958.Makabidhiano yalifanyikia shule ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Sina details nyingi za huyu mama, WanaJF kama kuna anayefahamu zaidi kuhusu huyu mama shupavu basi atupe historia yake.

*Mwami ZITTO KABWE sasa hivi ndiye Chifu wa Heru.
Ngoja aje Mzee Mohamed Said...
 
Kwa mujibu wa historia niliyoisikia ni kuwa enzi za kale wabantu hawakuwa na utawala wa mwami/wami zaidi ya machifu tu na watu walikua wakiishi kijamaa. Lakini jamii ya wahamiti ambo ni pamoja na watutsi walikuwa wakivamia jamii za wabantu ma kusimika tawala zao kila walipovamia kwakuwa ndiyo asili yao ndio maana hata huko Rwanda na Burundi wao tu ndio wanataka watawale. Sasa hawa watutsi wakivamia Buha na sehemu nyingine za Kagera na kwingineko na kusimika falme zao ndio maana mwami Ntare sio chimbuko au ukoo wa Buha Bali ni Mtutsi
Unaweza kusema kweli ingawa ukweli wako ni nusu. Watawala wa nchi za Rwanda, Burundi, Buhaya, Bunyankole, Bunyambo na Buha, walivyamia sehemu hizo lakini walichanganyika na wenyenyi na kuunda MFUMO wa utawala ambao uliwafanya wakatawala kwa karne nying. Hivyo kudai kwamba ni Wanyarwanda au Warundi, (Watusi) ni nusu ukweli. Na ukwe kwamba nusu ukweli ni hatari.
 
Wanyarwanda Warundi, Waha , Wahangaza na Wanyamulenge ni jamii moja, utakuta clan moja ya Waha imetawanyika hadi nchi nyingine ama Rwanda au Burundi.

Kumbukeni tu kuwa Rwanda na Burundi zilikuwa ndani ya Germany East Africa hadi baada ya vita ya kwanza ya dunia pale ambapo Mwingereza alipomzawadia Mfalme wa Ubelgiji hizo Rwanda na Burundi baada ya kumsaidia kumuondoa Mjerumani ktk Africa ya Mashariki.

Vv
 
Mwami Theresa Ntare alifunga ndoa na George Shinganya ambao kwa pamoja walijaliwa kupata watoto kadhaa.
Kwa mila za Kiha, Mwami haolewi. Akiolewa inabidi ahame milki yake ya Uchifu ili akawe mke wa huyo muoaji.
Hivyo basi, Mwami Ntare hakuolewa na Bw. George Shinganya. Familia ya Mwami ndiyo iliyolipa mahari kwa familia ya Bw. George Shinganya.
Baadaye ndoa hiyo iliingia tafrani na Mwami Theresa Ntare akaoana na Mwami Louis Dantes Ngua wa Ufipa.
Hivyo basi, Mwami Theresa Ntare hakuwahi kuwa mke wa Chief Makwaia wa Usukuma.
Kwenye Baraza la mwanzo la Mawaziri, Mwami Theresa Ntare alikuwa Naibu Waziri.

Unatuchanganya hapo kidogo
kulikuwa na mwami wangapi?
ufipa walikuwa na mwami?
Makwahia hakumuoa Theresa?
Baraza la mwaziri la Nyerere ndo mwami Theresa alikuwa naibu waziri?
 
Unaweza kusema kweli ingawa ukweli wako ni nusu. Watawala wa nchi za Rwanda, Burundi, Buhaya, Bunyankole, Bunyambo na Buha, walivyamia sehemu hizo lakini walichanganyika na wenyenyi na kuunda MFUMO wa utawala ambao uliwafanya wakatawala kwa karne nying. Hivyo kudai kwamba ni Wanyarwanda au Warundi, (Watusi) ni nusu ukweli. Na ukwe kwamba nusu ukweli ni hatari.
Unaweza kuleta ukweli kamili mkuu? Hii ni historia niliyosimuliwa na wazee wa huko huko. Ndio maana sehemu za kibondo pamoja na kuwa waha wapi hakukuwa na Mwami kule watu walikuwa wanaishi kijamaa tangu zamani. Hawa wahamiti ni jamii kubwa iliyokuja huku kwetu kutokea kaskazini mwa bara la Afrika miaka mingi na Watutsi ni miongoni mwa jamii ya Wahamiti. Ukisoma hata kitabu cha Zamani mpaka siku hizi utayakuta mkuu haya mambo
 
Unaweza kuleta ukweli kamili mkuu? Hii ni historia niliyosimuliwa na wazee wa huko huko. Ndio maana sehemu za kibondo pamoja na kuwa waha wapi hakukuwa na Mwami kule watu walikuwa wanaishi kijamaa tangu zamani. Hawa wahamiti ni jamii kubwa iliyokuja huku kwetu kutokea kaskazini mwa bara la Afrika miaka mingi na Watutsi ni miongoni mwa jamii ya Wahamiti. Ukisoma hata kitabu cha Zamani mpaka siku hizi utayakuta mkuu haya mambo
Cha msingi cha kutambua ni kwamba, watu wa nchi hizi tunazozikalia karibu wote ni Wavamizi labda wachache kama Wahdzabe, ambao wamekaa hapa kwa zaidi ya miaka elfu 2. Hivyo vitabu unavyovisema kama Zamani mpaka Siku hizi vimevufiwa na kasumba ya watu weupe ya kumwona Mtitu hasa kama mtu nusu. Hiyo iliwafanya wabuni msamiati wa Wahamiti ambao, katika maoni yao, wana kaasili ka weupe maana wanatokea Abisinia. Na tukisoma historia hiyo hiyo ndiyo inataka tuwaone Watutsi na Wahutu kama makabila mawili tofauti. Na kwa mtiririko huo, kuna watakaojidai na Waha original jambo ambalo si kweli. Haya unayoyaita makabila ni vinchi vidogo vidogo ambavyo vimeundwa na vikabila tofauti. Kwa kukazia hoja yangu, nakuomba utafute neno linalotafsiriwa kama kabila kwa lugha ya Kiha na uone linawakilisha kikundi gani katika jamii husika. Unaposema utawala wa kijamaa maana yake wale watu walikuwa hawajafikia hatua ya kuwa Wajamii? Je walibaki kuwa watu wa nasaba moja tu?
 
Nimevutiwa sana kujua Historia ya mwanamke shupavu ambaye alikuwa ni mtawala wa kutoka katika kabila la waha wa Jamii ya kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu.

View attachment 338139

Ambapo zama zile jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake, Mwanamama huyu aliweza kuwa Kiongozi wa Jamii ya Heru huko Kasulu. Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni mkuu wa machifu akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958.Makabidhiano yalifanyikia shule ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare.

Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Sina details nyingi za huyu mama, WanaJF kama kuna anayefahamu zaidi kuhusu huyu mama shupavu basi atupe historia yake.

*Mwami ZITTO KABWE sasa hivi ndiye Chifu wa Heru.
Ndugu zangu,
Nikifahaiana na huyu Bi. Mkubwa Theresa Ntare na mumewe Mzee Ngua.
Ninayo machache In Sha Allah nitakuwekeeni hapa nikitulia.
 
Ndugu zangu,
Nikifahaiana na huyu Bi. Mkubwa Theresa Ntare na mumewe Mzee Ngua.
Ninayo machache In Sha Allah nitakuwekeeni hapa nikitulia.
Sasa huyo Mzee Ngua na ana asili ya kichifu na ni Mfipa. Chief Ngua ni mume wa pili wa Mwami Theresa Ntare. Mume wa kwanza wa Mwami Ntare aliitwa George Shinganya.

Vv
 
Ngoja aje Mzee Mohamed Said...
Kwani umesikia na yeye ni wa ma mdogo? Waliopigania uhuru nchi hii Mohamed Said anawajua ndugu zake tu wa upande wake tu.

Ukisikia anamtaja mjukuu wa Sarah, basi ujue ni kwa ubaya tu. Mfano ukisikia limetajwa J.K. Nyerere ujue itaambatana na kashfa kibao alivyo kwamisha harakati zao. Never positive
 
Nimevutiwa sana kujua Historia ya mwanamke shupavu ambaye alikuwa ni mtawala wa kutoka katika kabila la waha wa Jamii ya kitutsi, ukanda wa Kasulu sehemu za Heru Juu.

Heru Juu
Heru ni eneo linalopatikana Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma.Heru imegawanyika katika sehemu mbili nazo ni Heru juu na Heru chini. Heru juu inaundwa na vijiji vya Munyegera,Heru na Buha pamoja na vijiji vya ukanda wote wa juu kuelekea Buhigwe. Heru Chini inaundwa na vijiji vya Nyansha, Mgandazi, Ntare, Bugaga, Nyumbigwa, Nkundutsi, Zeze na vijiji vyote vya maeneo ya Kasulu ya chini.

Asili ya kabila la Waha ni kijiji cha Buha kinachopatikana eneo la Heru Juu. Waha kutoka Buha walisambaa na kuja eneo la chini la Kasulu (Heru Chini). Muingiliano huu wa Wanyaheru kutoka Buha (Heru juu) na kushuka chini ya vilima vya Bugaga, Nkundutsi hadi kuelekea Zeze kulileta muingiliano wa Lugha na kuzaa tofauti za matamshi baina ya Waha wa Buha(Wanyaheru) na Waha wa Maeneo ya Chini. Lakini kihistoria Wanyaheru (Buha) ndiyo Waha asilia na Kiha cha Heru (Buha) kina tofauti ya kimatamshi na jamii zingine za Waha. Na kiha cha Buha/Heru ndicho kiha asilia. Usisahau pia pale ndipo kuna Ngoma za asili za waha zinazojulikana kama NGOMA ZA BWAMI.

Mwami Theresa Ntare
Mwami Theresa Ntare alifunga ndoa na George Shinganya ambao kwa pamoja walijaliwa kupata watoto kadhaa. Kwa mila za Kiha, Mwami haolewi. Akiolewa inabidi ahame milki yake ya Uchifu ili akawe mke wa huyo muoaji. Hivyo basi, Mwami Ntare hakuolewa na Bw. George Shinganya. Familia ya Mwami ndiyo iliyolipa mahari kwa familia ya Bw. George Shinganya. Jina la Shinganya likaondolewa na akaitwa George Ntare. George Ntare alikuwa akiishi maeneo ya karibu na barabara inayoelekea Munyegera - Kati ya ilipo shule ya msingi na Kahaga Dispensary (kulikuwa na soko hapo kati miaka ya 1985). Baadaye ndoa ya Mwami Theresa Ntare na George iliingia tafrani na Mwami Theresa Ntare akaoana na Mwami Louis Dantes Ngua wa Ufipa. Kama kumbukumbu zangu ziko sawa, nyumba ya Mwami Ntare haikuwa umbali mrefu na lilipo kanisa la Roman Catholic, Heru Juu kama unatokea Mapanda Njia au zilipo ofisi za kijiji.

Zamani zile jamii nyingi za Kiafrika zilitajwa kuwaweka nyuma wanawake, Mwanamama Mwami Theresa Ntare aliweza kuwa Kiongozi wa Jamii ya Heru huko Kasulu. Hakuishia hapo, mama huyu aliweza kushika wadhifa mkubwa ambapo alikuwa ni mkuu wa machifu akipokea kijiti kutoka kwa Chifu Petro Itosi Marealle mwaka 1958. Makabidhiano yalifanyikia shule ya Mzumbe, na mpaka sasa Mzumbe kuna bweni linaitwa Ntare. Mwami Theresa Ntare alikuwa ni mmoja ya Wabunge wachache wa Baraza la Kutunga Sheria la Tanganyika kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika.

Tulashashe numbu, nzembagiza nu mukubhi!

Tuendeleze historia kutoka hapa sasa kwa wanaoifahamu kwa undani Zaidi.

Credit to JF particularly Chachu Ombara, fundimchundo, and Vyamavingi
 
Pia alikuwa mke wa one of the Sukuma Chiefs - I think Chief Kidaha Makwaia. Mwalimu Nyerere alimteua Chief Makwaia kuwa Area Commissioner baada ya Uchief kufutwa Tanganyika mwaka 1962 na wote waliokuwa ma-chief wakawa ex-chiefs.
Mwaka 1965 ex-chief Makwaia alikuwa area commissioner wa Arusha na Mwami Theresa Ntare alikuwa mashuhuri katika shughuli za jamii na social circles za Arusha Mjini.
Sio kweli mwami thereza ntare alitawazwa uchifu baada baba yake mwami ntare kukosa mtoto wa kiume ktk uzao wake hivyo baada kutawazwa uchifu ilibidi atafutiwe mchumba kutoka ukoo wa chifu lusimbi wa kalinzi hivyo akawa ameolewa na kijana wa kitutsi kutoka kalinzi akiitwa george
 
Sio kweli mwami thereza ntare alitawazwa uchifu baada baba yake mwami ntare kukosa mtoto wa kiume ktk uzao wake hivyo baada kutawazwa uchifu ilibidi atafutiwe mchumba kutoka ukoo wa chifu lusimbi wa kalinzi hivyo akawa ameolewa na kijana wa kitutsi kutoka kalinzi akiitwa george

Yeye ndiye aliyeoa mkuu.
 
Sio kweli mwami thereza ntare alitawazwa uchifu baada baba yake mwami ntare kukosa mtoto wa kiume ktk uzao wake hivyo baada kutawazwa uchifu ilibidi atafutiwe mchumba kutoka ukoo wa chifu lusimbi wa kalinzi hivyo akawa ameolewa na kijana wa kitutsi kutoka kalinzi akiitwa george

Hii umeiweka sawa kabisa manyovu 1. Binafsi nilishakutana na Mume wa Mwami Theresa miaka ya 1983 hapo kijijini Heru Juu. Sina uhakika kama bado yu hai au alishatangulia mbele za haki!
 
Hii umeiweka sawa kabisa manyovu 1. Binafsi nilishakutana na Mume wa Mwami Theresa miaka ya 1983 hapo kijijini Heru Juu. Sina uhakika kama bado yu hai au alishatangulia mbele za haki!
George Shinganya alishafariki miaka ya tisini na pale Kwenye lile Jumba lao yamebaki magofu tu. Enzi za Mporogomyi akiwa mbunge wa jimbo lile alikuja kuchukua mafuvu ya Mwami Ntare na George Shinganya na haijulikani alienda kuyafanyi nini japo inasemekana yalimsadia kushinda chaguzi mbali mbali katika jimbo lile enzi hizo Kasulu Magharibi. Kumbuka George alipokfariki alienda kuzikwa karibu na kaburi la Mwami Ntare.
 
Back
Top Bottom