Uchaguzi 2020 Mwana JamiiForums Happiness Essau, achukua fomu ya Ubunge Jimbo la Bukoba

Uchaguzi 2020 Mwana JamiiForums Happiness Essau, achukua fomu ya Ubunge Jimbo la Bukoba

Sorry mkuu nilipitia comment za huyo dada niliona anasema ni afisa habari wa jamii media...

Kwahiyo Wewe utakuwa ukiona tu kila ' Kinachokomentiwa ' hapa ni cha Ukweli kisha nawe unakibeba hivyo hivyo kama Inzi wa Soko la Tandale?
 
Mbona naitafuta sana humu ( hapa ) hiyo ID yenye Jina lake la Happiness Essau ili niwe naona Michango yake ya Akili lakini haionekani Mkuu?
Mimba za utotoni ni Janga la Taifa. Idadi ya watoto wanaokatisha masomo kwasababu hii inazidi kuongezeka mara dufu. Athari ya janga hili ni zaidi ya hawa mabinti kukosa elimu. Mabinti wetu hawa hata wakipata nafasi ya kurudi tena shule zaidi ya 80% hawawezi kumudu kwasababu ya aina ya familia wanazotoka, jamii inayowazunguka na walimu wetu walivyoandaliwa.

Suluhisho la hili tatizo ni zaidi ya kurudi shule, suluhisho ni kushughulikia sababu za tatizo na kuangalia ni wapi tumekosea kama taifa na kujisahihisha. Tulipokosea sio kutokuruhusu hawa mabinti kuendelea na shule, tulipokosea ni pengine....tupasahihishe hapo. Tusishabikie tu kauli ya Rais kama ndiyo sababu au suluhisho la mimba za utotoni.

Mimi kama ningekua ni mwalimu wa rika la hawa watoto hakika nisingependa kufundisha darasa moja lenye mchanganyiko wa binti wa miaka 12 na mama wa miaka 12 kwasababu handling yao ni tofauti. Walimu wetu wameandaliwa kwaajili ya kufundisha watoto, hawa mabinti zetu wanaokuwa mama ktk umri mdogo wanahitaji waalim maalum. Lakini mimi pia kama mzazi nisingependa binti yangu wa miaka 12 kufundishwa darasa moja na binti mwingine wa miaka 12 ambaye ameshakuawa mama kwasababu sitaki aone kama hilo ni jambo la kawaida. Naamin hata mabinti wengine waliokwisha zaa na wanasoma/walasoma shule binafsi hawajulikani kinaga ubaga kama wana watoto.

Sababu kubwa ya mimba za utotoni sio kubakwa, takwimu zinaonyesha 80% wanafanya ngono kwa hiari. Ninaamini wengi walioepuka ngono na mimba za utotoni ni kwasababu ya woga/hofu ya Mungu na wazazi. Woga na hofu ndio sababu kubwa ya mabinti wengine kutokujiingiza ktk ngono na kutokupata mimba, elimu ya uzazi, mazingira bora na sababu nyingine vinafuatia kwa uzito mdogo. Kwahivyo mabinti zetu wanapaswa kuogopa, wanapaswa kuwa na hofu ya ngono na mimba kwa ujumla, kama hawana hofu na woga hata ifanyike nini haitasaidia. Hawa mabinti tunaowatetea hawana woga kabisa kabisa na ngono, hawaogopi wababa wala wababu!

Kama tunavyopaza sauti kuwatetea warudi shule, vivyo hivyo tupaze sauti kuwakemea dhidi ya ngono ktk umri mdogo, tuwatie woga, tuwatie hofu, waache tamaa. Wao wakikataa wanaume hawana nguvu dhidi yao! Tunavyoendelea kumkanya Rais dhidi yao, tunavyoendelea kuwakanya wanaume dhidi yao tunawafanya wajione vulnerable wakati nguvu ya kukataa na kutokupata mimba iko ndani yao na si kwa kundi lingine lolote!
ca028500cb9173860716291a1476618e.jpg
 
Roving Journalist, Ok noted

Chama kinatiwa najisi cha mapinduzi

Chama kimegeuzwa sehemu ya kuonyeshea maigizo

Dunia ina vituko sana na vichekesho zaidi

Wasiojielewa na mbumbumbu wote wanachukua fomu ili wakatunge sheria zikatumike mahakamani

Kuna watia nia wengine ukiwaangalia sura zao tu inaonyesha hawaelewi kazi ya mbunge na kazi ya bunge

Hii ni fedhea kukidhalilisha chama cha mapinduzi,Watu wanakiabisha chama

Kwa hiyo ukiondoa wale wahamihaji toka chadema na wajenga hoja toka chadema,Chamani tumebaki na steve Nyerere na Mpoki comedian kweli?

Hivi Mpoki na Steve wanaweza chambua vifungu vya sheria bungeni?

Kuna kitu hakipo sawa chamani,Sasa mbumbumbu na wasiojielewa wa
megeuza chama sehemu ya maonyesho na kuvaa nguo za kijani,

Hii ni aibu kuu
Nasema wamekidhalilisha chama

Watembea nusu uchi,na wavaa hovyo wote wanatia nia ccm kweli?

Wazinzi na makahaba wamo

Matapeli na wasanii wasio na kazi maalum wamo

Hii ni aibu kuu
Heri wewe umesema...
 
Congratulations Bi Happiness, InshaAllah utafanikiwa na utashinda.

Jamaani huyu ni mwenzetu, tusimvunje nia, tusimjengee mizingwe na unafiki. Tumuunge mkono tumjengee moyo, tumpe ushauri mzuri, hebu tuungani tumpate mbunge mwana JF nwenzetu amabye atakwenda bungeni na siasa mbadala za kuwaunganisha wananchi na kuzifanya siasa za vyama vingi siasa zenye afya na upendo.
 
Back
Top Bottom