Mwanamke mpumbavu hubomoa nyumba yake mwenyewe, bali mwenye hekima huijenga nyumba

Mwanamke mpumbavu hubomoa nyumba yake mwenyewe, bali mwenye hekima huijenga nyumba

Showmax

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2022
Posts
6,592
Reaction score
12,707
MWANAMKE MWENYE MAKELELE

Tarehe 9/10/2021 nipo stendi ya mabasi Iringa, nimekaa karibu na wakatisha tiketi za mabasi waliokuwa wakifanya mazungumzo yao, na katika mazungumzo yale ninawasikia wakijibiza. "USIRINGE WEWE SI USHUKURU NDOA YAKO HAINA MAKELELE, MI MWENYEWE HAPA NI MNENE, BASI TUU KWA VILE MKE WANGU ANA KELELE NDIO MAANA NIMEKONDA HIVI”

Maongezi yale na majibizano ya wale watu yakaingia haswaa ndani ya moyo wangu, na yakanifanya kutafakari sana, MWANAMKE MWENYE MAKELELE, NDOA YENYE MAKELELE, ni nini hiki? Kwanini mwanaume huyu ajione kwamba afya yake imedhoofu kwasababu mke wake ana kelele?, nikawaza zaidi kwanini suala la kelele za mwanamke ni kero sana kwa wanaume?

Kile nilichokisikia kutoka kwa wanaume wale kikanipa kurudisha fikra zangu nyuma na kutafakari baadhi ya wanaume ambao nimekuwa nikihusiana nao kuanzia na mume wangu, kaka zangu, marafiki na ndugu wengine, nikagundua karibu wanaume wote hawa hawapendi kelele

Nikajiuliza zaidi, kelele ni nini mbele ya macho ya wanaume? Hii ikanikumbusha kile neno la MUNGU linasema katika kitabu cha MITHALI 21:9, 19 na MITHALI 25:24, hebu soma na mimi maandiko hayo hapa chini;

MITHALI 21:9, 19
9 Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi
19 Ni afadhali kukaa katika nchi ya nyika; Kuliko na mwanamke mgomvi, mchokozi.

MITHALI 25:24
24 Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, Kuliko katika nyumba pana pamoja na mwanamke mgomvi.

Ukisoma maandiko hayo katika tafsiri nyingine hayo maneno mwanamke mgomvi na mchokozi yametafsiriwa kama mwanamke msumbufu, mwenye kelele na mwanamke mbishi

Nyika ni mahali ambapo ni pakame, hapana maji, pana joto kali, hapana kivuli kwasababu hapana miti, na kwasababu ni mahali pakame, basi hata uzalishaji huwa ni mgumu.

Dari pia ni sehemu pweke, ni sehemu ya maficho na ni sehemu yenye giza na isiyo na uzuri kwa mtu kuishi huko.

Sasa basi, Neno la Mungu linataja maeneo haya mawili nyikani na darini kuwa ni afadhari mtu akae huko kuliko kukaa na mwanamke mgomvi, mwanamke mchokozi na mwanamke msumbufu, hii ni hatari.

Hebu tutafakari pamoja hapa yaani eti bora kwenda kukaa nyikani au darini kuliko kukaa na mwanamke?

Kwani wanawake tuna kasoro gani hadi tuogopwe kiasi hiki?

Tunatisha kwa kiwango gani hadi watu wawe radhi kwenda kuishi katika nchi kame kuliko kuishi na sisi?

Haya ni maswali ambayo kila mwanamke anapaswa kujiuliza, na kuona ni kwa kiwango gani mwanamke anapaswa kuwa makini.

Ugomvi, uchokozi na usumbufu wa mwanamke ndio unaoogopwa, unaudhi na ni kero kiasi ambacho watu huona ni bora wakakae peke yao nyikani, au darini, sehemu ya upweke kuliko kukaa na wanawake.

Sauti kali na kelele katika maongezi yetu ya kila siku inatufanya kuwa wanawake wagomvi na wakorofi, hii ni hatari.

Sauti kali, sauti yenye kelele ni sauti ya mwanamke mgomvi na mkorofi.

Kelele zinakera, kelele zinaumiza, kelele zinavuruga utaratibu, kelele zinaondoa amani

Kelele ni ishara ya ukaidi – MITHALI 7:11

Kelele ni ishara ya fujo

Makelele ya mwanamke yanaweza kuharibu na kuvuruga afya ya mwanaume kabisaaa

Ni maombi yangu kwamba MUNGU atupe neema sana kama wanawake, yapo mambo mengi ambayo tunatakiwa kuyatilia maanani ili tuweze kuwa wanawake bora, wakati mwingine mambo mengine yanaonekana ni kama sio rahisi, mengine yanaweza onekana ni kama ndivyo mtu alivyozaliwa, lakini maadamu tunaye MUNGU muumbaji wetu, tukiwa tayari kubadilika, tukajinyenyekeza kwake anaweza kutufanya kuwa watu bora zaidi

Mdomo wa mwanamke unapaswa kuepuka Mzozo/Ubishi, Malalamiko, Upinzani/Upingaji, Lugha za mashambulizi na Sauti kali/kelele. Badala yake kila mwanamke anawajibika kujifunza namna anapaswa kuzuia kinywa chake kisinene mabaya, kusoma mazingira ya nini aongee na kwa wakati gani, lakini Zaidi sana kumuomba MUNGU aweke mlinzi na mngojezi katika kinywa chake, mlinzi atakayemsaidia kunena mema na si mabaya.

MITHALI 9:13
Mwanamke mpumbavu hupiga kelele, Ni mjinga, hajui kitu

©️Cecilia Charles
Fb: Cecy de Charles
Instagram: Cecydecharles
 

Attachments

  • Screenshot_20230226_093951.jpg
    Screenshot_20230226_093951.jpg
    74 KB · Views: 10
Kelele ni mpangilio wa sauti yenye maneno yasiyofaa.
Maneno makali, machafu.
Neno ni roho na linaishi, kupitia neno mtu upata baraka au upata madhara.
Neno lenye baraka uleta uponyaji, amani, utajiri.
Maneno machafu, makali yamebeba nguvu ya uharibifu ndani yake uleta madhara ya sonona, stress, vifo, ulemavu, jela, talaka, umasikini, upungufu wa nguvu za kiume,vurugu na mivurugano katika familia, wanaume kishinda bar na kurudi usiku nyumbani, uchepukaji,kuoa mke wa pili.
Mwanamke mpumbavu upiga kelele.
 
Ndoa ni ibada. Ndoa ni muunganiko wa kiroho zaidi kuliko kimwili.
Kama huna utii, upendo na heshima acha kwenda kumchafulia mwingine cheti chake cha ndoa na kuharibu cv yake.
Ndoa sio maalumu kwa kila mtu.
Imeandikwa:

Akamwambia mwanamke,
Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako;
kwa utungu utazaa
watoto;
na tamaa yako itakuwa kwa mumeo,
naye atakutawala.

Sasa hawa wasiotaka kutawaliwa wanaenda kinyume na maandiko ndio wenye makelele makelele mengi, mwanaume aliumbwa kutawala sio kutawaliwa.
 
Huwezi
Imeandikwa:

Akamwambia mwanamke,
Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako;
kwa utungu utazaa
watoto;
na tamaa yako itakuwa kwa mumeo,
naye atakutawala.

Sasa hawa wasiotaka kutawaliwa wanaenda kinyume na maandiko ndio wenye makelele makelele mengi, mwanaume aliumbwa kutawala sio kutawaliwa.

Wanashindana kuibadili asili, asili ni asili huwezi ibadili, ukishindana kuibadili asili ni lazima utawatajirisha waganga na mitume na manabii wa uongo pasipo msaada wowote.
Maneno ya Mungu ni hakika na yalifungwa seal muhuri.
 
Wanawake ni jeshi kubwa wanao uwezo wa kuibadili Jamii kama watakaa kimya.
Kukaa kimya means kuwa na hekima.
Waweke filter kwenye vinywa vyao na sio kubwatuka hovyo. Unnecessary noice. Kitu chenye herufu tano ataongea maneno elf moja.
Mume akichoka kelele uikimbia nyumba yake. Maana ni heri uishi pekee YAKO pangoni kuliko kuishi na mke mwenye makelele.
 

Attachments

  • Screenshot_20230226_093951.jpg
    Screenshot_20230226_093951.jpg
    74 KB · Views: 8
Kama ulikosea kuoa ukaangukia kwenye kelele ukifika miaka 50 au 60 keep distance kama unataka kuishi maisha marefu.
Tafuta Shamba nje ya mji jenga mji weka mifugo, mazao, tafuta Shamba boy wajakazi. Kaa huko Acha wao wakae mjini, mwenye shida nae atakufata Shamba kukusalimia, akitosheka arudi zake mjini. Bila hivyo utakufa siku si zako.
Magonjwa ya uzee mfano, kisukari, pressure, stress, stroke, chanzo kikuu ni makelele
 
Kelele ni mpangilio wa sauti yenye maneno yasiyofaa.
Maneno makali, machafu.
Neno ni roho na linaishi, kupitia neno mtu upata baraka au upata madhara.
Neno lenye baraka uleta uponyaji, amani, utajiri.
Maneno machafu, makali yamebeba nguvu ya uharibifu ndani yake uleta madhara ya sonona, stress, vifo, ulemavu, jela, talaka, umasikini, upungufu wa nguvu za kiume,vurugu na mivurugano katika familia, wanaume kishinda bar na kurudi usiku nyumbani, uchepukaji,kuoa mke wa pili.
Mwanamke mpumbavu upiga kelele.
Umetumia tafsida kali na nzuri sana
 
Mungu akibariki kinywa changu kikawe neema kwa kaka mzuri na wote wanaonizunguka.
Amen
 
Sema tu vitabu vya dini vimeongelea sana wanawake in negative side, kuna wanaume wajinga sana ila ndo wanajifi ha kwenye uananume
 
Sema tu vitabu vya dini vimeongelea sana wanawake in negative side, kuna wanaume wajinga sana ila ndo wanajifi ha kwenye uananume
Kwahiyo wewe unajifanya una akili kuliko watu walioishi miaka zaid ya 900 wakandika vitabu hivyo??
YAn wewe una akil kuliko Mungu na mitume wake wote? 😂
 
Sema tu vitabu vya dini vimeongelea sana wanawake in negative side, kuna wanaume wajinga sana ila ndo wanajifi ha kwenye uananume
Umeona.!! Sijui kwann hili hawalioni.
 
Kwahiyo wewe unajifanya una akili kuliko watu walioishi miaka zaid ya 900 wakandika vitabu hivyo??
YAn wewe una akil kuliko Mungu na mitume wake wote? 😂
Mtoto wa kiume unajibu hoja kwa kuchekacheka na vi emoji,

Inawezekana na wewe ni miongoni mwa qapumbafu ndo mana unaamini upumbafu upo kwa wanawake pekee
 
Mtoto wa kiume unajibu hoja kwa kuchekacheka na vi emoji,

Inawezekana na wewe ni miongoni mwa qapumbafu ndo mana unaamini upumbafu upo kwa wanawake pekee
Usiwe na hasira
Jibu hoja
 
Back
Top Bottom