Mwanangu Chalamila umerudia tena kunigombanisha na wapiga kura? Hapana mama nimesema ukweli wa hali ilivyo...poa

Mwanangu Chalamila umerudia tena kunigombanisha na wapiga kura? Hapana mama nimesema ukweli wa hali ilivyo...poa

Resilience

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2023
Posts
1,096
Reaction score
4,948
Muda mfupi kabla ya kuondolewa kwa Mkuu wa Mkoa wa DAR es salaam nafsi za mteua na mteuliwa zitakuwa zinajiuliza maswali haya mawili
Mwanangu Chalamila kwanini umenigombanisha na wananchi ?

Hapana mama nilitaka wafahamu ukweli wafanye kazi nakufahamu kwamba huduma ya afya ni gharama kubwa na wanapaswa kugharamia

Nimekuelewa lakini umeongea lugha ambayo haina ubinadamu. Hivi kijijini wanaweZa wakapata 50,000 kwa hali ya uchumi ilivyo? Unafahamu msimamo wa serikali kuhusu huduma ya afya? Unafahamu kwamba haki ya kuishi ni kipaombele cha kila serikali? Unaposema mtoto afe na mzazi afe na ukasema ni uzembe unamaanisha nini?

Je, ni lini serikali inayoongoza imewahi kutoa huo msimamo wako?

I'm sory mama
 
IMG-20250126-WA0074.jpg
 
Lakini wakati ufike tuseme ukweli! Ngono na kungoneka ufanye wewe alafu kuzaa tugharimie wengine! Astaghafullulah! Wakati mimba imekaa miezi 9 hukujua utakuja kujifungua? Acha masikhara nyie waswahili!
 
Hospitali inakosa gloves za 1000 halafu Rais anatapanya pesa kununua magoli kwa milioni 5, ni punguani pekeyake anayeweza kuunga mkono huu ujinga wa wana ccm na mama yao
Sasa wewe miezi 9 umekosa gloves za buku ukitegemea utapata bure? Acha ngono! Ukitaka kuzaa jipange!
 
Sasa wewe miezi 9 umekosa gloves za buku ukitegemea utapata bure? Acha ngono! Ukitaka kuzaa jipange!
Huku kwetu mtaa mzima mwenye cash 30,000/ ni balozi wa mtaa Jana alipata pesa hiyo kwa udalali wa kuuziana shamba la dhuluma!!

Nakushangaa unayetamka hiyo 50k
 
Wakina mama wote Tanzania waungane wamkatae Samia kwenye sanduku la kura maana ccm wameshindwa kuboresha huduma za afya.
 
Sasa Chalamila nje ya ukuu wa mkoa kauli zake ni hatari zaidi,

Rejea Ile kauli ya " Tupate Katiba mpya haraka Ili Makamo asije akam.....ceo Ili aupate uceo kirahisi.

Aachwe tu nadhani.
 
Muda mfupi kabla ya kuondolewa kwa Mkuu wa Mkoa wa DAR es salaam nafsi za mteua na mteuliwa zitakuwa zinajiuliza maswali haya mawili
Mwanangu Chalamila kwanini umenigombanisha na wananchi ?

I'm sory mama
Huyu Chalamila si ndie aliwaambia watu wa Mwanza Samia anakuja ukitaka kuandika ujumbe kwenye bango uko huru, hata kama unataka kumtukana?

Na Samia bado hajakoma nae tu? Labda wana historia.
 
Wapannga mikakati wa CHADEMA naona wanachukua kila tamko na kujiandaa kuwalipusha wananchi.
 
Back
Top Bottom