Mwanangu anapenda kuwa Askari polisi namsaidiaje kufuta fikra hizo?

Mwanangu anapenda kuwa Askari polisi namsaidiaje kufuta fikra hizo?

Rozela

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2024
Posts
845
Reaction score
2,235
Yuko primary, ameniambia zaidi ya mara 5 kuwa anatamani sana kuwa askari polisi, ikifika jioni jioni anaanza kupiga kwata kuzunguka nyumba na kupiga saluti.

Akikutana na wenzake anataka wacheze kipolisi yeye awe askari polisi, siku nyingine anaigiza kuongoza magari na kuongoza wanafunzi kuvuka barabara.

Leo ndio funga kazi, baada ya kufunga shule kapitia kituo jirani cha polisi kaja na majarida kadhaa kuhusu mambo ya usalama wa raia inaonesha alienda kuwahoji maswali kadhaa wakampa zawadi.

AKienda shule anarudi akiwa msafi vilevile anasema polisi sio wachafu.

NAMTOAJE KWENYE HILI JANGA WAKUU BILA KUM-ATHIRI KISAIKOLOJIA?
 
Stop it ndugu .
Nipo chini ya miguu yako naomba muache mwanao aamue hatma yake, Ikiwa hautakuwa tayari kumlea kwasababu hiyo naomba awe mwanangu wa hiyari nipambane kuitimiza ndoto yake.

Yuko primary, ameniambia zaidi ya mara 5 kuwa anatamani sana kuwa askari polisi, ikifika jioni jioni anaanza kupiga kwata kuzunguka nyumba na kupiga saluti...
 
Mlee kwa namna ambayo itamfundisha uadilifu, uwazi na haki

Hapo utamsaidia aje kuwa polisi mzuri sana

Atatoa mchango kwenye jamii na ataridhika kimaisha(fulfilment)
 
polisi nao ni binadamu na si wote wana ubaya kwa raia, ikiwa mtoto wako akabahatika kupata nafasi muache aende huko.

ikiwa tutahukumu watu kwa kada zao hakuna msafi miongoni mwetu.;

1. Watendaji serikalini hawa baadhi yao wanakwamisha maendeleo rejea sakata jairo, issue ya masamaki wa tra.

2. Wanasiasa hawa wanatuuza rejea issue ya ununuzi wa rada au issue ya prof. mahalu na sakata la ununuzi wa jengo kule italy kipindi cha mkapa

Note: uadilifu wa mtu haupimwi kwa kazi anayoifanya bali matendo yake.
 
Yuko primary, ameniambia zaidi ya mara 5 kuwa anatamani sana kuwa askari polisi, ikifika jioni jioni anaanza kupiga kwata kuzunguka nyumba na kupiga saluti...
Uaskari pia ni kazi njema madam mtu ana wito. Inawezekana akaenda kuwa chachu ya mabadiliko. Mfundishe tu ajue maana ya kuwa Askari polisi, wajibu na maadili yanayotakiwa.
 
Taasisi ya POLISI haina tatizo, tatizo lipo kwa baadhi ya watumishi wake wasio waadilifu. Mimi Nina jamaa zangu ni askari POLISI na hawana tatizo lolote.

Itapendeza wewe Mzazi kama ukianza mapema kumjenga mwanao aje kuwa askari POLISI mwadilifu asaidie jamii na wanyonge.

Usiue ndoto za bwana mdogo.
 
Uaskari pia ni kazi njema madam mtu ana wito. Inawezekana akaenda kuwa chachu ya mabadiliko. Mfundishe tu ajue maana ya kuwa Askari polisi, wajibu na maadili yanayotakiwa.
Jambo afande ; Jambo

Kuhusu maelekezo: anaelezea instructions zoteee

Maafande kwa pamoja : Wazi afande

Ukiwa afande kubali kushikiwa akili maana huto ruhusiwa kuhoji ukiwa na cheo kidogo ni mtu wakupokea/ kutekeleza maagizo kutoka JUU.


ni kuitikia kwa sauti.
WAZI AFANDE.

Nimefanya hizo kazi nimekaa huko kwa miaka minne.
 
Back
Top Bottom