Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Inasikitisha sana ad nmehisi msisimko mwilin,jariribu kua Karibu nae ili uwajue marafik zake pia yawezekana aliupata kupitia vitu vyenye nja Kali au saloon

Mungu akutie nguvu ndugu!
 
Duuh, Mungu awajalie moyo waenye subra, ni ngumu kumeza lakini kaeni mpange namna ya kumtunza mtoto wenu.

Pengine katika matibabu yake, kuna dakatari, au mtu wa maabara au nurse mchoma sindano alifanya uzembe akatumia kifaa ambacho tayari kimetumika.

Au pengine amechangia nyembe za kuchongea pencil shuleni, au kukatia kucha na the like. Kifupi inauma sana
 
Kwa hiyo katika maelezo yoooote wewe umeona hilo tu??
Ngoja yakukute utaipeleka hospital ikapimwe hadi gari unayopanda.
Usicatch feelings haraka hivyo mama!.. Wengine tuna mitazamo ya nje ya box. After all nishampa pole!.
 
Wengine ndio tunaitwa waganga wa kienyeji kabisa, lol

Yaan kwa sasa namsisitiza adeal na Mlonge mbona atasahau kila kitu.

Bila shaka wewe ni mfuatiliaji wa tiba za Dr.Sebi. Big up!!.
Ukweli nikwamba kinachowaumiza na kuwapoteza wengi ni vidonge hatari vyenye sumu vya Arv's. Hivi vidonge baada ya kugundulika kwa lengo la kupambana na cancer wakavidirect kama anti retrovial drugs which is killing people more than AIDS itself. Halafu hawajali maan kampuni hizi big pharmas wanapata pesa mno.

"Let food be thy medicine and medicine be thy food"
 
Duuh, Mungu awajalie moyo waenye subra, ni ngumu kumeza lakini kaeni mpange namna ya kumtunza mtoto wenu.

Pengine katika matibabu yake, kuna dakatari, au mtu wa maabara au nurse mchoma sindano alifanya uzembe akatumia kifaa ambacho tayari kimetumika.

Au pengine amechangia nyembe za kuchongea pencil shuleni, au kukatia kucha na the like. Kifupi inauma sana
Nakubaliana na views zako.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Pole sana, Mungu akupe faraja maana hili linaumiza mno.

Inawezekana ameambukizwa kwa njia nyingine na si kwa kujamiiana, hata michezo mashuleni inawezekana ikawa ni sababu.

Cha maana kwa sasa weka nguvu nyingi kumsaidia na chache kuchunguza sababu. Epuka kumhoji saaana, tumia muda mwingi kumfariji na kumuelimisha.
 
Mkuu acha kupanic mchukue mtoto wako ukampime tena inawezeka wahusika walijichanganya na ukapewa majibu ya mtu mwingine
 
HIV huambukizwa kwa njia nyng na sio kufanya ngono isiyo salama pekee yake kama tunavojua wengi,kuna njia kama kuongezewa damu inaweza tokea accidentally in medical profession so u need to trace back if ur kid used to have blood transfusion, also sharing of unsterilized tools like wembe hasa kwa watoto inaweza sababisha though ni kwa %ndogo sana..kWa hyo nachokushaur ni kwamba try to act as a doctor of ur own family,take the medical history of ur kid in relaxed situation...am sure u can find sth unrevealed yet.
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Imenitouch sana hii asee! Hadi amefikia hatua ya kuharisha na kutapika viral load itakuwa heavy sana na stage yake itakuwa sio ya kuridhisha.

Muwaishe akapate medication mapema, but habari nzuri zipo kwamba kuna uwezekano mkubwa HIV ndani ya miaka 10 ikapatiwa cure kwani research za Dawa ya kutibu kabisa zimefikia karibu sana kugundua Dawa ya HIV akiwemo Dr Khalil mmarekani huyu amefanikiwa kutibu panya na sokwe kibao kwa tiba yake ya cell editing waliowapandikiza HIV na wote wàlipona kabisa.

Israeli wana Dawa yao inaitwa Gamorah iko katika hatua ya mwisho kabisa kukamilika.

USA tu ndio wanachelewesha maana HIV kwao ni fimbo ya kuchapia mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa misaada via USAID.. Sasa ikipatikana tiba tutakuwa na kiburi so he is controlling us kwa kupitia HIV maana soon Dawa ikigunduliwa atapoteza ushawishi wake Duniani.

But its around the corner maana mataifa kibao yanavumbua Dawa na kupata nguvu kijeshi punde Dunia itashindwa kuvumilia na kuzindua tiba kamili.

Relax! We will survive!

Usife moyo mkuu..mwanao probably akapona kabisa kama atasurvive for the next 10 years to come which is possible akipata medication early.

Don't lose hope.

Though, I'm so sorry to hear this? Sometimes the world is cruel and heartless.

Mkuu kweli nimeamni USA wanatumia ngoma kutokomoa mataifa yetu nasikia maambukizi mapya yemepungua sanaa kwa siku za hivi karibuni wazungu wanachukia sana mkienda upimaji afu mnaludi bila positive za kutosha
 
Daaahhh...imenigusa sana...pole ndugu yangu. Changamoto za maisha yetu ni nyingi sana ila kwake yeye aliyetuumba bado ni kimbilio sahihi juu ya haya. Naomba mrudie mungu atakupa jibu na sio jibu la wapi au imekuwaje kijana kapata tatizo hilo. Ni jibu la kuondoa tatizo hilo katika familia yako...yeye hashindwi kitu au jambo lolote...mkimbilie BWANA utaupata UZIMA WA MILELE.
 
Pole sana ndugu. Jaribu kumuuliza kama katika kucheza alikuwa anatumia vitu vyenye ncha kali vilivyotumika. Nakumbuka nilipokuwa mdogo ilikuwa ndio tabia yangu, wazee walikuwa wakinichapa sana maana nilikuwa naweka hadi kwenye mfuko wa kaptula. Nashukuru MUNGU sikupata magonjwa ila ni hatari sana.

Cha muhimu kwa sasa anahitaji uwepo wenu wa karibu mno. Usimjengee hali ya uoga kuepusha kujitenga au kutengwa na wenzake. Ikiwezekana muanzishie dozi huku ukimuomba MUNGU kwa sana. Narudia tena pole kwa matatizo yaliyokufika!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Me nahisi kwenye michezo yao kutumia kitu chenye incha kali akajikata kidogo akaona kawada au kuna mgeni alikuja kwenu hapo akawa anatumia vitu vyenye ncha Kali mtoto wako akawa anatumia si unajua watoto mama mdogo, au mjomba inawezeka akaupatia kwa hivo kwa yote pole sana but dawa itapatikana
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Imenitouch sana hii asee! Hadi amefikia hatua ya kuharisha na kutapika viral load itakuwa heavy sana na stage yake itakuwa sio ya kuridhisha.

Muwaishe akapate medication mapema, but habari nzuri zipo kwamba kuna uwezekano mkubwa HIV ndani ya miaka 10 ikapatiwa cure kwani research za Dawa ya kutibu kabisa zimefikia karibu sana kugundua Dawa ya HIV akiwemo Dr Khalil mmarekani huyu amefanikiwa kutibu panya na sokwe kibao kwa tiba yake ya cell editing waliowapandikiza HIV na wote wàlipona kabisa.

Israeli wana Dawa yao inaitwa Gamorah iko katika hatua ya mwisho kabisa kukamilika.

USA tu ndio wanachelewesha maana HIV kwao ni fimbo ya kuchapia mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa misaada via USAID.. Sasa ikipatikana tiba tutakuwa na kiburi so he is controlling us kwa kupitia HIV maana soon Dawa ikigunduliwa atapoteza ushawishi wake Duniani.

But its around the corner maana mataifa kibao yanavumbua Dawa na kupata nguvu kijeshi punde Dunia itashindwa kuvumilia na kuzindua tiba kamili.

Relax! We will survive!

Usife moyo mkuu..mwanao probably akapona kabisa kama atasurvive for the next 10 years to come which is possible akipata medication early.

Don't lose hope.

Though, I'm so sorry to hear this? Sometimes the world is cruel and heartless.
Kabisa Mkuu, umefanya vema kumtia moyo ndugu yetu.
 
Nimejisikia huzuni pole sanaa
Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi kulikabili hili pamoja na msongo wa mawazo
 
pole sana....nenda jukwaa la jf doctor "" katafute Uzi unaoitwa "" je unaweza kutembea na mtu aliyeathirika lakini usipate maambukizi.....utapata majibu yote huko """tena nivizuri zaidi kama mods wakiuhamishia huu Uzi wako huko
Acha bhana!!, wacha uzi huu ujitegemee.
 
Nililazwa na binti yangu wa kwanza kwa takribani siku 6 baada kuugua homa (akiharisha na kutapika ) lakini tukaruhusiwa juzi baada ya afya yake kutengemaa(japo amethoofika).

Majibu ya ugonjwa aliokuwa anaumwa yametoka kuwa ni HIV +, tulipatwa na mstuko kwa majibu hayo ilibidi mimi na mke wangu tupime lakini majibu yametoka hatuna maambukizi.

Hatukutosheka na majibu hayo tulienda Consolota na The dream kupima tena wote watatu lakini majibu yale yale sisi wazima ila mtoto ndio Positive.

Tulikaa kujiuliza kavitoa wapi? Ilibidi nisombe nyumba nzima maana nipo mimi, mke wangu, wanangu watatu, msichana wa kazi na bibi yangu nikawapeleka kupima lakini majibu ni yale yale.

Ikabidi tukampime kama aliwahi kubakwa ila alituficha lakini vipimo havioneshi hivyo.

Mpaka dakika hii tunajiuliza amevitoa wapi?

Niko na huzuni sana ndugu zangu.
Looo! Pole sana mkuu, it is very touching.
 
Back
Top Bottom