DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

DOKEZO Mwanangu ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inazungushwa

  • Thread starter Thread starter Anonymous
  • Start date Start date
Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kimsingi siwezi kutoa lawama sana kwa waziri kwa sababu kimsingi awezi fanya kila kazi mwenyewe anapaswa kusaidiwa lakini anachotakiwa kuhakikisha wanao msaidia wawe active na wawe ni wenye uelewa na utu sio wajinga wajinga,jeuri ,kibri na dharau …dawati linapaswa liwe na watu wenye utu!

Kimsingi hao watu watamuharibia sana Dkt. Gwajima D sifa zake na juhudi zake maana kila mwana jf anajua anavyo jitahidi kujibu na kutolea ufafanuzi na kushughuliakia matatizo ya watu na ni kati ya mawaziri walio active sana hapa na hawaogopi mijadala…
Bila shaka atakuja kulijibu hili swala maana watu kama hawa wanao puuza watu hawapaswi kumzunguka wana muharibia sana sana!
Nyumba ikiharibika lawama ni kwa kiongozi wa nyumba haijalishi upo low or high mental.
 
Poleni sana Kwa Msiba huo...

Hivi inaingia akilini kabisa wewe Mwalimu mtu mzima uanze kumchapa mtoto hadi kumpiga na ngumi kabisa?

Angekuwa mtoto wako ungemfanyia hivyo?

Tuweni na kiasi jamani, it's unfair kumfanyia mtoto mdogo ukatili Mkubwa hivyo hadi kupelekea apoteze maisha🥲

Kuna wakati nilisoma mahali kwamba Viboko vimepigwa marufuku mashuleni hadi Kwa Kibali maalumu cha Mkuu wa Shule n.k na mwisho ilikuwa Viboko kama sikosei 2 ama 3, Je huyo Mwalimu alipewa kibali cha kumchapa huyo mtoto.
 
ushauri wa bure hata akienda mahakamani hatapata haki huyo mama dr gwajima hatamsaidia nchi hii , kila mtu anajua hadi yaliyoshindikana mahakamani makonda anaweza kuyatatua amvizie makonda kila anakoenda amweleze shida yake ndio ukweli wa nchi yetu akishindwa makonda amwachie Mungu au achukue mwili na kwenda kuroga mwisho.
 
ushauri wa bure hata akienda mahakamani hatapata haki huyo mama dr gwajima hatamsaidia nchi hii , kila mtu anajua hadi yaliyoshindikana mahakamani makonda anaweza kuyatatua amvizie makonda kila anakoenda amweleze shida yake ndio ukweli wa nchi yetu akishindwa makonda amwachie Mungu au achukue mwili na kwenda kuroga mwisho.
Makonda ndo mahakama anatoa haki? Mkuu jitafakari
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan

Pole sana Mkuu
Dkt. Gwajima D kuna kazi huku
 
Makonda ndo mahakama anatoa haki? Mkuu jitafakari
labda hujanielewa mleta mada amesema waziri muhusika na maswala hayo dr gwajima ameshindwa zipo kesi nyingi watu wanapata dhulma na watendaji wa mahakama, kwanini kwa makonda ni rahisi kusaidiwa serikali inatumia mfumo huo kwa maslahi ya chama ccm, lakini nani alikwambia mahakamani wanatoa haki, pata shida ya kisheria ndo utajua hakuna haki kule haki yako unaipigania utatoa pesa kumpata wakili na mengineyo, ukiwa huna pesa mahakama haikupi haki wewe, sio mahakamani tu hata ukienda polisi baadhi ya maeneo ukawaambie mda huu kuna majambazi yanaiba nyumbani kwangu na kubaka usipotoa hela ya mafuta hawaji yani utarudi nyumbani majambazi wamepika na ugali wamechinja kuku wamekula wameondoka zao.
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Nimesisimka Kwa uchungu
 
Kwanini Dr D kamrudisha mara 2 kwa yule yule aliekataa kunsaidia?
Najiuliza hili swali sana
Msipopiga marufuku kuchapa watakufa wengi kwa upumbavu wenu
Ipo siku mwalimu atachinjwa pia ndio mtajua hamjui
Unampiga mtoto kama una uadui nae
Ngumi kweli mtoto mdogo why?
Mmezidi unyonge
 

Naitwa Janeth Shayo, mkazi wa Uru, Moshi. Naomba unisaidie kupaza sauti mwanangu Jonathan Makanyaga (07) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Mrupanga, ameuawa kwa kupigwa na Mwalimu lakini kesi inataka kupindishwa.

Tar.28/02/2024 mwanangu alienda shuleni akiwa mzima. Alipofika aliadhibiwa kwa kuchelewa "namba". Alipoingia darasani alianza kutokwa damu puani na mdomoni. Akarudishwa nyumbani. Nilipomkagua nikamkuta na majeraha yaliyovilia damu mgongoni, kwenye mbavu na mguuni.

Kesho yake nikaenda nae shuleni kutaka kuoneshwa mwalimu aliyemfanyia ukatili mwanangu. Lakini Mwalimu mkuu akaomba nibaki nje. Akaingia na mwanangu ofisi ya walimu na kumtaka amtambue Mwalimu aliyemuadhibu. Mwanangu akamtanbua. Mwalimu Mkuu akaniambia wameshamfahamu ni mwalimu wa "Field" hivyo atazungumza nae.

Wakanipa 20,000/= za matibabu. Nikampeleka mwanangu zahanati. Kesho yake akazidi kutoka damu, na kulalamikia maumivu sehemu za mbavu. Nikampeleka hospitali ya masista. Daktari akaniambia bandama imejeruhika ndio sababu ya kutoka damu mdomoni. Mtoto alidai pamoja na viboko alivyochapwa, Mwalimu pia alimpiga ngumi tumboni. Huenda ndiyo iliyopasua bandama.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya tukapewa rufaa kwenda KCMC. Akatakiwa kufanyiwa upasuaji. Gharama 350,000/= lakini sikuwa nayo. Nikapiga simu shuleni wakasema tuombe afanyiwe halafu watalipa baadae. Hata hivyo kabla hajafanyiwa hali yake ikazidi kuzorota, akashindwa kupumua, akawekwa kwenye Oxygen. Akashindwa kula, akawekewa mpira wa chakula. Baada ya siku chache akafariki 😭.

Lakini ripoti ya hospitali inasema mwanangu amekufa kwa kansa ya damu. Kansa gani ya damu inayomuua mtoto kwa wiki mbili? Na kwanini hiyo kansa itokee baada ya kuadhibiwa shuleni? Kwanini Mwalimu aliyemuadhibu mwanangu anafichwa, na sipewi haki ya kumfahamu?

Nalazimishwa nichukue maiti nikazike lakini nimekataa. Nataka uchunguzi huru. Nimeenda dawati la jinsia kulalamika nikapuuzwa. Nimepiga simu kwa Waziri Dkt. Gwajima D akanipa namba ya mtu wa kunisaidia. Nilipopiga kumbe ni yuleyule Mkuu wa dawati la jinsia aliyenipuuza. Nikamrudia Gwajima akasema niwasiliane nae huyohuyo. Nimekosa pa kulilia haki ya mwanangu Jonathan
Nchi inalaaniwa kwa mambo kama haya.
 
Back
Top Bottom