Mwanamke akutwa mtupu akiwa ameuawa Shinyanga

Mwanamke akutwa mtupu akiwa ameuawa Shinyanga

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Lucia Michael maarufu Mama Kulwa, mkazi wa Majengo Manispaa ya Shinyanga, amekutwa ameuwa na watu wasiojulikana, na mwili wake kutupwa nyuma ya Msikiti wa Majengo.

1626099822358.png

Picha: Polisi wakichukua mwili wa Marehemu

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo, ambapo aligundulika na majirani majira ya saa 12 asubuhi, mara baada ya kuuona mwili wake ukiwa nyuma ya Msikiti wa Majengo jirani na makazi yao akiwa mtupu.

Akielezea tukio hilo mmoja wa majirani ulipokutwa mwili huo, Anastazia Amosi, amesema baada ya kupata taarifa, alifika eneo la tukio na kumkuta jirani yake akiwa mtupu huku akiwa amefariki, ndipo wakamfunika nguo na kutoa taarifa kwa mwenyekiti wa mtaa.
"Mwanamke huyu ni jirani yetu ana watoto watatu, na kazi yake ni msusi maarufu sana hapa mtaani kwetu, tunasikitika sana kumkuta akiwa ameuawa tena kavuliwa nguo zote," amesema Amosi.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Manispaa ya Shinyanga, Iddi Bwana, amesema mwanamke huyo huenda aliuawa na vibaka, sababu pulukushani zilianzia kwenye vichochoro, na kisha mwili wake kutupwa nyuma ya msikiti jirani na makazi ya watu.

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, George Kyando, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kubainisha kuwa jeshi bado linafanya uchunguzi ili kubaini chanzo chake na wahusika.
 
Kanda ya Ziwa punguzeni mauaji, Tanzania ni kisiwa cha amani kwanini kila siku nyinyi tu?
 
Kwa Shinyanga ndani ya kipindi kisichozidi miaka 2 tukio la aina hii ni la nne au la tano lilitokea Ndala, Ibinzamata, Ngokolo, Ndembezi na sasa Majengo!
 
Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Manispaa ya Shinyanga, Iddi Bwana, amesema mwanamke huyo huenda aliuawa na vibaka, sababu pulukushani zilianzia kwenye vichochoro, na kisha mwili wake kutupwa nyuma ya msikiti jirani na makazi ya watu.
Kuna mtu anajiita waziri wa home matters anajidadavua kuwa crimes zimedhibitiwa
 
Nashauri jeshi la polisi wangekua wanaleta mirejesho ya hizi kesi. Ili watu wawe na imani na jeshi la polisi, Tunatangaziwa mauaji mengi mengi ila miendelezo hakuna. Kuna tatizo kwa waandishi wetu wa habari na jeshi letu kwenye utoaji wa taarifa.
Hawa watu wanauana inawezekana ni vile tu mtu anahisi haki kwenye vyomb vya sheria hakuna.

Apumzike kwa amani mama watatu.
 
Kwa Shinyanga ndani ya kipindi kisichozidi miaka 2 tukio la aina hii ni la nne au la tano lilitokea Ndala, Ibinzamata, Ngokolo, Ndembezi na sasa Majengo!
Una uhakika na unachokisema mkuu?
 
Back
Top Bottom