Tetesi: Mwamposa mbioni kuinunua E-FM, TV-E

Tetesi: Mwamposa mbioni kuinunua E-FM, TV-E

Afadhali, atuachie ITV yetu tutazame Al Jazeera usiku mpaka asubuhi!
Mkuu, kwanini usiangalie channel ya Al Jazeera hadi usubiri huko kuonjeshwa na ITV?
Binafsi hiyo ndiyo Channel yangu pendwa, kila news hour lazima niangalie.
 
Alidandia gari kwa mbele, hii habari itamfurahisha sana Diamond.
Nadhani siyo suala tu la mtu kukurupuka. Main stream media zinapitia changamoto kubwa sana kufuatia mabadiliko ya kasi kubwa ya teknolojia.

Ujio wa social networking services na blogosphere umepunguza sana faida za mainstream media.

Wanaoyumba kwa kipato siyo EFM na TVE pakee, Sahara media na Ippmedia Cloudsmedia group, wana kilio cha kimya kimya, Makampuni ya magazeti mengi yamefungwa.
 
Juzi napita kawe, nawaon wamama wamelala kwenye kordo za watu na watoto wao wakisubiria mkesha.
Ni wamama ambao ukiangalia hali zao zinatia huruma sana. Hawana hela za kulipia Vyumba vya wageni hata chakula sa ingine. Ila wanaenda kuacha hela zote tena kwa mtume wao ambae ni Billionea .

Naumiaga sana namna ya hao wamama kwa ujinga wao wanavyowatesa watoto kukesha na kuambatana nao kila mahali ilihali mtoto hajafika umri wa maamuzi.
Wajinga ndio waliwao
 
Hapo unakuta money withdrawn for family use kwenye kampuni ndio kipengele kikuu kinachokwamisha taasisi. Nimewahi kufanya kazi kwenye taasisi za kifamilia kama Hizo. Sikukuu kama christmas muhasibu unaforciwa kufanya transfer ya 15m kwa kila mwana familia ( kwa sikuku ya siku moja) na ilihali mishahara ya staff hawatoi approval. Unakuta familia inainyonya kampuni
Yaan Mkuu acha kabisa safari ni ndefu hasa kwa familia zetu ubia wa kibongo... Ukiwa Muhasibu ni ugomvi ugomvi ... Ukitoa baadae unaulizwa nani alikuruhusu... Aliyekuja kudai naye ana share na sauti duuuu...
 
View attachment 3184579

Katika kilichoonekana kama kusogeza ‘huduma’ karibu kwa waumini wa kanisa lake, Askofu na Mtume Boniface Mwamposa yupo kwenye mchakato wa kuinunua EFM Company Limited.

EFM ni kampuni iliyosajiliwa kama chombo cha habari, ikiwa na umiliki wa Redio na Televisheni.

Mwamposa na Mkurugenzi wameshibana…
Mkurugenzi wa EFM Bwana Francis Ciza maarufu kama Majizzo (Mume wa muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’) wamekuwa wakishirikiana kwa ukaribu na Askofu Mwamposa katika kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mikutano na ibada zinazoendeshwa na Mwamposa kwa kipindi kirefu.

Baada ya kufanya kazi pamoja kwa kipindi kirefu, hivi sasa wapo kwenye mazungumzo ya kumuuzia media hiyo Mwamposa.

Nimetaarifiwa kwamba vikao vya mauziano hayo vinafanyika kwa siri nyumbani kwa Majizzo, huku dau likiwa bado halifahamiki lakini ikielezwa Majizzo anataka dau kubwa linalokwamisha taratibu za mauziano kuanza.

EFM Radio imemshinda Majizzo!
Kwa kipindi kirefu kumekuwa na minong’ono ya wafanyakazi kushindwa kulipwa mishahara kwa wakati, ikisemekana wanaolipwa bila kusumbuliwa ni wale watangazaji wenye majina makubwa pekee, huku wale wachanga wakipitia wakati mgumu kimalipo.

Taarifa za uhakika ni kwamba redio hiyo imemshinda Majizzo, changamoto za uendeshaji zimemuelemea na inasemekana kama sababu kuu ya yeye kufikia uamuzi wa kumuuzia Mwamposa kampuni yote hiyo ya habari iliyokuja kuzipa chachu redio kongwe miaka ya mwanzoni mwa uzinduzi wake.

Majizzo siye mmiliki pekee…
Taarifa za usajili wa kampuni zinaonesha kumilikiwa na ndugu watatu, yeye Majizzo (Francis Ciza 40%) ndugu zake kwa upande wa baba yake mlezi Mzee Ciza… Jean Ciza 40% pamoja na Justine Ciza 20%

Wenu katika unyetishaji, mimi na chanzo changu,

Nifah.
Uko vizuri kwenye hiki kitengo, ngoja tusubirie.
 
View attachment 3184579

Katika kilichoonekana kama kusogeza ‘huduma’ karibu kwa waumini wa kanisa lake, Askofu na Mtume Boniface Mwamposa yupo kwenye mchakato wa kuinunua EFM Company Limited.

EFM ni kampuni iliyosajiliwa kama chombo cha habari, ikiwa na umiliki wa Redio na Televisheni.

Mwamposa na Mkurugenzi wameshibana…
Mkurugenzi wa EFM Bwana Francis Ciza maarufu kama Majizzo (Mume wa muigizaji Elizabeth Michael ‘Lulu’) wamekuwa wakishirikiana kwa ukaribu na Askofu Mwamposa katika kurusha matangazo ya moja kwa moja ya mikutano na ibada zinazoendeshwa na Mwamposa kwa kipindi kirefu.

Baada ya kufanya kazi pamoja kwa kipindi kirefu, hivi sasa wapo kwenye mazungumzo ya kumuuzia media hiyo Mwamposa.

Nimetaarifiwa kwamba vikao vya mauziano hayo vinafanyika kwa siri nyumbani kwa Majizzo, huku dau likiwa bado halifahamiki lakini ikielezwa Majizzo anataka dau kubwa linalokwamisha taratibu za mauziano kuanza.

EFM Radio imemshinda Majizzo!
Kwa kipindi kirefu kumekuwa na minong’ono ya wafanyakazi kushindwa kulipwa mishahara kwa wakati, ikisemekana wanaolipwa bila kusumbuliwa ni wale watangazaji wenye majina makubwa pekee, huku wale wachanga wakipitia wakati mgumu kimalipo.

Taarifa za uhakika ni kwamba redio hiyo imemshinda Majizzo, changamoto za uendeshaji zimemuelemea na inasemekana kama sababu kuu ya yeye kufikia uamuzi wa kumuuzia Mwamposa kampuni yote hiyo ya habari iliyokuja kuzipa chachu redio kongwe miaka ya mwanzoni mwa uzinduzi wake.

Majizzo siye mmiliki pekee…
Taarifa za usajili wa kampuni zinaonesha kumilikiwa na ndugu watatu, yeye Majizzo (Francis Ciza 40%) ndugu zake kwa upande wa baba yake mlezi Mzee Ciza… Jean Ciza 40% pamoja na Justine Ciza 20%

Wenu katika unyetishaji, mimi na chanzo changu,

Nifah.
Hehehe
 
Back
Top Bottom