Mwanamke

Mwanamke

Hata mimi nimeshahitimisha kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu.

Kwa sababu haingii akilini kuona mwanamke akimtusi mwanamume kuwa eti 'ana mambo ya kike'.

Mambo ya kike yangekuwa si 'mabaya' kwa nini sasa hata hao hao wanawake wangeyahusisha na tusi?

Na imani yangu ni kwamba hata wao wanawake [na hapa nazungumzia kiujumla jumla tu] huwa wanajiona ni viumbe duni mbele ya wanaume.

mtoto wa kike na wa kiume wanalelewa na mama aliyekuwa programmed kuwa mwanamke ni dhaifu na mwanaume ni shujaa na kuna mifumo ya kijamii ya kufanya iwe hivyo. Kwa hiyo toka utotoni watoto wote wanakuwa programmed hivyo. Kwa hiyo si ajabu kukuta mwanamke akimdharau mwanamke mwenzie kwa sababu ndivyo wanavyojiona. Mtoto wa kike aliyelelewa katika mazingira ya usawa wa kibinadamu mara nyingi hujikuta akiambatana zaidi na wanaume kuliko wanawake waliolelewa katika mazingira ya "mwanamke dhaifu". Hutamkuta akiomba "favours" - anajua kujitegemea na kusimama mwenyewe. Huyu hawezi kukaa na wanawake walioambiwa na kuamini hawajiwezi bila msaada wa wanaume. Na mwanamke wa aina hii wanaume humgwaya kwa sababu haenei kwenye fremu wanayoijua ya mwanamke; wanawake waliokubali kuwa ni dhaifu pia humbeza na kusema anajitia kufanya mambo ya kiume. Hata akigombea uenyekiti wa kitongoji hawamchagui kwa sababu walishaambiwa na kuamini mwanamke kwake jikoni. Kwa hiyo mwanamke kujiona kiumbe dhaifu si ajabu, na mama kumtukania mwanae sehemu zake za siri ni mwendelezo wa mfumo ule ule wa "mwenye nguvu kumuonea "dhaifu". Mimi siku hizi hata sishangai kuskia mwanamke anajitukana, au yuko ofisi flani ananyanyasa wenzie. Ni kwamba wamerithi mifumo kandamizi.
 
Kiuhalusia sisi ni wadhaifu na ndio maana MWENYEZI MUNGU aliwaamrisha muishi na sisi kwa umakini mkubwa........... Ukiyafata hayo hutoona tabu kuishi nasisi

hapo kwenye "sisi" weka "mimi". Mtu dhaifu unaishi nae kwa umakini ili iweje? Ukiona mtu anahangaika kukukandamiza kwa nguvu au kwa maneno na nyimbo ujue una nguvu kwa hiyo anataka kuendelea kukunyonya. Usimsingizie Mwenyenzi Mungu. Mbona kuna wanawake ndo wanalisha familia na kusomesha watoto na kutunza wazazi na kuendesha vijiji na nchi? Au mungu wao mwingine?
 
hapo kwenye "sisi" weka "mimi". Mtu dhaifu unaishi nae kwa umakini ili iweje? Ukiona mtu anahangaika kukukandamiza kwa nguvu au kwa maneno na nyimbo ujue una nguvu kwa hiyo anataka kuendelea kukunyonya. Usimsingizie Mwenyenzi Mungu. Mbona kuna wanawake ndo wanalisha familia na kusomesha watoto na kutunza wazazi na kuendesha vijiji na nchi? Au mungu wao mwingine?

Kwa batili mbaya sio mzuri kwenye notes ukitaka tuelewane njoo inbox nikudadavulie
 
Nimekuwa nikijiuliza kwa muda mrefu sana kama mtu kuzaliwa mwanamke ni laana, hususan katika hii jamii yetu. Kwanini nimekuwa nikijiuliza hivyo? Sababu ni nyingi na hapo chini nitazitaja chache.

Uanamke umekuwa ukihusishwa na mambo mabaya mabaya tu. Tusi kubwa kwenye lugha ya Kiswahili linahusu kiungo cha uzazi cha mwanamke [mfano, K ya mamako].

Ukitaka kumtusi mwanaume basi mwambie kuwa 'ana mambo ya kike'. Kwanza, mambo ya kike ni yepi hayo? Na pili, kwa nini kuwa na mambo ya kike kutumiwe au kuchukuliwe kuwa ni tusi?

Cha kusikitisha zaidi ni unakuta wanawake nao wako mstari wa mbele katika kuendeleza hiyo dhana ya uanamke kuwa tusi.Hata humu tumeshaona watu ambao wamejipambanua kuwa ni wadada/ wanawake wakisema waziwazi kuwa wao hawana marafiki wengi wanawake na kwamba marafiki zao wengi ni wanaume.

Mwanamke kuwa na marafiki wengi walio wanawake ni mkosi, au? Vile vile, humu humu jamvini tumeshaona watu wajipambanuao kuwa ni wanawake wakiwatukana watu wajipambanuao kuwa ni wanaume na kuwaita ama kuwaambia kuwa wana mambo ya kike.

Inasikitisha kuona mtu ajipambanuaye kuwa ni mwanamke akitumia hiyo hiyo hali ya uanamke kumtusi mtu mwingine. Wakati mwingine huwa nakubaliana na ule usemi wa kwamba adui wa mwanamke ni mwanamke.

Wadau nyie mna maoni gani?
Halafu
 
Back
Top Bottom