Mwanamke anayechepuka ni hatari kwa uhai wa mume wake kuliko hata wauaji wa kutumia silaha

Mwanamke anayechepuka ni hatari kwa uhai wa mume wake kuliko hata wauaji wa kutumia silaha

Hata sisi tukichepuka bado tunakuwa na mapenzi nanyi jamani, ndio maana huwa hatuhamii kwa michepuko na watoto tukizaa mnalea nyie waume zetu. Ikijulikana basi mtusamehe tu tuendelee kusongesha maisha.
Duh! [emoji21] [emoji21]
 
Wanaume mngekuwa mnaweka angalau robo ya hizi nguvu mnazitumia kuzini kwenye mambo ya familia hii nchi ingekuwa mbali saaana. Kama wewe ni mtu mzima mwenye mke na watoto na unachagua kuenda kulala na mwanamke asie wako, na wewe unastahili kumegewa. What goes around comes back around.

Tulieni ! Kama unajijua huwezi kujizuia basi usioe kabisa.

Anaanza kwa kusema......"Mwanaume anaweza kuchepuka na bado akawa na upendo wa dhati kwa mke wake lakini mwanamke hawezi kuchepuka na akaendelea kumpenda mume wake kwa dhati.Nasema hivi kwasababu mwanaume hafanyi tendo la ndoa kwa hisia, mwanamke hawezi kufanya tendo la ndoa bila hisia mguso.Ndiyo maana wanaume wanahitaji mahali pa kufanya tendo la ndoa ila wanawake wanahitaji sababu ya kufanya tendo la ndoa.

Wanawake wengi wanaoenda mahakamani kudai talaka kwa waume zao ni wale wachepukaji,mwanamke asiyechepuka hawezi kwenda mahakamani kudai talaka isipokuwa kama mumewe atakuwa amezidisha unyanyasaji wa kimwili na kiakili kiwango cha kukaribia kumuua mkewe.

Wanaume hawawezi kubadili tendo la ndoa na upendo.Mwanaume anaweza kufanya tendo la ndoa na mwanamke lakini bado akawa hampendi-ndiyo maana wanawake wanaojikuta kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanaume waliooa wanaowapenda wake zao kwa dhati hupata tabu saana kupata kufurahia mahusiano hayo kwani huwa wanatumika tu na hao wanaume wenye ndoa zao. Lakini pindi tu mwanamke aliyeolewa anapolala na mchepuko wake huanza hata kusimulia habari za siri kuhusu mume wake na anaweza pia kusema ni kwa namna gani anamchukia mume wake anaweza hata kukubali kuchukua sumu kwa mchepuko wake ili amwangamize mume wake.

Kwa mwanaume tendo la ndoa na upendo ni vitu viwili tofauti kabisa,lakini kwa mwanamke tendo la ndoa na upendo ni vitu viwili vinavyoenda sambamba.Kwa mwanaume tendo la ndoa huja kwanza kabla ya upendo (matamanio) lakini kwa mwanamke upendo huja kwanza kabla ya tendo la ndoa (upendo wa dhati); kwahiyo pindi mkeo anapoanza kuchepuka upendo wake huhama kutoka kwako kwenda kwa mchepuko, anaweza hata kuanza kumpa chakula kizuri na mahaba ambavyo amekuwa akikupa wewe tu.

Mwanaume kuchepuka haimaanishi kuwa ameacha kumpenda mkewe la hasha!, ila siwezisema hivyo kwa upande wa mwanamke.Pindi mwanamke anapoanza kuchepuka anakuwa ametumbukia kimapenzi kwa mchepuko huo na maisha kwenye ndoa hayawezi kuwa sawa kamwe; na anaweza hata kumuua mmewe endapo tu atakuwa ameanza kuchepuka.

Mkeo akianza kuchepuka utakuwa mwanaume mwenye bahati sana endapo hautakufa ndani ya miaka 10.Tafiti zinaonesha kuwa 95% ya wanawake wanaochepuka huwaombea waume zao wafe haraka, ndiyo maana ni hatari sana kwa mwanaume kuendelea kuishi na mwanamke anaechepuka; vilevile ndiyo maana inashauriwa kila mahali hata kwenye Biblia kumtaliki mwanamke pindi tu anapogundulika kuwa amezini(amechepuka).

Mwanamke anaechepuka ni hatari kwa uhai wa mume wake kuliko hata wauwaji au silaha.Kuna wanawake wengi wachepukaji duniani hualika wauwaji usiku waje watoe uhai wa waume zao na askari hata ndugu wa mume hawawezi kugundua hilo kwani msibani huyo mwanamke atakuwa analia kwa uchungu wa kuigiza na kuficha maasi yake.Ndiyo maana wanasaikolojia hukataza sana mwanamke kuchepuka kuliko mwanaume.Wanawake hawawezi kuhimili mitafaruku ya kihisia itokanayo na kuchepuka; ndiyo sababu wanaume watafiti na wenye uelewa mkubwa watajua tu kuwa mkewe ameanza kuchepuka kwasababu huanza kumdharau mmewe na hujaribu hata kumnyima mumewe tendo la ndoa kwa visingizio lukuki.

Tafiti zinaonesha kuwa 90% ya wanawake wanaochepuka hawafurahii tendo la ndoa na waume zao hapo mwanaume makini atagundua tu hasa tabia za mkewe zitakapobadilika kuhusiana na tendo la ndoa, lakini mwanaume zube hawezi kugundua hili ataendelea kuvumilia sababu dhaifu za kunyimwa unyumba mpaka atakapoondolewa duniani.

Mwanamke hawezi kuchepuka na mtu ambae hampendi, huwa wanaitoa mioyo yao kwa kila kitu, ndiyo maana huwezi kuamini maamuzi yao.Kichekesho kikitolewa wanawake wengi wanaocheka hawacheki eti kwa sababu kichekesho ni kizuri ila ni kwasababu huwapenda wale waliotoa vichekesho hivyo; na endapo hawakupendi hata kichekesho chako kingekuwa kizuri kwa kiasi gani hawatacheka, ila mwanaume akicheka kuhusu kichekesho fulani ni kwasababu kichekesho chenyewe ni kizuri lakini si kwasababu eti anampenda mchekeshaji hii ni kwasababu wanaume wana uwezo wa kukabili hisia.

Tafiti zinaonesha kuwa ndoa nyingi huanza kuyumba pindi mwanamke anapoanza kuchepuka.Kuna wanaume wengi wanaochepuka lakini bado wanawaonesha wake zao upendo wa dhati, ila ni vigumu kukuta ndoa imesimama na mambo yanaenda sawa huku mwanamke akiwa mchepukaji.Ninarudia, karibia 100% ya wanawake wanaochepuka huwaombea waume zao wafe haraka au hulazimisha talaka ili wawe na uhuru wa kufurahia penzi la kwenye mchepuko, ila wanaume wengi hawawezi kuruhusu wake zao wa ndoa wanyanyaswe ama kwa vitendo au kwa maneno na michepuko yao, siku zote wanaume husimama upande wa wake zao.Mwanaume anaweza kuchepuka na bado akampenda mkewe lakini mwanamke hawezi kuchepuka na bado akampenda mmewe.
 
Bila sisi kuwepo mtachepuka na nani? Mbwa???
Hoja ni kuwa Mwanamke akichepuka anakuwa from that day anakuwa hana heshima kwa Mume wake tena na upendo hupotea kabisa yaani inabaki kuishi kwa mazoe.. Unajua Mnachangia kwa mihemuko tu.. Hakuna aliyesema kuwa mkichepuka sijui mnafanya na nani.. The issues is Matokeo yanayokuwepo baada ya Mwanamke kuchepuka kinamdadilisha kutoka kwenye utu na kuwa Mtu mwenye malipizo kwa Mume wako... Na kumbuka tofautisha Mwanamke anayemsaliti Mume wake na Mwanamke anayemsaliti Mchepuko wake. Mleta mada ameongelea Watu wenye Mahusiano ya Mme na Mke.. Msije changanya maada hapa sawa Mchepukaji demi
 
kwahyo sie hatuumii eh
Ndiyo maana nikasema ''hakuna kitu kinachoumiza km usaliti''
Usaliti una umiza kote kote haimaanishi ww ni jinsia gani.
Ili utengeneze ndoa yenye furaha na amani vitu km usaliti, chuki, hasira n.k visiwepo.
-Ukimwaga mboga nakula ugali maana yake mtu anayekusaliti mpe uhuru (Mwache aende). Tafuta mwingine jenga naye familia.
-ukisema akimwaga mboga namwaga ugali sasa hapo (mtabaki na njaa wote)mnakaribisha magonjwa
Siyo watu wote ni wasaliti kwenye mapenzi kuna watu wema kbsa ambao ukikutana nao hautaweza kuamini.
 
Ndiyo maana nikasema ''hakuna kitu kinachoumiza km usaliti''
Usaliti una umiza kote kote haimaanishi ww ni jinsia gani.
Ili utengeneze ndoa yenye furaha na amani vitu km usaliti, chuki, hasira n.k visiwepo.
-Ukimwaga mboga nakula ugali maana yake mtu anayekusaliti mpe uhuru (Mwache aende). Tafuta mwingine jenga naye familia.
-ukisema akimwaga mboga namwaga ugali sasa hapo (mtabaki na njaa wote)mnakaribisha magonjwa
Siyo watu wote ni wasaliti kwenye mapenzi kuna watu wema kbsa ambao ukikutana nao hautaweza kuamini.


ni sawa usemayo !
 
Yaan tunda unalonipa mm then unaenda kumpa boy mwenzangu, zile style zote unazonipa unaenda kumpa pia na mchepuko, Aaaaah ngumu kumeza aisee.
Inshort Dada zangu msitufanyie hayo pls
Akimnyima baadhi ya style kuchepuka hakuumizi au unamaanisha nini?
 
  • Thanks
Reactions: ovi
Kwani mwanamke akichepuka anatembea au anafanya mwenyewe.Wanaume bwana wakiamua kujihalalishia udume wao huja n nyuzi Kama hizi.Wewe unafanya Nini mpaka mke wako achepuke?lazima unashida Tena kubwa Sana na Tena Bora ufe Basi kwa sababu umepunguza uwezo was kuitwa mwanamme.Kwendeni huko
Mimi nashangaa hawa wanaume wapumbuvu sana eti wanazuia wanawake kujipa raha na michepuko yao kama hawawezi ndoa zenye michepuko si wakae bila kuoa ili wanaume wanaokubali wake zao kuchepuka waendelee kufaidi maisha ya ndoa.
 
  • Thanks
Reactions: ovi
Back
Top Bottom