bigmind
JF-Expert Member
- Oct 28, 2015
- 12,457
- 12,689
Asante shangazi nitamleta mkweo umfunde aisei..Inakuwa hivi, umesikia tetesi kuwa mume ana mchepuko, mwanaume huyu mlioana akiwa anamiliki baiskeli na anaishi kwenye chumba. Wazazi pia walimuona he is just a waste of space lakini ulimpenda sana mpaka wazazi waliruhusu ndoa.
Baada ya harusi ulitaka kuwanyamazisha midomo wale waliokuona umeolewa na apeche alolo. Zile hela za field ulishea chumba na mtu ulihakikisha zimebaki na umeweza kununu kiwanja.
Hubby nae alikupiga tough, nyumba ya nyuma imekwisha yenye vyumba vitatu vya kulala na mmezungushia fence eneo lote sasa mko kwenu.
Leo hubby amerudi asubuhi, kimekuuma umemhadithia shoga Kidawa. Shoga amekupa pole na jioni amemhadithia binamu yako Irene. Irene ameyafikisha kwa mama yako. Wote wanaona umeenda kumnufaisha huyu mwanaume.
Vikao vya familia vimeanza, wanashauri uondoke kabla hajakuletea maradhi.
Haya ni mambo ambayo mgeweza kuyamaliza wenyewe. Sasa una hasira na shost Kidawa. Kidawa angeyajuaje kama usingemwambia!
Matatizo yako shost ni pichu yako haitakiwi kuonekana na mwingine zaidi ya mume wako.
Sent using Jamii Forums mobile app