TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

TANZIA Mwana JamiiForums mkongwe, Dena Amsi afariki dunia

Sikuhizi kuna kufahamiana kati ya memba huyu na yule

Na hasa hizi grps zimetuleta karibu zaidi. So inakua rahisi kujua kilichomsibu mwingine

R.I.P Dena... Pole kwa ndugu,jamaa na marafiki kwa kumpoteza mpendwa wetu
Wewe mbona hujuani na mimi [emoji15] [emoji15]
 
Sijakulazimisha kutelezea wasifu wa ndugu yetu Marehemu, ila kila mtu anaweza kumuelezea kwa jinsi anavyomfahamu sio kuleta hapa mawazo mfu eti tusiseme au kueleza wasifu wa ndugu Dena Amsi kwa sababu alitumia Fake ID hapa JF!!.

Akina Oscar Kambona, Bibi Titi Mohamed, John Okello, Omari Makunganya, Chief Mkwawa wasifu wao ungefichwa leo hii watu tungeliwafahamu kweli?


Acha mawazo mfu wewe!!!
Uko sawa mkuu, Kutumia ID fake haiondoi ukweli.
 
R.I.P dada DA...

mbele yake nyuma yetu

raha ya milele umpe ee BWANA na Mwanga wa milele umuangazie, marehemu apumzike kwa amani
 
naomba kama kuna mtu ananyuzi zake tatu hv au zaidi anisaidie

nashukuru
 
Kwao na Dena Amse night Bunju A au Bunju Shule. ..

Ukifika Bunju A ulizia wapi ilipo Baa Juleva

Nyumbani kwao ni opposite na hiyo Baa.

Msiba upo hapo. . Baba yake anaitwa Mwalimu Komba

Sina details nyingine maana nipo nje ya Dar
asante kwa info... R.I.P Dena...doooh this life I lead
 
Mungu ampumzishe salama.Sikuwai kumuona physically ni michango yake tu,kweli kaniskitisha.
 
Back
Top Bottom