Mwanangu kaniuliza baba mbona mama kajaa tumbo (mjamzito) nimepatwa na kigugumizi. Wewe ungejibuje?

Mwanangu kaniuliza baba mbona mama kajaa tumbo (mjamzito) nimepatwa na kigugumizi. Wewe ungejibuje?

Shida ni curiosity
Baadhi ya watoto wakijua mtoto anapatikana
Baada ya sex huenda kujaribu Ku sex ili wapate na wao watoto...

Kumbuka watoto huona mtoto mdogo ni kama mdoli...

Kingine ukiwaambia kuna Mtoto ndani ya tumbo huwezi jua curiosity Yao itaishia wapi?
Wanaweza hata kujipasua tumbo ili waone Kama na wao kuna Mtoto..
Some informations ni dangerous Kwa watoto
Wakipewa jumla jumla
Aya ya mwisho ni nyeti na muhimu kwelikweli aisee Asante mkuu The Boss maana asipojipasua yeye tumbo kwa maumivu atawapasua wengine Kama wanavyowapasua vyura.
 
Swali hili nililoulizwa na mwanangu Justine wa miaka 4 limeniacha mdomo wazi na nimeshikwa na kigugumizi.

BABA MBONA MAMA KAJAA TUMBO?

Wewe ungejibuje hebu tusaidiane wakulungwa.
Majibu utakayompa yalingane na upeo wake na uwezo wa kupambanua mambo, usimpe majibu makubwa kuliko uelewa wake na usimpe majibu mepesi chini ya kiwango cha uelewa wake maana kila jibu utakalompa litazaa swali, pia majobu yalingane na jinsia yake, watoto wa kiume hulka zao ni tofauti na wa kike

Wakati niko na mimba ya last born wangu, my first born alikua around 6 yrs na alijua grade one, ilifika wakati tukaanza kuwajenga watoto wetu kwamba we are expecting a baby na mtakua na mdogo wenu na tukawaambia mpaka jinsia, sababu ilikua ni kuwajenga kisaikolojia ili mtoto atakapozaliwa wasiwe na mapokeo tofauti,

Siku moja nikaenda shuleni kwa mwanangu kupeleka risiti za ada, kumbe aliniona na akawaonyesha wenzake kwamba yule ni mama yangu

Jioni aliporusi nyumbani akaniambia mamy Makayla told me that you ara having a baby in your stomach thats why your stomach is too big, ilibidi tu nimwambie ni kweli na ndio maana tuliwaambia kwamba we are expecting a baby, mwanangu wa kiume yeye hakuhangaika na maswali mengi aliridhika na jibu na akaendelea kuendesha magari yake, shida ni huyu wa kike

maswali yaliyozuka hapo yalikua ni mengi na inabidi akili kuyajibu maana kila unachomjibu kinaweza kuzaa swali na asiporidhika atawauliza wenzie shuleni au hata mwalimu, akija anakuja na jibu la mwalimu na jibu la marafiki basi ni vurugu tupu

Swali kubwa hapo aliuliza huyo baby ameingiaje kwenye stomach yako na atatokaje, hapa ndio ilibidi nimdanganye tu kwamba kuna sindano ukichoma baby anaingia kwenye stomach na dokta anapasua stomach anamtoa then you be back to noramal akili yake ikatulia lakini kila tukiona mjamzito ananiambia mama yule ana baby kwenye tumbo

Kids are so curious sometimes ni kutafuta namna ya kuwaeleza isiwe uongo sana maana watoto wa karne hii wanajua vitu vingi na wana intereact na wenzao in unexpected ways
 
Mwambie ni mimba
Ni mtoto ...
Mungu ndo kamuweka humo

Usiwabanie watoto experience hiyo
Mwambie mdogo wake anakuja
Ila usitaje sex.. mwambie Tu mliomba Mungu
Ndo anamleta..
Vip kama ukimwambia mlifanya tabia mbaya ndo maana tumbo la mtoto limejaa
 
Vip kama ukimwambia mlifanya tabia mbaya ndo maana tumbo la mtoto limejaa
Hutakiwi kumwambia anaweza ama kujaribu aone au kuchukia sex pia sio nzuri
Muepushe mtoto na chochote kitako chompa mawazo
 
Halafu ngoja...

Sie wa pande hizi enzi hizo tulikuwa tunadanganywa mtoto anapatikana baharini... wazee wetu Mungu anawaona!!

Hivi wale ambako bahari hamna watoto wao walikuwa wanawadanganya mtoto anapatikana wapi?!

Mizee ya enzi za Nyerere bure kabisa!!!

Halafu tukishindwa kufanya uvumbuzi mtuambie vijana wa siku hata ubunifu hatuna wakati mmeanza kutulisha ujinga tangu tukiwa makinda!! Hivi walikuwa wanafikiria nini hawa?! Mtoto na bahari wapi na wapi?! Aaarrrgh!!

Btw, hivi sasa watoto wakiwauliza mtoto anapatikana wapi huwa mnawajibu nini?!
Maisha yako yote wewe ni kulalamika tu, kila jambo wewe ni kulalama tu jamani huoni aibu mwanaume mzima?
Khaaaaaa
 
Hutakiwi kumwambia anaweza ama kujaribu aone au kuchukia sex pia sio nzuri
Muepushe mtoto na chochote kitako chompa mawazo
Mtoto Anatakiwa aambiwe mama ameshiba hamna haja ya kumuelezea hayo yote
 
Maisha yako yote wewe ni kulalamika tu, kila jambo wewe ni kulalama tu jamani huoni aibu mwanaume mzima?
Khaaaaaa
Unaweza kuniambia nimewahi kulalamikia nini wakati hata hiyo ID yako yenyewe siifahamu kwa sababu you sound too irrelavant kwangu!! Au unaweza kutaja nilicholalamika kwenye hiyo post ni nini?!
 
Back
Top Bottom