Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Mwanangu wa miaka 9 amekutwa na Virusi vya UKIMWI, sijui amevitoa wapi?

Umenikumbusha jambo baya sana, Siku ka binti kangu nilikakuta kanachezea surgical/examination gloves! Nilijisikia vibaya sana tena alikuwa anapuliza kama puto!
Duh! Mungu atulindie tu hawa watoto wetu maana bila yeye ni ngumu sana kulifanikisha hili.
 
Nililazwa na binti yangu wa kwanza kwa takribani siku 6 baada kuugua homa (akiharisha na kutapika ) lakini tukaruhusiwa juzi baada ya afya yake kutengemaa(japo amethoofika).

Majibu ya ugonjwa aliokuwa anaumwa yametoka kuwa ni HIV +, tulipatwa na mstuko kwa majibu hayo ilibidi mimi na mke wangu tupime lakini majibu yametoka hatuna maambukizi.

Hatukutosheka na majibu hayo tulienda Consolota na The dream kupima tena wote watatu lakini majibu yale yale sisi wazima ila mtoto ndio Positive.

Tulikaa kujiuliza kavitoa wapi? Ilibidi nisombe nyumba nzima maana nipo mimi, mke wangu, wanangu watatu, msichana wa kazi na bibi yangu nikawapeleka kupima lakini majibu ni yale yale.

Ikabidi tukampime kama aliwahi kubakwa ila alituficha lakini vipimo havioneshi hivyo.

Mpaka dakika hii tunajiuliza amevitoa wapi?

Niko na huzuni sana ndugu zangu.
Pole mno mkuu, hakika niko katika viatu vyako naona jinsi unachomeka. Kwa kuwa mtoto ameanza kuugua jua kabisa hakapata virusi siku za karibuni. Atakuwa amepata nyuma kidogo kama immune yake ni nzuri. Kwa misingi hii ni ngumu sana kuweza ku trace chanzo ila kwa harakaharaka unaweza suspect yafuatayo:

i. Shuleni anakosoma kama kuna mtoto mwathirika na akawa say kuna contamination yoyote mtoto anaweza kuambukizwa.

ii. Watoto wa siku hizi kwa miaka tisa pia kuna utundu shuleni, imagine kama kuna uwezekano huo kuwa anaweza say kufanya kissing na mwenzie kumbe ana michubuko na kuambukizwa.

iii. Kuna incidence za ndugu au watumishi wa ndani ambao kama mkikosana na akiwa ni victim basi huwa anaweza kutumia miswaki ya watoto na kuacha traces za virusi hivyo ni rahisi mtoto kuambukizwa.

Cha msingi ni ngumu kupata chanzo sasa focus namna ya kumpatia tiba na matunzo mtoto wako. Jipe moyo ataendelea vizuri na ninaamini itapatikana dawa. Mungu akupe nguvu ya kustahimili yote haya.

Pole nyingi mno. Nimeumia sana
 
Ukiona jambo lolote limetokea ambalo sio la kawaida sana kwa binadamu, aidha liwe jema au baya, ujue Mwenyezi Mungu keshasaini...
 
Pole sana mkuu. Inawezekana ni katika michezo ya watoto maana huwa wanapenda kuokota vitu vyenye ncha kali na kuvichezea. Kwa upande wangu binti yangu alishawahi kufanya kitu cha hatari sana akiwa shule alitoa heleni na kuitumia kutobolea masikio ya wenzie pia na yeye kujitoboa tena. Kiukweli nilikosa amani mwezi mzima nilikosa ujasili wa kwenda kumpima. Lakini kikubwa kwa sasa fanya yale unayotakiwa kufanya kwa mgonjwa
 
Anaweza kuwa aliambukizwa wakati wa kujifungua na ma dr. Ama mtotk huyo sio wako walikubadilishia wakati amezaliwa
 
Dooh, pole sana Mkuu, dunia ina mengi, mtoto hana mipaka ya kutengamana na wenzake,kwa hiyo possibility ni ametoa kwa watoto wenzake, hususan kushea vitu
 
Pole, watoto wanachangia vitu vingi sana wawapo nje ya mazingira ya nyumbani
 
Imenitouch sana hii asee! Hadi amefikia hatua ya kuharisha na kutapika viral load itakuwa heavy sana na stage yake itakuwa sio ya kuridhisha.

Muwaishe akapate medication mapema, but habari nzuri zipo kwamba kuna uwezekano mkubwa HIV ndani ya miaka 10 ikapatiwa cure kwani research za Dawa ya kutibu kabisa zimefikia karibu sana kugundua Dawa ya HIV akiwemo Dr Khalil mmarekani huyu amefanikiwa kutibu panya na sokwe kibao kwa tiba yake ya cell editing waliowapandikiza HIV na wote wàlipona kabisa.

Israeli wana Dawa yao inaitwa Gamorah iko katika hatua ya mwisho kabisa kukamilika.

USA tu ndio wanachelewesha maana HIV kwao ni fimbo ya kuchapia mataifa ya ulimwengu wa tatu kwa misaada via USAID.. Sasa ikipatikana tiba tutakuwa na kiburi so he is controlling us kwa kupitia HIV maana soon Dawa ikigunduliwa atapoteza ushawishi wake Duniani.

But its around the corner maana anataifa kibao yanavumbua Dawa na kupata nguvu.

Relax! We will survive!

Usife moyo mkuu..mwanao probably akapona kabisa kama atasurvive for the next 10 years to come which is possible akipata medication early.

Don't lose hope.

Though, I'm so sorry to hear this? Sometimes the world is cruel and heartless.
hii itakuwa biashara kama zingine tuu
 
Pole sana! Maambukizi yanaweza tokea hata kwa vitu vyenye incha Kali!
 
Pole sana mkuu. Inawezekana ni katika michezo ya watoto maana huwa wanapenda kuokota vitu vyenye ncha kali na kuvichezea. Kwa upande wangu binti yangu alishawahi kufanya kitu cha hatari sana akiwa shule alitoa heleni na kuitumia kutobolea masikio ya wenzie pia na yeye kujitoboa tena. Kiukweli nilikosa amani mwezi mzima nilikosa ujasili wa kwenda kumpima. Lakini kikubwa kwa sasa fanya yale unayotakiwa kufanya kwa mgonjwa
Hakika watoto wapo hatarini! Umenikumbusha jambo kubwa sana! Watoto hata kushirikiana heleni haifai kabisa. Kwa bahati mbaya katika kucheza watoto wanaweza badilishana hata heleni.
 
Back
Top Bottom