Mwanariadha Alphonce Simbu amaliza nafasi ya 17 Olimpiki Jijini Paris, Ufaransa

Mwanariadha Alphonce Simbu amaliza nafasi ya 17 Olimpiki Jijini Paris, Ufaransa

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Leo aubuhi nimefuatilia shindano la Olympic kule Paris la mbio ndefu ya kilomita 42 na mwanariadha Ndugu Simbu akiwa mshiriki toka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kweli matokeo yake hayakuwa mazuri kwa kushika nambari 17 akitumia saa 2:10: 03
katika mbio hizo. Pole sana. Rudi nyumbani ukaendelee na mazoezi tena.

Matumaini ya Tanzania kuambulia chochote yapo kwa kinadada Jackline Sakilu na Magdalena Shauri ambao watatupa karata za mwisho za Tanzania katika mbio za Marathon kwa Wanawake ambazo ndio zitakuwa zinahitimisha rasmi Paris 2024.

Soma Pia: Wanariadha wa 4 kutuwakilisha kwenye mashindano ya Olimpiki huko Paris Ufaransa Mwezi Julai, Kambi kuwekwa Arusha

Katika matokeo mengine.

Tola Tamirat wa Ethiopia ndiye mshindi wa kwanza akinyakua medali ya dhahabu akiwa na rekodi mpya ya Olimpiki ya saa 2:06:26 huku nguli wa Kenya Eliud Kipchoge akishindwa kutetea taji lake.

Tola aliingia katika mbio za marathon za Olimpiki kama mchezaji wa akiba wiki mbili zilizopita, akijaza nafasi ya mchezaji mwenzake aliyejeruhiwa.

Bashir Abdi wa Ubelgiji alinyakua medali ya shaba kwa saa 2:06:47, huku Mkenya Benson Kipruto akitwaa shaba (2:07:00).

 
Leo aubuhi nimefuatilia shindano la Olympic kule Paris la mbio ndefu ya kilomita 42 na mwanariadha Ndugu Simbu akiwa mshiriki toka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kweli matokeo yake hayakuwa mazuri kwa kushika nambari 17 katika mbio hizo. Pole sana. Rudi nyumbani ukaendelee na mazoezi tena. Katika mashindano haya sijui kama Tanzania tutapata hata medali moja.
Tunampongeza mama kwa kufanikisha hilo
 
Leo aubuhi nimefuatilia shindano la Olympic kule Paris la mbio ndefu ya kilomita 42 na mwanariadha Ndugu Simbu akiwa mshiriki toka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa kweli matokeo yake hayakuwa mazuri kwa kushika nambari 17 katika mbio hizo. Pole sana. Rudi nyumbani ukaendelee na mazoezi tena. Katika mashindano haya sijui kama Tanzania tutapata hata medali moja.
Ni mpango wa Mungu, tena hapo alipaswa awe wa-30 kwakuwa SIFA NA UTUKUFU ALIKUWA amwagiwe FULANI , waacha iwe hivyo.
 
Back
Top Bottom