DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
ila huyu mzazi ana moyo sana hakika mimi nisinge ondoka hapo ni lazima ningekula sahani moja na huyo Mwl nisinge kubali hiyo elfu ishirini ….yani hiyo mbwa ingejuta! Lakini bado nafasi ipo huyu mtu anapaswa kusakwa!
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dorothy Gwajima akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Mwalimu wa field? Huyo ni mwalimu wa aina gani. Mwalimu mkuu bado yuko madarakani?
 
Kama imefikia hatua Waziri anarusha mpira kwa mtu aliye chini yake kwa tukio la kikatili na kupelekea mauaji kwa namna hii basi nchi haina uongozi.

Inaumiza sana kuuliwa mwanao alafu walioshika mpini wanalindana, haki mzazi achana na hiyo maiti hadi haki ipatikane vinginevyo ukiibeba umeruhusu jinai kuwa haki.
 
Kuna walimu ni vichaa, miaka 7 unampiga ngumi....hata kama angekua na 30 viboko si vipo kama kuna ulazima wa viboko.

Pumzika kwa amani toto, pole sana mzazi 😢
Huyo sio mwalimu ni mbwa tuuu! Yani huyu ni kula nae sahani moja…..hapa ndio naoma umuhimu wa kuroga huyu anatakiwa kufanywa awe ana jikojolea tuu muda wote….
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dorothy Gwajima akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Poleni wafiwa.
Mungu awape faraja.
 
Kama imefikia hatua Waziri anarusha mpira kwa mtu aliye chini yake kwa tukio la kikatili na kupelekea mauaji kwa namna hii basi nchi haina uongozi.

Inaumiza sana kuuliwa mwanao alafu walioshika mpini wanalindana, haki mzazi achana na hiyo maiti hadi haki ipatikane vinginevyo ukiibeba umeruhusu jinai kuwa haki.
Kimsingi siwezi kutoa lawama sana kwa waziri kwa sababu kimsingi awezi fanya kila kazi mwenyewe anapaswa kusaidiwa lakini anachotakiwa kuhakikisha wanao msaidia wawe active na wawe ni wenye uelewa na utu sio wajinga wajinga,jeuri ,kibri na dharau …dawati linapaswa liwe na watu wenye utu!

Kimsingi hao watu watamuharibia sana Dkt. Gwajima D sifa zake na juhudi zake maana kila mwana jf anajua anavyo jitahidi kujibu na kutolea ufafanuzi na kushughuliakia matatizo ya watu na ni kati ya mawaziri walio active sana hapa na hawaogopi mijadala…
Bila shaka atakuja kulijibu hili swala maana watu kama hawa wanao puuza watu hawapaswi kumzunguka wana muharibia sana sana!
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.
Pole mama.

Umasikini ni aghari, mama kitu cha kwanza haukutakiwa kuipokea hiyo shs. 20,000/=, kwa kifupi shule ilitumia udhaifu huo kukusukumia mzigo wewe mzazi, mzazi ulitakiwa ukaripoti polisi kwa hatua za kisheria badala ya kujadiliana na shule, pia shule ilitakiwa ichukue jukumu la matibabu ya mwanao wewe ukiwa msindikizaji tu.

Udhaifu wa kupokea ile pesa ili umpeleke hospitali ndiko kulikoifanya shule ikuambie gharamis upasuaji watakurudishia pesa zako, kwa kifupi walijitoa kwenye tatizo hilo.

Mama hapo Moshi ipo mamlaka ya wizara ya elimu inayosimamia shule zote, pia yupo mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa ambao ulitakiwa uende ofisini kwao kuwajulisha kuhusu tatizo hilo.

Mwisho ulitakiwa upate ripoti ya kina mobiTuki yaani postmortem ya maiti. Hii postmortem inakuwezesha kufungua kesi ya jinai dhidi ya shule na mwalimu.

Mwisho, kabla ya kupeleka tatizo lako kwa Waziri anza na viongozi wa mkoani mwako, vinginevyo utadhani unakosa msaada kumbe ni njia ambazo si sahihi unazotumia.
 
Pole mama.
Umasikini ni aghari, mama kitu cha kwanza haukutakiwa kuipokea hiyo shs. 20,000/=, kwa kifupi shule ilitumia udhaifu huo kukusukumia mzigo wewe mzazi, mzazi ulitakiwa ukaripoti polisi kwa hatua za kisheria badala ya kujadiliana na shule, pia shule ilitakiwa ichukue jukumu la matibabu ya mwanao wewe ukiwa msindikizaji tu. Udhaifu wa kupokea ile pesa ili umpeleke hospitali ndiko kulikoifanya shule ikuambie gharamis upasuaji watakurudishia pesa zako, kwa kifupi walijitoa kwenye tatizo hilo.
Mama hapo Moshi ipo mamlaka ya wizara ya elimu inayosimamia shule zote, pia yupo mkuu wa wilaya na mkuu wa mkoa ambao ulitakiwa uende ofisini kwao kuwajulisha kuhusu tatizo hilo.
Mwisho ulitakiwa upate ripoti ya kina mobiTuki yaani postmortem ya maiti. Hii postmortem inakuwezesha kufungua kesi ya jinai dhidi ya shule na mwalimu.
Mwisho, kabla ya kupeleka tatizo lako kwa Waziri anza na viongozi wa mkoani mwako, vinginevyo utadhani unakosa msaada kumbe ni njia ambazo si sahihi unazotumia.
Shida ni umaskini jamani huyu mtu alicho jali mwanzo ni uhai na afya ya mtoto hakujua kama yange pelea haya!
 
Back
Top Bottom