Mwanamke Kutotongozwa…. JAMANI Tatizo nini?

hahaha.... Si nilikwambia kua huyo Fatma alikua anataka? Alafu shem si kuna ile ambayo wanaume huangalia kama atapata hapo anapo papenda ama lah! Akiona kua chances are slim wala hata haangaiki kabisa! lol
Ewaaaa!

Hakuna kitu mwanaume anachoogopa kama kupigwa kibuti. Ndo maana huwa haingizi neno kama mtongozwaji mwenyewe anaonekana katia pamba sikioni....

Mwanaume anayeingia kichwa kichwa afu akalimwa kibuti basi huyo SI MWANAUME BANA!
 
Nimekuelewa Big SISY,na ni kweli huwa wanajipanga hakurupuki kwa kuogopa vya mbavu,

Ila hawa wanaume bana hata hawaeleweki unakuta hata umeongozana na mdada kavaa ile km kamkusudia mtu,
Cha kushangaza ww ambae umejivalia zako kawaida ndio unapata usumbufu yule mwezio wakishachekean pale mkapita ndio basi lkn ww mwingine ndio lijamaa linaenda kujikoki mistari anakuibukia upya!!!!

Labda hapa tuseme kuna aina za tongozo,means kuna zile za serious na zile za kupigiana makele bara baran kutokana na uvaaji wa mtu,mie hizo za makelele bara baran sikutan nazo kwa namna ya uvaaji wangu,

Mie hapa naiongelea ile ya serious ambayo haihusiani labda na kumtega mtu kimavaz,isitoshe unajikuta unatokewa hata na watu wanaokufahamu ww umeolewa au uko kwenye relation!!!
 
Ni matatizo tu ya hapa na pale ya kidunia babu lakini namshukuru Mungu niko salama............oooppsss sorry ADI kwa kuwa off topik......babu huyo
Orayt.... pole kwa matatizo. Ila hayahusiani na mitongozo wala mafumanizi, right?

Sori ADI fo zis ofutopiki, (Source: Kbd)
 

Mapenzi ya kweli sio art.... Siamini hili Ole..... Ila tu nakubalisana na hio ya kwamba they should learn the theories....lol... Kazi kweli kweli! lol

Hivi kwani lazima kutongozwa bana? Mzukie mwenyewe tu, khaa mbona mbwembwe nyingi sana!!

Kipipi sijasema ni lazima.... Na kuna raha bana mwanamke uzukiwe sio umzukie.... hawa kaka zetu hawachelewi kusema kwanza ulinitongoza mwenyewe! lol

AD,
Kumbe msipotongozwa nalo ni tatizo hata kama mnajua jibu litakuwa yes or no depending on many different issues?

lol.... Ndahani bana.... Ndio usitongozwe kabisa?? Ilo kwa kweli ni tatizo. Labda kama tayari you have your own....
 
Orayt.... pole kwa matatizo. Ila hayahusiani na mitongozo wala mafumanizi, right?

Sori ADI fo zis ofutopiki, (Source: Kbd)


Ohhh nooo! Hayahusiani kabisa. Asante, no mo off topik pls.
 
Duhhhh
Mi nimesikia na nimeona wasichana/wanawake wanatongozwa hadi usumbufu.
Sijawahi sikia mwanamke ambae hajawahi tongozwa kabisa ...



Nyie warembo msijione kua mna bahati (or call it whatever) ya kutongozwa na ukadhani wanawake wote hutongozwa hivo hivo.... Wengine wanakosa wa kuwatongoza......lol

@Dena....

Wifi hivi unafikiri ni wangapi wanatumia JF, FB na twitter katika jamii yetu? Ni wachache mno.... kutongozwa kwenye mtandao ni rahisi saana (thou haijawahi nitokea :wink2🙂; Lakini wapo wale katika jamii hapati watu wa kumtongoza.
 
Lol. . mapenzi na mahusiano dah! mapenzi yanarun dunia! sababu nyingi zinasababishwa na infriority complex ya kaka zetu! mwanamke ajifanyishe wa chini ili atongozwe? yani ingekuwa kwa mila zetu mwanamke unaweza ukaanza ingekuwa bora sana jamani!

Twande
Hapo kwenye bold hapo ni kwamba kila mtu anataka a user friend now adays si suala la kujifanyisha wa chini NO....ni hoja ya kujiweka katika a common ground level !!!!! Ukijibagua na wengi expect kubaguliwa na wengi in return, kuna ka usemi "wa matawi ya juu" haka kanawalevya wengi wake kwa waume kama dada wa matawi ya juu ni sawa na yuko busy na safari ok....ila hakuna a common grounder anayependa co-pilot...so you enjoy flights wakati wenzako wana enjoy togetherness and vice versa.....so umsubiri wa matawi ya juu mwenzako naye if it happens akiwa free ndo akupe 1 hour treat then akaendelee na mitkas yake.........coz kwa mwanaume (akishakuwa wa matawi) likely anakuwa na familia tayari.....so why the hell wasting resources for non-sense and danger??????

Unajua plug and play????? Simaanishi kuwa simplistic ila lazima ujue kucheza na biti no matter who you are othewise waweza DODA mchana kweupe ukilaumu inferior complex za wanaume kumbe watu siku hizi hawana time ya kupoteza

Hata nyimbo siku hizi zimebadilika
Zamani; Africa unite, Prison, No woman no cry, Liberia nakadhalika za kusaka uhuru
Siku hizi; Wine Gal, Hold my hand, My love is wicked, 03bone n clyde, my boo etc etc

Unakuta demu kang'ang'ana ooonh m beautiful.....atanipa nini yule.....kazi yake haitoshi hata mafuta kwa mwezi......mwanaume gani hatumii hata IseyMiyake (akimaanisha designer notes)....yaani bora plasticity tuuuuu

Plain fact ni kwamba any responsible dude with focus n plan anakuwa engaged sana na mambo ya maisha kuliko hizo chase with NO rewards....mtu hajibu salamu....anaingia kwenye lift hasalimii.....huyu ndo umfikirie kuwa partner......ukiumwa atalala hospitali huyu kukuona uki-puke akusaidie??????

Jamani ukweli ni kwamba the way you present yourself before people has a lot to tell, do and even label you!!!!!!
You btter lie low so that you get embraced (itakayopelekea kutongozwa) by all characters ili uew na mawanda mapana ya kuchagua kilicho bora kwako

KALAGA BAHO wazaramu wanasema
 
wengine nasikia huwa wanaoga mtoni saa kumi usiku maji ya bariiiiiidi kama barafu ile watongozwe
Fidel80 nadhani anajua vizuri

Condoreza una vituko wewe!! lol.... Dah! hii dawa kiboko na itabidi Fidel aieleze zaidi aisee....lol

Lol. . mapenzi na mahusiano dah! mapenzi yanarun dunia! sababu nyingi zinasababishwa na infriority complex ya kaka zetu! mwanamke ajifanyishe wa chini ili atongozwe? yani ingekuwa kwa mila zetu mwanamke unaweza ukaanza ingekuwa bora sana jamani!

hahaha.... Twande mila zina evolve ujue... Waweza jitoa muhanga na kuevolve hio mila..... lol... Ingawa in the long run lazma ikusumbue.....

Hii sredi bado inaendelea au tuianze uchakachuzi?

Sori ADI for zis schupid ofutopiki lakini inayodizevu ka-LIKE kamoja.

:iamwithstupid::iamwithstupid:

ODM mbona uchakachuzi niliona kama umeanza kitambo? lol... Have a kick off it! lol


Mie mzima na nimefurahi kukuona.... ila tu umenifurahisha ume manipulate hadi kuweza chakachua sig yangu iweze kubali maelezo.... hahahaha.....

Illa kuna mtu akikutongoza lazima urudi kijijini kufanyiwa sadaka ya kutoa nusks.... lol
 
Reactions: Kbd
Asante AD for this post. Mie langu moja tu, hivi, kutongozwa ni kitu cha kidini au? Yaani , kinakubalika kidini ?==> na hence muongozo kuwa ni lazima itoke kwa wanaume tu?
Au ni a generic term ambayo inaweza kutoka hata kwa wanawake?

Hofu yangu kubwa ni kuwa , kama ni jambo linalotakiwa kutoka upande mmoja, tiyari lina set precedence na mazingira yanayompa superiority m-gender mmoja dhidi ya mwingine.

Na hasa tukizingatia kuwa wanaume wana list yao ya 'wanavyovipenda' au kuvitamani kwa jenda hii ingine na hali kadhalika, wanawake huwa wana yao, na bado kuna vigezo-changia-kote i.e vinavyokubalika na ku feature katika list zote mbili.
Mfano, mwanaume atavutwa na umbile na sura ( asilimia kubwa, sijasema wote, kabla hamjanitovoga na bisbisi machoni), atapenda labda mwenye haya kidogo , though wengine wanapenda macho makavu, wengine wanapenda mwanamke independent ila eti awe submissive ( hapo inakuwaga ngumu kubalansisha ikwesheni ila ndo hivyo)etc.
Wanawake nao hupenda ( walio wengi) security in a man - mara nyingi hili hupimwa na juhudi ya kazi , mara nyingine pesa , na historia ya mafanikio maana hiyo pia itamu assure maisha bora ( sio wote jamani); uaminifu ( kigezo kigumu kabisa), un-mkatili ( sijui ndio mpole, au sijui nini but antonym ya mkatili- hapa nakumbuka lile tangazo la kwenye luninga la mwanaume ambaye akiingia home, hadi watoto wanajificha katika makapu) .

Lakini pia kuna vile vigezo changia kote kama uaminifu na ukweli ambavyo havina jinsia.
Na hapa natoa heshima ( pay respect, lol) to ukweli kuwa sio tongoza zote zitaishia katika ndoa. Najua zingine ni patapotea lakini sijataka kuketi ( ku base) katika utongozaji wa kihuni tu wa tamaa ( one night stands), ila zaidi katika ule utaoleta mahusiano thabiti.
Naomba kuwasilisha
 

Kwa mwanamke kutongozwa hakukwepeki hata ukijipiga kininja, atakuja ustadhi na kibaragashia atakutongoza, ukijivika sura ya kilokole, pia ataibuka mjuaji ajifanye anakufundisha neno mwisho wa siku anamwaga sera.

Kuna watu wao kazi ni kudeal na wake za watu, na wana kimsemo eti mke wa mtu hana gharama.
Kwa wanawake kutongozwa ni jambo la kawaida (sunnah) kama mnavyosema, tatizo ni kukubali kila unapotongozwa mmh hapo ndio noma kumkubalia kila mwanamme anaekutongoza.

Kingine kwa mwanamke ni type ya huyo mtongozaji kama anaendana na ww, kama utaona wanakutongoza hamuendani type hapo pia kuna question mark......!

tatizo leo j3 mikazi kibao hata kujiachia katika huu uzi inakuwa tabu.
 
Ni vizuri ukatumia lugha moja tu,(kiswahili au kingereza). kwa kuchanganya hivi wana jamii wanakuona kama Mshamba. Na huyo mwanamke mzuri asietongozwa ana mkosi unaoitwa KIMAVI.
 
Ewaaaa!

Hakuna kitu mwanaume anachoogopa kama kupigwa kibuti. Ndo maana huwa haingizi neno kama mtongozwaji mwenyewe anaonekana katia pamba sikioni....

Mwanaume anayeingia kichwa kichwa afu akalimwa kibuti basi huyo SI MWANAUME BANA!


Shem hapo in blue sio yategemea kweli? mbona your hommie enzi hizo alinitongoza mara 3 nikawa nampa za uso lakini hakukata tamaa mara ya 4 nikaingia line.... :redface: Na I know you know as I know kua ni Mwanaume hasa! lol
 


Sis naona umenipata kabisaaa..... Ninaposema tongozo ni zile genuine tongozo, sio za kulazimisha.... na kutega ni kulazimsha.... atleast that is IMO.
 
Shem hapo in blue sio yategemea kweli? mbona your hommie enzi hizo alinitongoza mara 3 nikawa nampa za uso lakini hakukata tamaa mara ya 4 nikaingia line.... :redface: Na I know you know as I know kua ni Mwanaume hasa! lol
Hehehehe.... kile kibuti chako cha staki nataka?.... Hata mi nlijua tu ulikuwa unakataa kimagumashi...
 

Hapo in blue jamani, mbona sasa mtihani.... Kujua kama ni kidini ama vipi? And then kwa jamii za kwetu hizi naamini kabisa ni vema mwanaume awe ndo mtongozaji thou Mwongozo hata kwa mwanamke hutolewa japo mara nyingi kwa vitendo.

Mandawa umezungumzia vitu ambavo huweza vutia kwa wanaume na wanawake.... Take note kua mara nyingi mwanaueme aweza pata kirahisi yule of his choice (hasa basing on muonekano) kuliko mwanamke... Wanawake mara nyingi you compromise... waona kua this is better or less ya kile nitakacho but sio mbaya....

Tongozo za kuishia ndani ya ndoa ziko wapi? lol.... Mara nyingi togozo zote huishia tu kulalana na mahusiano.... na hio ya one night stand naona haipo katika tongozo ambazo nimelenga.... hahaha...
 
Kutongoza kumepungua sana nyakati hizi...incedentally na hata wanawake wanaohitaji mpaka watongozwe (ili 'watoe mzigo' kwa mfano!:thinking🙂 pia wamepungua/wanapungua kwa kasi. I will dare to say kuwa trend ni kwa wanawake wengi zaidi kujirahisisha/kufungua milango na hivyo dhana nzima ya kutongoza inapotea. So katika mazingira haya mwanamke anayengoja mpaka atongozwe anaweza kujikuta anangoja milele! Au pengine kama alivyosema AshaDii, inawezekana ni namna tu kutongoza kumebadilika!
Ladba nitoe true story yangu moja - zipo nyingi za namna hii zilinikuta kipindi hicho (na sasa? -mmmhh wife huwa anapita humu mara kwa mara😛eep🙂:


Lakini ninachotaka kusema ni kuwa kutongoza (actively) kunapungua sana....kuna mawasiliano na makubaliano mengi yanafanyika by implications na body language tu. Kwa mfano kwa namna anavyovaa mwanamke anaweza kutoa ujumbe kwa kukusudia au bila kukusudia fulani kwa 'potentials'! ipo mifano mingi na naamini wanaume wengi humu wanaweza kuwa mashuhuda.
 
Wengine Hawatongozeki na hata ukiwatongoza watakuona kama umechanganyikiwa, Na hiyo hali kwao imezoeleka. Eti Age haina nafasi, Oh please if that the case nafikiria kumtokea Bikidude je ataniona nina akili timamu? Au atahisi zishafyatuka?
 

Pole na kazi Scofield.... Huu uzi upo bana waweza endelea kuchangia hata baadae.... Kikubwa umechangia na baadae unaweza changia tena ukipata nafasi....lol

Nimekupata... post yako, na ndio maana kuta post nimegusia kua ingawa hili la kutotongozwa lipo, sio saana kivile. Na naelewa kua kuna watu wana ma theories na formulae zote za kuweza mpata mwanamke akipania!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…