Mwanafunzi Esther wa Panda Hill aliyepotea kwa siku 35 amepatikana, yadaiwa alitoroshwa na mchoma mkaa

Mwanafunzi Esther wa Panda Hill aliyepotea kwa siku 35 amepatikana, yadaiwa alitoroshwa na mchoma mkaa

hii shule ni ya roman catholic asilimia 80 ya watoto wanasoma hapa ni wakishua haswaaa naishi kama umbali wa mita 200 hivi ilipo shule hii na nasikia hata ridiwani msoga alisoma hapa na yeye alisumbua knoma ruka sana fence
Kibaha enzi hizo kuna mtoto wa KJ alikuwa anamiliki simu kaliii balaaa hata waalimu hawanaa.. anaenda club wanalewaaa wakirudi kelele kama zoteee..!! Aisee mtoto wa mkubwa kumhandle kama hajielewa ni balaaaaa...
 
Kwa binti WA umri huyo anaakili kabisa. Ni MTU mzima.
Kuna Binti akipotea zaidi ya miezi mitatu, alikuwa kidato cha tatu, Baba yake kuhangaika weeh! Polisi wakamuambia wanafuatilia. Ikaja kubainika kawekwa kinyumba na Mjeda mmoja mtaa wa Saba Huko.
Binti kadinda ATI mjeda(Mchumba wake) asichukuliwe hatua yoyote ya kisheria na kinidhamu. Vinginevyo atajidhuru. Kwa Akili za Yule Binti(kwani pia ninamjua) kila MTU alikuwa anaelewa nini angekifanya. Wakaachwa.
Binti alirudi baadaye akaenda kufanya paper (alikuwa akisoma hizi shule za kayumba). Akamaliza shule.
[emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]Yani dyudyu ikawanogeaa wanachanganyikiwaa kabisaa akili huwa zinarukaaaa...
 
Hatimaye Ester Noah Mwanyiru mwanafunzi wa sekondari ya Pandahill aliyetoweka 18 May 2023 amepatikana.

Taarifa iliyotolewa na mama yake mzazi inaeleza amepatikana wilayani Mbalizi kwa mama fundi cherehani. Alibadili jina kuwa Erica na amekua akivaa Hijab inayofunika uso, na kuacha macho tu na hivyo kuwa ngumu kutambulika.

Chanzo cha kupatikana ni baada ya binti mmoja wa Mbalizi kusimuliwa kisa cha Ester na kudai amemuona kwa mama mmoja fundi cherehani. Leo asubuhi polisi wamevamia nyumba ya mama huyo na kumkuta Ester. Wote wawili wapo kituo cha Polisi Mbalizi kutoa maelezo.

#MyTake:
Simulizi ya kupotea kwa Ester na kupatikana kwake inaacha maswali mengi kuliko majibu.

1. Ester alitoroka shuleni baada ya kukutwa akifanya udanganyifu kwenye mtihani. Akachapwa viboko vitatu, kisha akapewa mtihani mwingine afanye. Lakini polisi walipoenda shuleni hakukua na mtihani wowote Ester aliofanya. Je mitihani yake ilienda wapi?

2. Shule ya Pandahill ina ukuta (fence) ya urefu wamita 3 na juu kuna nyaya za umeme. Inawezekanaje mtoto wa kike kuruka ukuta wa mita 3 wenye umeme?

3. Matron wa shule anasema Ester alitoroka na mwenzie mmoja na walikimbizwa hawakupatikana. Hata hivyo "rall call" ilipofanyika wanafunzi wote walikuwepo isipokua Ester tu. Je huyo aliyekimbia na Ester akiwa kwenye sare za shule ni nani?

4. Barua aliyoacha Ester alidai kuonewa na Mwalimu Jimmy, japo hakutaja uonevu huo. Kwanini hakwenda nyumbani kuwaeleza wazazi badala ya kukimbilia Mbalizi?

5. Kwanini Headmaster alienda kwa wazazi wa Ester kutoa pole?

6. Huyo mama wa Mbalizi aliwezaje kumpokea binti asiyemfahamu na kukaa nae comfortably?

7. Aliishi kwa huyo mama kama nani? Housegirl au?

8. Inaelezwa alienda kwa huyo mama na Hijab. Aliipata wapi? Sare za shule alizototoka nazo aliziacha wapi?

9. Alibadili jina kuwa Erica lakini akavaa Hijab. Huyo mama hakujiuliza iweje mtoto wa Kikristo kuvaa Hijab?

10. Binti aliyetoa taarifa kuwa amemuona Ester Mbalizi alimtambuaje ikiwa alivaa Hijab ya kufunika uso na kubakiza macho tu?

NB: Tunamshukuru Mungu Ester amepatikana akiwa mzima, lakini kwa kuwa suala hili limepaziwa sauti na umma, basi ni vema umma ukapewa majibu ya kuridhisha.!
Kule facebook kwenye page ya askofu mwamakula niliwaambia watu wasijisumbue sana yule ni binti mkubwa huenda yupo kwa msela anapika na kupakuwa.....watu walinishukia kama mwewe
 
Walimu wanakazii sana kizazii hiki,shule ni nidhamu watoto wenyewe ndo Hawa....Mwalimu ukitaka wakae kwenye mstari wanakupa kesi ya kuwalaaa....utahahaaa.
 
Huyu inaonekana alishakuwa
#UPDATES Mwanafunzi Ester Noah Mwanyilu, amepatikana katika chumba cha kupanga cha Mama Abdul kilichopo maeneo ya Ifisi Mbalizi, na kwamba alipelekwa hapo na muuza mkaa aitwaye Baba Jose na kusema ni mke wake hivyo anaomba hifadhi baada ya siku mbili angemchukua ili wakaishi wote.

Aidha vipimo vyote vya kiafya vimefanyika na Ester hana ujauzito na hivyo ataendelea kukaa na maafisa ustawi wa jamii ili kumsaidia kumpa ushauri wa kisaikolojia arudi shule, na mwanaume huyo atasakwa mpaka akamatwe.

RC Homera ametoa rai kwa walimu wa Pandahill kupunguza kasi ya kuchapa viboko.

#MwanafunziApatikana
#EastAfricaTV
Huyu inaonekana alishakuwa mhuni muda mrefu, angalia alivyonyoa nywele, kiduku, hiyo shule inaruhusuje huo mnyoo au mambo ya kubembeleza ada? Ila sazingine waziri mkuu uwe na subra, mambo haya yalikuwa siyo size yako, unaona sasa unaishia kuaibika.
 
Back
Top Bottom