TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

Kwa kuwa Mungu ndiye aliyeleta Uhai na kwa vile ndiye mtwaa uhai,basi nimtakie Dena Amsi pumziko la milele! Nichukue fursa hii kuwapa pole ndugu,jamaa,marafiki walioguswa kwa anmna moja ama nyingine na msiba wa mwnajamii mwenzetu!
 
Ni habari za kusikitisha kwa familia ya JamiiForums kwa ujumla wake.

Inadaiwa marehemu Dena Amsi amefariki jana baada ya kuugua kwa siku kadhaa.

Taarifa za kina juu ya nini kilitokea na msiba upo wapi zitafuatia.

Mwenyezi Mungu amsamehe dhambi zake na kumjalia pumziko la milele.

R.I.P Dena Amsi
R I P
Weka picha yake
 
Msiba upo Bunju na wanatarajia kuzika leo. RIP Dena Amsi
Mlioko Dar mtufikishie salamu zetu za pole.... Utaratibu wa kutuma rambi rambi ukoje?

Miss you sana Belinda Jacob, msiba huu umewaibua members wengi sana waliokuwa wamepotea
 
Bwana Ametoa na Bwana Ametwa, Jina la Bwana Lihimidiwe!!

R.I.P Dena.
 
Dena Alale Pema Peponi.... Tutamkumbuka Sana... Michango yake ilipungua humu kumbe Masikini alikuwa Anaugua.. May God aiweke Roho ya Marehemu pahali pema panapostahili...
 
Ukifa huna tamanio.
Kama unabisha jaribu kufa uone kama jamaa hawatakufukia fasta (najua hupendi kufukiwa)

Iwekwe picha yake, hakuna atakayemshtaki kwa michango yake enzi za uhai wake.
Mkuu kama yeye alipokuwa hai hakuweka picha yake halisi sidhani kama ni busara mtu yeyote aweke bila idhini yake.Ukitaka kujua ni ngumu ebu mkuu wewe weka picha yako halisi.
 
Ukifa huna tamanio.
Kama unabisha jaribu kufa uone kama jamaa hawatakufukia fasta (najua hupendi kufukiwa)

Iwekwe picha yake, hakuna atakayemshtaki kwa michango yake enzi za uhai wake.
Mkuu nilitegemea utanielewa haraka lakini naona bado.Jiulize kwanini kuna "verified user" kwani wewe,mimi na yule siyo verified user?
Je unajua mtu si mwili bali ni nafsi yake ya ndani,mtu anapokufa ni roho inatengana na mwili lakini nafsi yake inaishi,kwa lugha nyepesi mwili viungo vyake muhimu kama ubongo na moyo vinakuwa havifanyi kazi lakini roho na nafsi zipo hai.Zinaenda wapi? ndiko huko wengine wanasema zi rest in peace.
 
Najiuliza siku nikifa nani atawapa taatifa maana hakuna mtu hata mmoja anayenijua.

Inabidi ujitambulishe angalau kwa rafiki yako mmoja mwana jamii unaemuamini!!! Ikiwa utapatwa na jambo lolote awe tayari kutoa taarifa kwa wana jamii wenzako.

REST IN PEACE DENA.
 
Back
Top Bottom