Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango Kanda ya Ziwa akamatwa kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu

Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango Kanda ya Ziwa akamatwa kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
JESHI la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kanda ya Ziwa, Elias Anania (20) kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu kupitia kundi sogozi la WhatsApp.

Inadaiwa mwanafunzi huyo amewataka wenzake kununua petroli na kuchoma askari polisi wenye sare popote watakakokutana nao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, alidai kuwa mbali na kuhamasisha askari kuchomwa moto, pia aliwataka wachome moto watumishi wa umma.

Alisema kijana huyo anadaiwa kusambaza ujumbe katika kundi hilo, akishawishi wenzake kununua petroli na vibiriti kushambulia askari wa jeshi hilo.

"Anashikiliwa kwa tuhuma za uchochezi, katika kuhamasisha hivyo, alidai kuwa vijana wamechoka, hivyo anawahimiza kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya maslahi yao na kudai haki zao za msingi," alisema.

Kamanda Mutafungwa alisema mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

NIPASHE
 
JESHI la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kanda ya Ziwa, Elias Anania (20) kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu kupitia kundi sogozi la WhatsApp.

Inadaiwa mwanafunzi huyo amewataka wenzake kununua petroli na kuchoma askari polisi wenye sare popote watakakokutana nao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, alidai kuwa mbali na kuhamasisha askari kuchomwa moto, pia aliwataka wachome moto watumishi wa umma.

Alisema kijana huyo anadaiwa kusambaza ujumbe katika kundi hilo, akishawishi wenzake kununua petroli na vibiriti kushambulia askari wa jeshi hilo.

"Anashikiliwa kwa tuhuma za uchochezi, katika kuhamasisha hivyo, alidai kuwa vijana wamechoka, hivyo anawahimiza kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya maslahi yao na kudai haki zao za msingi," alisema.

Kamanda Mutafungwa alisema mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

NIPASHE
Ila yule Askari Fatuma Kigondo aliyekula njama ya kumfanyia udhalilishaji yule binti wa Yombo siyo mhalifu????????
 
JESHI la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kanda ya Ziwa, Elias Anania (20) kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu kupitia kundi sogozi la WhatsApp.

Inadaiwa mwanafunzi huyo amewataka wenzake kununua petroli na kuchoma askari polisi wenye sare popote watakakokutana nao.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, alidai kuwa mbali na kuhamasisha askari kuchomwa moto, pia aliwataka wachome moto watumishi wa umma.

Alisema kijana huyo anadaiwa kusambaza ujumbe katika kundi hilo, akishawishi wenzake kununua petroli na vibiriti kushambulia askari wa jeshi hilo.

"Anashikiliwa kwa tuhuma za uchochezi, katika kuhamasisha hivyo, alidai kuwa vijana wamechoka, hivyo anawahimiza kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya maslahi yao na kudai haki zao za msingi," alisema.

Kamanda Mutafungwa alisema mtuhumiwa huyo anaendelea kuhojiwa na uchunguzi utakapokamilika atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

NIPASHE

Kwani bangi, ugaidi au kukutwa na silaha au hii, ipi ni rahisi kumbambikizia mtu?

Kwa hawa wambambikiziaji wabobezi, lipi lisilowezekana?
 
Kama wana akili timamu inabidi wajiulize kwa nini hadi kijana mdogo namna hiyo anawachukia kiasi hicho
Miaka 20 sio kijana mdogo

Vijana wadogo ni chini ya miaka 18

Salim Ahmed Salim aliteuliwa kuwa balozi wa Tanzania misri akiwa na miaka 19
 
Sipati picha kijana anapitia nn ktk hayo mahojiano, muhimu awe mzima.
Wasi msativaa jamaniii, [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Upelekwa shule kusoma umeacha kufanya kilichokupeleka mwaza umeadapt hasira za watu wakanda ya ziwa mwanakulitafuta kalipata
 
Tatizo la copy and paste Gen Z ya Kenya walikuwa hawatumii watsapp
group hilo analo atakoma

Watsappp groups usalama wa taifa kama wote wa umri wake wanaoandaliwa kufanya kazi usalama wa taifa wengine wana ajira tayari toka sekondari walikokuwa recruited na maafisa usalama wa taifa walimu wa kawaida au walimu wakuu baada ya kuwaona wanafaa

Magroup ya WhatsApp yamejaa usalama wa taifa yote tu

Ukipost chochote tishio kwa nchi jiandae kudakwa wala sio siri
 
Back
Top Bottom