Duh...!, nadhani hili ni bandiko la hisia tuu, CCM na serikali yake haiwezi kuwa na uoga wa kushindwa uchaguzi kihivyo kwasababu Rais Magufuli sasa anakubalika sana hadi wapinzani wanaacha vyama vyao kwa hiyari yao na kumuunga mkono.
Tena na kwa track record ya utendaji wake uliotikuka so far, ushindi wa kishindo kwa CCM ni uhakika!, wembe ule ule uliotumika kuwanyoa wapinzani kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, ndio utatumika kuwanyoa kwenye uchaguzi mkuu.
Kwa mujibu wa sheria iliyounda Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC ni tume huru japo sio shirikishi.
Uchaguzi unaendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni za uendeshaji uchaguzi huru na wa haki tena tutashauri kwa uchaguzi wa mwaka huu, mawakala waruhusiwe hadi kwenye tallying.
Kama uchaguzi unandeshwa very transparently kwa kura zote hadi za rais kubandikwa vituoni.
Tutawashauri mawakala wote wa vyama vyote wapewe smart phones na ku scan matokeo ya kila kituo na kutuma kwenye tallying centres za kila chama.
Ili kuthibitisha hakuna goli lolote la mkono, hakuna sababu yoyote ya NEC kuzuia independent tallying centres, ila haziruhusuwi kutangaza matokeo, ila matokeo yasipotally then they'll have a strong case to challenge with Documentary evidence, numbers don't lie.
Matokeo ya mwisho ya uchaguzi mkuu ni ushindi wa kishindo cha asilimia 93% kwa CCM, hizo asilimia 7% ni Pemba na yale majimbo mawili ya Zanzibar ambayo yatakwenda ACT!.
Kanuni ya ushindi ni "the end justifies the means"
" the winner takes it all, the losers standing small"
Kwa vile kila mtu ameishajua CCM itashinda uchaguzi, bado naendelea kuisisitiza hoja hii
Wanabodi. Kwa Kasi Hii ya Rais Wetu Mpendwa, Dr. John Pombe Joseph Magufuli na Falsafa yake ya "Hapa Kazi Tu", na kama hiki tunachokiona sasa, sio nguvu ya soda tuu, yaani ataendelea kwa kasi hii hii hadi 2020, kuna haja kweli ya kufanya tena uchaguzi wa rais?. Kwa maoni yangu, uchaguzi wa...
P