Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kuna kitu mtu kanikumbusha, huyo Zahir Zorro nimesoma nae Primary Dar. Nilimsahau kabisa. Alikuwa darasa moja nyuma yetu, Kisarawe Primary School.Mzee wangu Slay Shaggy,,,jina lake kamili ni Abdulkareem Al Majid,,,,,,chotara wa kiarabu na rafiki wa karibu sana wa uncle Zahir zorro!!
Mzee wake Majid alikua mwarabu wa kutokea Sana'a Yemen...na mama yake alikua manyema wa tabora..
Mzee majid alikua hakai kkoo,,mda mwingi Sanaa Yemen ila familia yake ndio ilikua inakaa,,kule nyuma ya lile jengo ambalo baadae likikuja kua fire station mpaka leo,,,,,pale opposite na iliyokua baadae jangwani sec school.
Slay Shaggy na uncle Zahir zorro moja wa mabishoo wavaa nguo nzuri nzuri miaka hiyo ya 1960,s na 1974,s alipoondoka Tanzania na kwenda Sana'a kutafuta maisha zaidi!!
Nadhani miaka hiyo ya 1962 mpaka 1974 ulikua bado mdogo sana ww,,upo chekechea
Huu ni UBUYU DISCRIMINATION.. Mmabagua wa kuweka mafaili yao hakuna cha heshima, una faili weka nasi tujue chui wenye ngozi ya kondooHuyo Maza nampenda sana huwa naogopa hata kumsema ila sio msafi kihivyo, nae ana mengi chungu tele.
Tumsitiri Mkuu.
Code hakuna hapo ni Simbachamwene bora Ungesema "Ras Simba " ingekuwa SawaDALALI SALMA JR,,,,, SIO HUYU WA MGANGA MIKUFU ...
USHAMJUA MH LION CHA.......????
MZEE WA THREESOME,,,,
WAZEE WA HOTEL VIP TUNAJUANA🤣🤣🤣
Si angemquote hata faiza jamani 😅😅😅😅 wapambaneNa amekuonea masikini katuacha sisi tunaozogoa umbea hapa kakuquote wewe.
Pole
Kuna kitu mtu kanikumbusha, huyo Zahir Zorro nimesoma nae Primary Dar. Nilimsahau kabisa. Alikuwa darasa moja nyuma yetu, Kisarawe Primary School.
Huyo Shagy hatujamfahamu wote, AbdulKareem tuliowafahamu ni kama nilivyokueleza juu hao, na anaefanana na jina Shagy, ni Shedi Sheni, mtoto w gerezani huyu alikuwa anapiga organ, Mwenyezi Mungu amrehem.
Kuna mtu mwingine nyumba uliyoitaja alikuwa akiitwa Hamza. Halafu wengine tuliwajuwa ni kina marehem Jerry Riyami, hao wote tukijuwana sana utotoni, mtaa huo huo lakini kama unarudi kwenda shule ya Zanaki.
Siku nikimpata au nikimbuka ntakujulisha lakini mpaka sasa piucha yake haiji kabisa katika watu niliowafahamu enzi hizo mitaa hiyo.
Ukitoka nyumba hiyo unayoisema ukienda kama unaelekea Muhumbili kulikuwa kina Bate, ndugu watatu mabaharia na baba yao alikuwa Captain wa meli. Nadhani wanaishi Australia hivi sasa kasoro mmoja nilikuwa naonana nae Kariakoo, anaitwa Othman, wenhine ni Farouq na Mustafa. hawa ni mitaa hiyo unayosema na walikuwa hawatoki hiyo nyumba, walikuwa na kijiwe chao kinaitwa Black September.
Shosti angu faiza umekula maisha iaseeh,yaelekea ulikuwa mrembo Sana🤣hongera kwa umri na bata ulilokula enzi hizoUmekazana "ulikuwa mdogo, ulikuwa mdogo", Huyo mzee wako simfahamu, nyumba ile pale unayoisema watu wote nawafahamu sana wa miaka hiyo. Hiyo nyumba inatazamana na kiwanja nilichokuwa nakwenda kucheza netball enzi hizo.
Nyumba ya nyuma ya fire naifahamu miaka hiyo, mwenyewe anaitwa Ahmed Masoud na ndiye pia alikuwa na Petrol station opposite na fire station. Na yeye huyu alikuwa Myemen, alipoondoka aliwaachia akina Akrabi, hawa walitokea Mwanza, na hapo pakawa miaka hiyo ya 70 panaitwa Black September, nawakumbuka vijana wote wa pale. Wengine waliotangulia Mwenyezi Mungu awarehem.
Miaka hiyo mimi nakwenda Disco Africana na Bahari beach, kijana mbichi. Kama alikuwa rafiki yake ni Zahir Zorro huyo siwezi kumfahamu, madensi yao yalikuwa ya kishamba, sisi watoto wa Kariakoo tulikuwa na hadhi, tunakwenda sehemu za heshima yake na family zetu.
Lakini ntawauliza wazee wenzangu wa zamani labda watamkumbuka watanielekeza vizuri.
Mpaka sasa watu wa enzi hizo Waarabu wanaoitwa Abdul Kareem nimewakumbuka wawili, mmoja ni cousin wake huyu Naibu Spika wa bunge Azzan Zungu, huyu alikuwa anakaa mtaa wa Amani Kariakoo. mwengine alikuwa anaitwa Abdul Kareem macho ya paka, huyu alikuwa mkubwa sana kwetu, huyu ni mbulushi, siyo Mwarabu, jamaa yzake kina Rostam Aziz. Huyu alikuwa Kariakoo Aggrey lakini akipita sana huo mtaa unaosema alikuwa na ndugu zake kule mbele mtaa wa Mindu.
Anyway umenipa homework, ngoja niifanyie kazi. Umenikumbusha mbali sana kijana. Mwaka huo wa 1974 mimi nimeondoka Tanzania kuelekea ughaibuni., December 9 naikumbuka.
Almasi?Nipo kisangani...nikirudi bongo...nakuletea uzi kamili wa mdau anaekula cocaine first grade...
Wamemgeuza teja ili wapige hela zake kirahisi....
Afu ni mchicha mwiba pia..
ASILIMIA 35% YA WABANA PUA NI MCHICHA MWIBA...
Kwa jinsi anavyomuongelea sio yeye, halafu ingekuwa ndio yeye unafikiri angekuja hapa?Kuna vijana wanapiga hesabu hapa muda ambao bi Salma yuko nyuma ya nondo ndio muda ambao ulipotea jukwaani.. Alivyotoka nawe ukarudi kwa kasi ya 5G..
Nawasilisha....
Atakuwa toto la kimanga, shomboshombe flani hivi kama Fatma Karume.Shosti angu faiza umekula maisha iaseeh,yaelekea ulikuwa mrembo Sana🤣hongera kwa umri na bata ulilokula enzi hizo
Saivi naona unashinda ndani tu,ukila,ukichat na kutumia penshen yako taratibuuu.
Fatma Karume ni mdogo sana kwangu. Fikiri ikiwa Zahir Zorro alikuwa darasa moja nyuma kwangu, primary school. Babake banana Zorro ndiyo rika langu.Atakuwa toto la kimanga, shomboshombe flani hivi kama Fatma Karume.
Eti FaizaFoxy wewe na Fatma ni rika moja?
Sema wengi ilikuwa kweli wapigaji. Unakuta dogo wa TPA ana beach plots zaidi hata ya 20 kwa bei ya 50m kila moja hadi unashangaa....Yule mzee kalostisha wengi sana mkuu, na kama angekuwepo mpaka leo aisee watu wengi sana wangekuwa wanaishi kama mashetani kama akivyokuwa akisema..
Salma wala sikuwa na habari kama kafungwa mpaka nilipousoma uzi huu wa Nifah.Kuna vijana wanapiga hesabu hapa muda ambao bi Salma yuko nyuma ya nondo ndio muda ambao ulipotea jukwaani.. Alivyotoka nawe ukarudi kwa kasi ya 5G..
Nawasilisha....
Basi nimepata kufahamu rika lako, Zahir nae mjanja sana mzee wa mjini yule hakubali kuzeeka mpaka leo anavaa kama kijana wa miaka 20!Fatma Karume ni mdogo sana kwangu. Fikiri ikiwa Zahir Zorro alikuwa darasa moja nyuma kwangu, primary school. Babake banana Zorro ndiyo rika langu.
Nifah kumbe hujaniona? Toto la kishombe la haja, si mchezo mchezo.Mbona picha yangu niliiweka JF.
Nikuwekee?
Nimeingia katika uchunguzi rasmi juu ya madai ya Salma kuwa huru, nitaleta majibu kama wewe ulivyofanya.Salama wala sikuwa na habari kama kafungwa mpaka nilipousoma uzi huu.
Mpaka sasa naamini alikuwa innocent, na nimethibitisha hilo kwa kujiridhisha kuwa kweli alifungwa lakini kashinda rufaa yake na kaachiwa huru.
Kupiga hesabu ndiyo maarifa, usilishwe matango na kina Nifah hapa, si kama hivyo nimepiga hesabu na imeonekana kweli alikuwa na kesi za kubambiukiwa. Na ushahidi wa kesi aliouleta Nifah post namba moja hauhusiani kabisa na kesi alizofungwa, hiyo aliyoweka attachment Nifah ni kesi ya ya madai ya mirathi.
Mpaka sasa Salma, mahakama zimeamuwa kuwa ni innocent, msimpakzie kijinga.
Hapana siyo ya kwenye avatar, niliwachia full body, vijana wakajiumize na "selfie", nyoko zao, ngunga siku hizi wanaita "selfie".Basi nimepata kufahamu rika lako, Zahir nae mjanja sana mzee wa mjini yule hakubali kuzeeka mpaka leo anavaa kama kijana wa miaka 20!
Nakumbuka uliweka picha katika Avatar yako ukasema ndio wewe, kama sivyo basi nimepitwa.
Naomba ufanye hivyo, niwekee.
Mahusiano ni kitu cha kawaida hicho, mwanamke hana mume na pesa anazo na kijana ana njaa, kibaya ni kuwa Mwanamke wa Kiislam ilitakiwa aolewe na asifanye zinaa na uasherati. Tunafundishwa zinaa inaleta umasikini, na kilichompata ni ushahidi kamili kuwa uasherati na zinaa vinaleta umasikini na ni uchafu.Nimeingia katika uchunguzi rasmi juu ya madai ya Salma kuwa huru, nitaleta majibu kama wewe ulivyofanya.
Kwa sasa naomba nisiongelee masuala ya kesi yake bali mahusiano na Cheni ambayo ndio lengo hasa la uzi huu.