TANZIA Mwanamuziki Waziri Sonyo afariki dunia

Basi mijitu itaanza, ooh, tuchukue tahadhari, ni mwaka upi watu hawakufa?
Basi mijitu itaanza, ooh tusichukue tahadhari, ooh ni mwaka upi watu hawakufa? Hii hata kama viashiria vyote vinaonyesha zama hizi si zile.

Zama zile pneumonia watoto wadogo. Leo hadi kina Mpango na machozi juu?
 
Hivi Mtaji wa masikini aliutunga yeye?
 
Be careful when you write because it will remain on record.
Mwenzio kauliza Miss Zomboko na yule Zomboko anayechambua mambo ya muziki wa dance
Haa ha ha, nimekuelewa mkuu but rudia tena, jamaa kazungunzia habari za Uzalamo wao mi ndio nikaandika vile, but i do appreciate hasa hapo uliposema "be careful"
 
sikosagi mkuu nyimbo za zomboko nilivyo kuwa mdogo wazazi na mabro walikuwa wakizisikiliza nilikuwa sizipendi,
Nashangaa nimeanza kuzipenda kipindi hiki kinoma,,,,sijui nimekuwa mzee?


Mkuu kitonsa nimecheka sana, hata Mimi oldies nilikuwa zisipendi sana, but nowadays nazikubali sana!

Anyway mkuu, hili jina kitonsa, kama nalikumbuka Fulani kulikuwa na dereva mmoja wa police mnene sana anaendesha Yale makarandinga (malori) ya wafungwa ya police, Leyland Daf Comet, alikuwa anaitwa "kitonsa" vipi hakuna uhusiano na huyo jamaa?!

R.I.p kwake Waziri Sonyo!
 
RIP Sonyo Waziri
Nakumbuka nyimbo zake akiwa African Revolution (wana Tamtam) akiwa na Badi Bakule, Mviko Sound, Chuchu Sound na TOT. Jamaa alikuwa na sauti nzuri sana. Naweka hapa vibao vyake viwili, akiwa Mviko na akiwa African Revolution ya Asha Baraka
 

Attachments

kitonsa alikuwa mhuni maarufu kariakoo ,sina husiano naye ,ila masela walinipa kumwakilisha msela

Hizi nyimbo za zomboko zinanikumbusha sana marehemu mama na baba ,sinanipa hisia sana
 
kitonsa alikuwa mhuni maarufu kariakoo ,sina husiano naye ,ila masela walinipa kumwakilisha msela

Hizi nyimbo za zomboko zinanikumbusha sana marehemu mama na baba ,sinanipa hisia sana


Daah, kumbe basi sikulijua hili mkuu, kuna dereva bonge nae walikuwa wanamwita kitonsa miaka ya 90.

Kweli hizi nyimbo za zamani zinagusa hisia sana, nimezijaza sana kwenye memory ya simu yangu,

Nakumbuka mzee wangu (rip kwake) alikuwa na radio cassette yake aina ya Phillips 540 enzi hizo, alinunua miaka ya 60's alikuwa anapiga sana kanda za miziki ya zamani, nyingi alizinunua moja ya duka maarufu sana la kanda za muziki pale kurasini likiitwa "Bukavu!"
 

Kweli ukimsahau mtu ujui kinacho endelea baada ya kutafuta youtube kuna nyimbo ndoto tata

Kipindi wasanii wa zamani wanaimba walikuwa wanajieshimu sana lakini siku hizi mpelekee moto,ingiza kama inabana.aibu tupu
 
Kwahiyo sauti ya radi lazima ajifungie ndani
Inawezekana alikuwa nayo tayari.Shida ni huko kaambukiza wangapi huko mpirani,@,kwenye daladala.R.IP Waziri Sonyo. Halafu wanene inawaondoa faster.
 
Safi mnooooooooo
 
Kiongozi kama una nyimbo ya Beatrice ya Mzee zahir zollo naomba nisaidie plz
 
Kiongozi kama una nyimbo ya Beatrice ya Mzee zahir zollo naomba nisaidie plz
Huo wimbo sina, ila kuna thread yenye nyimbo mbali mbali, huo wimbo kuna mtu ali upload. Ingia kwenye search hapo juu, andika jina na mtunzi, utaupata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…