Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Nililazwa na binti yangu wa kwanza kwa takribani siku 6 baada kuugua homa (akiharisha na kutapika ) lakini tukaruhusiwa juzi baada ya afya yake kutengemaa(japo amethoofika).

Majibu ya ugonjwa aliokuwa anaumwa yametoka kuwa ni HIV +, tulipatwa na mstuko kwa majibu hayo ilibidi mimi na mke wangu tupime lakini majibu yametoka hatuna maambukizi.

Hatukutosheka na majibu hayo tulienda Consolota na The dream kupima tena wote watatu lakini majibu yale yale sisi wazima ila mtoto ndio Positive.

Tulikaa kujiuliza kavitoa wapi? Ilibidi nisombe nyumba nzima maana nipo mimi, mke wangu, wanangu watatu, msichana wa kazi na bibi yangu nikawapeleka kupima lakini majibu ni yale yale.

Ikabidi tukampime kama aliwahi kubakwa ila alituficha lakini vipimo havioneshi hivyo.

Mpaka dakika hii tunajiuliza amevitoa wapi?

Niko na huzuni sana ndugu zangu.
Pole sana nazani Shuleni katika kucheza na wenzie au mtaani kuna kitu cha ncha kali alichangia na mtoto ambaye ameathirika na VVU. Hawa watoto tunaawaacha wqcheze na wenzao lakini hatujui afya za marafiki wanacheza nao
 
sijaongelea mke wake, nmeongelea DNA ya Baba na huyo mtoto...kwani mke hawezi shiriki na dume gonjwa akapata ujauzito? alafu mama akabaki kuwa mzima...mtoto akaathiriwa?. Afanye hilo km ataweza maana kuishi na mwanamke kunahitaji akili ya ziada
Mkuu ww hujui sayansi kabisa. Mtoto hawezi zaliwa na HIV kamwe kama mama hana HIV.
 
Hivi vitu vyenye ncha kali vikitumika Na mtu ambae ni + alafu kikakaa labda hata masaa mawili je mtu ambae sio + akitumia anaweza pata maambukizi?

Napata mashaka sana na hizi vifaa vya masaloon jamani tutapona kweli?
 
Nililazwa na binti yangu wa kwanza kwa takribani siku 6 baada kuugua homa (akiharisha na kutapika ) lakini tukaruhusiwa juzi baada ya afya yake kutengemaa(japo amethoofika).

Majibu ya ugonjwa aliokuwa anaumwa yametoka kuwa ni HIV +, tulipatwa na mstuko kwa majibu hayo ilibidi mimi na mke wangu tupime lakini majibu yametoka hatuna maambukizi.

Hatukutosheka na majibu hayo tulienda Consolota na The dream kupima tena wote watatu lakini majibu yale yale sisi wazima ila mtoto ndio Positive.

Tulikaa kujiuliza kavitoa wapi? Ilibidi nisombe nyumba nzima maana nipo mimi, mke wangu, wanangu watatu, msichana wa kazi na bibi yangu nikawapeleka kupima lakini majibu ni yale yale.

Ikabidi tukampime kama aliwahi kubakwa ila alituficha lakini vipimo havioneshi hivyo.

Mpaka dakika hii tunajiuliza amevitoa wapi?

Niko na huzuni sana ndugu zangu.
Pole sana mkuu,
 
Kuna vitu viwili au vitatu hapo inaweza kuwa sababu.
1. Mazingira ya shule watoto hushirikiana vitu vingi bila uangalifu, au aliumia ktk bembea au vitu vingine vyenye ncha kali kama compass, nyembe
2. Watoto huchezea vitu hatari vyenye ncha kali hasa mazingira ya nyumbani. Pengine na watoto wenzie walio athirika.
3. Kwenye milango ya mabasi ya daladala au school bus kama anatumia huduma hiyo.
4. Je mliwahi kubadilisha mfanyakazi? Pengine huyo aliye ondoka ndio alikuwa muathirika. Sasa unakuta wana nyembe au sindano za urembo au heleni n.k.
5. Kuna mgeni alikuja na maradhi. Kwwnye miswaki watoto hawako makini.

Kuna watoto wengi tu huko mashuleni na jirani mtaani ambao ni waathirika wa HIV sema wanatumia dawa wanashirikiana na watoto wenzao vitu vingi vya hatari bila tahadhari. Pia wengine hupata mazingira ya hospital.

Jambo la msingi mtoto atumie dawa. Pole sana mkuu maana huo ni mtihani mkubwa sana kwa wazazi na mtoto mwenyewe.
Umeeleza vyema sana mkuu. Umeeleweka. Watoto kwasasa wapo ktk mazingira hatarishi sana kuliko enzi zetu tulivokuwa watoto.
 
Mkuu hili la route yake inaweza kuwa sababu.

Sasahivi watoto wengi wanaishi na VVU.
pole sana mkuu,samahani kwa swali hili au maoni haya nitakayo yatoa

huyo mtoto ni wa miaka 9 kama kafanya ngono ndio kwanza atakua ameanza muda mfupi uliopita,je kuna uwezekano ukampeleka kwa daktari kujua kama ana bikra?kwani si mtoto wa kike huyo au nimesoma vibaya?

ukijua hana bikra unaweza pata pakunzia atakuambia tu nani kamtoa,hapo utaanza ku deal na huyo mtu,ikiwepo kumfunga kabisa maana mtoto lazima atataja tu,na kwa umri huo hawezi kua katembea na watu wengi kama kaanza ngono

pole sana mkuu kwa huo mkasa,kama bikra ipo basi itakua kwenye michezo ya watoto,saloon,vitu vyenye ncha kali wanavyozea

hata hivyo mpaka ukimwi umeanza kuonekana inaashiria aliambukizwa si chini ya miezi sita iliyopita japo inategemea na kinga yake ipoje

kaa nae chini akuelezee vizuri ni mwanao tena mdogo hawezi kukushinda,kama hana bk utapata pazuri pakuanzia
 
Kingine HIV ni mdudu, je walimuona, uliza swali hili kwa hao walimpima, na sio kufanya kukisia maana mpaka sasa hakuna vipimo vya kumuonesha huyo mdudu kama ilivyo typhoid au malaria.
We ukipimwa mafua/influenza wanayaona?
 
Mkuu hili la route yake inaweza kuwa sababu.

Sasahivi watoto wengi wanaishi na VVU.
Mkuu nimewahi kufanya kazi ya kuhudumia nyumba za hawa watu. Maambukizi yana njia za ajabu nyingi. Labda shule alikuwa na kucha ndefu wakati wa ukaguzi akachukua wembe wa rafiki yake akakatia kucha.
 
Pole sana ndugu.aanze matibabu mapema ata survive tu
 
Imenitouch sana hii asee! Hadi amefikia hatua ya kuharisha na kutapika viral load itakuwa heavy sana na stage yake itakuwa sio ya kuridhisha.

Muwaishe akapate medication mapema, but habari nzuri zipo kwamba kuna uwezekano mkubwa HIV ndani ya miaka 10 ikapatiwa cure kwani research za Dawa ya kutibu kabisa zimefikia karibu sana kugundua Dawa ya HIV akiwemo Dr Khalil mmarekani huyu amefanikiwa kutibu panya na sokwe kibao kwa tiba yake ya cell editing waliowapandikiza HIV na wote wàlipona kabisa.

Israeli wana Dawa yao inaitwa Gamorah iko katika hatua ya mwisho kabisa kukamilika.

USA tu ndio wanachelewesha maana HIV kwao ni fimbo ya kuchapia mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa misaada via USAID.. Sasa ikipatikana tiba tutakuwa na kiburi so he is controlling us kwa kupitia HIV maana soon Dawa ikigunduliwa atapoteza ushawishi wake Duniani.

But its around the corner maana anataifa kibao yanavumbua Dawa na kupata nguvu.

Relax! We will survive!

Usife moyo mkuu..mwanao probably akapona kabisa kama atasurvive for the next 10 years to come which is possible akipata medication early.

Don't lose hope.

Though, I'm so sorry to hear this? Sometimes the world is cruel and heartless.
Mkuu una uhakika?hebu ongezea maneno hapo
 
daaah kuna vitu vinaumiza jamani, lakin ukimtunza vizuri ataishi maisha marefu na tiba zipo jirani, Mungu aibariki familia yako.
 
pole sana mkuu,samahani kwa swali hili au maoni haya nitakayo yatoa

huyo mtoto ni wa miaka 9 kama kafanya ngono ndio kwanza atakua ameanza muda mfupi uliopita,je kuna uwezekano ukampeleka kwa daktari kujua kama ana bikra?kwani si mtoto wa kike huyo au nimesoma vibaya?

ukijua hana bikra unaweza pata pakunzia atakuambia tu nani kamtoa,hapo utaanza ku deal na huyo mtu,ikiwepo kumfunga kabisa maana mtoto lazima atataja tu,na kwa umri huo hawezi kua katembea na watu wengi kama kaanza ngono

pole sana mkuu kwa huo mkasa,kama bikra ipo basi itakua kwenye michezo ya watoto,saloon,vitu vyenye ncha kali wanavyozea

hata hivyo mpaka ukimwi umeanza kuonekana inaashiria aliambukizwa si chini ya miezi sita iliyopita japo inategemea na kinga yake ipoje

kaa nae chini akuelezee vizuri ni mwanao tena mdogo hawezi kukushinda,kama hana bk utapata pazuri pakuanzia
Mkuu uwe unajitahidi kusoma mada na kuelewa. Ulichoongelea kipo kwenye mada tayari, unaharakia nini??
 
Mkuu mtoto ni wa kwangu na anafanana na mimi sio kawaida, Kusema alizaliwa na VVU ni ambacho hakiwezekani maana mama yake naye angekuwa na maambuki.

Ila kuna mdau amesema route yake ya mtaani na shuleni hii ndio na shaka nayo, maana watoto wengi sahizi wamezaliwa + .
nasemea kule hospital watoto kubadilishiwa wazazi au kuibiwa kabisa hizi kesi zipo hujawahi sikia hizoa....kwakuwa unasema mmefanana isivyokawaida basi sawa tupo pamoja.

itabidi uwekeze muda ktk kuchunguza hili swala la route zake

pole sana ndugu
 
This is very sad brother.

Issue zinazohusu watoto huwa very very sad.

Mungu akujaalie wepesi na familia yako.

The best you can do is stay strong for her. If you are weak, she will lose strength... and without strength and faith her perspective towards life and aurvival will be full of negative energy which is the last thing she needs.

She is still a child. She needs to enjoy her childhood without stigma, without having fingers pointed at her or being alienated and to achieve this you need to keep it secret, not out of shame but to protect her from all that.

 
Back
Top Bottom