Mwanasheria Dkt. Kilangi atoa ufafanuzi kuhusu mchanga wa madini uliozuiliwa na Rais

Mwanasheria Dkt. Kilangi atoa ufafanuzi kuhusu mchanga wa madini uliozuiliwa na Rais

Agent of imperialist at work. Ahadi mojawapo Ya mwana Tanu ilikuwa ikisema nitajiellimisha kwa kadri Ya uwezo wangu kwa faida Ya watanzania walio wengi .mleta maada kajielimisha sana kwa faida ya imperialists. Very sad.Yeye na tundu lisu wamejielimisha sana kwa faida ya imperialists
Usiwasahau walee wahusika walio saini hiyo Mikataba!!.

Dr. [emoji310] Ametoa facts [emoji115] [emoji115] [emoji115] . Muhimu kuzingatia.
Well written!
 
Agent of imperialist at work. Ahadi mojawapo Ya mwana Tanu ilikuwa ikisema nitajiellimisha kwa kadri Ya uwezo wangu kwa faida Ya watanzania walio wengi .mleta maada kajielimisha sana kwa faida ya imperialists. Very sad.Yeye na tundu lisu wamejielimisha sana kwa faida ya imperialists
Bahati mbaya wewe hukujielemisha hata kwa faida yako binafsi. Na baada ya TANU kuwa hijacked, the rest ni historia.
 
Narudia kusema tena. Rais asione nongwa kuwaita kina Lissu na wenzake kujadili mbinu na njia ambazo zitakuwa na athari ndogo katika kuwabana hawa jamaa wa mchanga.
Akitumia hasira na maamuzi yasiyozingatia sheria ataiumiza nchi vibaya. Akae nao wabobezi Wa sheria ila siyo masaju, chenge
na mwakyembe watampoteza.
 
Nadhani labda tumesahau kuna kamati nyingine itakayoshughulika kuangalia madhara ya kiuchumi yaliyotokea na pia changamoto za kisheria zilizopo.
 
Mkuu,ni kweli kabla ya kuanza vita ilitakiwa kuanza kwa kupanga vikosi vyetu pamoja na dhana zitakazotumika kwa kuangalia uwezo wa zana za wenzetu ( sheria,taratibu,mikataba kama alivyoandika Dr.)ndipo sasa tungeingia vitani kifua mbele tukiwa na uhakika wa ushindi kutokana na kujua adui yetu yukoje.

Sasa vita imeanza ndio wakina "General Mayunga,Black Mamba & wababe wengine wa vita hii" wanaanza kutoa mbinu zao ambazo mpaka sasa majeshi yetu yalipofikia, tukisema tuwarudishe nyuma ndio tujipange twaweza rushiwa likombora tukaangamizwa,na tukisema tuendelee mbele na mapambano, hizo zana zetu pengine hazifai tena kwa mapigano ya huko mbele.

Sasa tuache mihemuko,tukae kama Taifa tuwe na mjadala mpana ili tufikie hatima iliyo salama kwa ustawi wa vizazi na vizazi vya Taifa letu.
hoja yako ni ya kweli kujipanga ni muhimu lakini kumbuka moja ya kombora hatari tulilonalo ni Acacia kudanganya kuhusu uzito wa makontena,9 kwa yaliyopitiwa yapo yaliyozidi uzito kwa tani wala sio kilo. Huu nao ni wizi wala haihitaji tume huru ni kumuita yeye tukapima atasema tumeongeza mchanga wa baharini?
Ni kujipanga tu mpaka hapo tunaongoza moja bila.
 
Hakuna kitu kaandika mtetezi wa wahuni tu huyo. Atuachie wazalendo tupambane yeye abaki na vifungu koko vya sheria alivyokariri kutetea mabeberu management ya Accacia.

Msomi Gani koko huyo asiyejua kuwa kilichokuwa kikifanywa na management ya accacia hakikuwa na baraka ya wanahisa wa Accacia? Ndio maana namuona kibaraka tu wa management ya accacia sio wanahisa wa accacia.

Management ya Acacia wamewaibia sana wana hisa wao subiri na ripoti ya makontaina waliyosafirisha miaka yote itoke wanahisa wapate taarifa yake. Huyu mwanasheria koko na wenzie akina lisu watatafuta shimo la kujificha. Mleta mada ni kati ya wanasheria finyu wasioangalia swala kwa upana wake.

Kabeba cv kubwa hewa. Kwa sasa wanahisa wako busy kuhakiki je kilichotoka Tanzania kiliwafikia kama kilivyo? Na je makontaina yaliyoondoka nchini yote yalienda kule kiwanda walichokubaliana au kuna yaliyochepushwa kwenda smelters zingine? Macho Ya wanahisa yote yako kwa magufuli wako naye asilimia 100 kwani wanataka ukweli ujulikane kujua kama management imewaibia au la.

Wakati wanahisa wako na magufuli wasomi sheria koko kama mleta maada wako na management ya accacia na wanapiga filimbi Ya hamelini kuitetea management. Mleta mada ona aibu nakala mpelekee tundu lisu na chadema. Hii vita tuachieni wazalendo nyie kaeni na mavyeti yenu koko ya sheria
Uzalendo uchwara
 
Agent of imperialist at work. Ahadi mojawapo Ya mwana Tanu ilikuwa ikisema nitajiellimisha kwa kadri Ya uwezo wangu kwa faida Ya watanzania walio wengi .mleta maada kajielimisha sana kwa faida ya imperialists. Very sad.Yeye na tundu lisu wamejielimisha sana kwa faida ya imperialists
sasa we msoshalist njoo na hoja zako za kututoa hapa tulipo.
 
Kabla hujatoa povu ungekaa na kujiuliza nani alikuwa anasign hizi contract na ni wakati gani. Wewe Yehodaya miaka yote ni CCM na viongozi wake sasa unaposema tumeibiwa wakati wewe ndo ulikuwa ukiimba CCM mbele kwa mbele tukueleweje? Huyu unayemkashifu huwezi funga hata gidamu za viatu vyake achilia mbali kukaa kuonge naye meza moja. You have nothing to contribute in this poor nation more than talking shite. Nyinyi ndo mlikuwa mnakaa kwenye magofu mnasubiri kengere mwende kwenye gwaride la chipukizi. Argue with points not with matapishi.
Thanks Dr. Kilangi You made my day.
Kuitetea ccm kwa mambo wanayoyafanya lazima utakuwa unatembea na dozi toka mirembe mfukoni.
 
Kwa uelewa wangu,naona Dokta angalau ametoa mwanga.Kwa mujibu wa utangulizi wake anasema yeye hataki kuegemea upande wowote ,kwa maana ya kutoa uamuzi wa aliyeshinda au kushindwa.Ukisoma kwa utulivu yeye amejaribu kutuonyesha pande zote mbili za shilingi.Sehemu ambapo kuna makandokando na mahali ambapo kama nchi tuna ahueni na tunaweza kusimamia kujihami.Hii ni vita ni lazima tuipigane tulinde mali ya nchi yetu.Kujikwaa si kuanguka.Hebu vichwa hivi vyenye uelewa wa sheria za madini ,za nchi na za kimataifa vikutanishwe viunge uzi mmoja vitoe ushauri.Huu si wakati wa kutoa silaha zote ndio maana wanaojua wamenyamaza wanasubiri wakati muafaka.Naomba tuendelee kuelimishana na mwisho wa siku",kitabu" kitasomeka kilaini na vita tutaishinda.Jiulize kama hii hela yote ingekuwa hazina ,maendeleo yangekuwaje.Kilio cha maji maji maji maji maji....umeme ..... kingeisha mara moja.
 
Doctor Kilangiee!! nakupinga sasa hatuwezi kuuza nchi kwa ajili ya makaratasi sasa!!!!!!

1. Umezungumzia suala la common heritage kuwa kwa kuwa baadhi ya nchi hazina madini basi iwe ruksa kwenda kuchota kwenye nchi zilizonayo .........Haikubalikiii!!!!! madini ni yetu na suala la madini si kama kwenye "high sea" amabapo kila mtu anaruhusiwa kutembea na kuvua ( shammba la bibi ) @ " RESCOMUNIIS"

2.Eti tutaenda kunyolewa bila maji huko ICSID kwa ku breach 'fair and equitable treatment' Hakuna hiyooo!!! wao wametutendea equity gani mpaka na sisi tuwatendee equity wanatuibia halafu waseme equity " IF YOU NEED EQUITY DO EQUITY:

3. Kwa kuwa hakuna mkataba wa kimataifa ambayo haina claus ya " PACTA SUNT SERVANDA" na kwa kuwa hao "mabwana wakubwa" hawakuiheshimu na wakaendelea kusafirisha mchanga kwa udanganyifu " maana yake hawajaheshimu mkataba" basi automatical doctine ya '' REBUS SIC STANTIBUS '' ita apply na kuufanya huo mkataba usitekelezeke !! yaani umevunyika nganganyanga beyond repair.
Endelea unadhani Iraq na libya walipenda ,ukikataa kutoa huwa wanatumia nguvu hao mabepari, watatungo uongo kuwa mnahifadhi magaidi kibiti huko wanashambulia kibiti madini wanavuna geita
Hakuna kitu kaandika mtetezi wa wahuni tu huyo. Atuachie wazalendo tupambane yeye abaki na vifungu koko vya sheria alivyokariri kutetea mabeberu management ya Accacia.

Msomi Gani koko huyo asiyejua kuwa kilichokuwa kikifanywa na management ya accacia hakikuwa na baraka ya wanahisa wa Accacia? Ndio maana namuona kibaraka tu wa management ya accacia sio wanahisa wa accacia.

Management ya Acacia wamewaibia sana wana hisa wao subiri na ripoti ya makontaina waliyosafirisha miaka yote itoke wanahisa wapate taarifa yake. Huyu mwanasheria koko na wenzie akina lisu watatafuta shimo la kujificha. Mleta mada ni kati ya wanasheria finyu wasioangalia swala kwa upana wake.

Kabeba cv kubwa hewa. Kwa sasa wanahisa wako busy kuhakiki je kilichotoka Tanzania kiliwafikia kama kilivyo? Na je makontaina yaliyoondoka nchini yote yalienda kule kiwanda walichokubaliana au kuna yaliyochepushwa kwenda smelters zingine? Macho Ya wanahisa yote yako kwa magufuli wako naye asilimia 100 kwani wanataka ukweli ujulikane kujua kama management imewaibia au la.

Wakati wanahisa wako na magufuli wasomi sheria koko kama mleta maada wako na management ya accacia na wanapiga filimbi Ya hamelini kuitetea management. Mleta mada ona aibu nakala mpelekee tundu lisu na chadema. Hii vita tuachieni wazalendo nyie kaeni na mavyeti yenu koko ya sheria
 
Maelezo ya Dr. Kilangi ni namna nyingine yenye ufasaha zaidi ya maelezo ya Mhe. Tundu Lissu. They have the same position. Na kwa maelezo ya Dr. Kilangi kweli hii ni vita, na mshindi wa vita anajulikana wazi kwa mujibu wa maelezo hayo ya Dr. Kilangi.

Kwa mtazamo wangu kabla ya kuanza vita, maelezo ya namna ya Dr. Kilangi yalitakiwa kutumika kwenye kupanga vita hii ili kuona kama kuna faida kubwa hasara kidogo au hasara kubwa faida kidogo. Pia ingesaidia kutoa options nyingi na kuchagua favourable option kama ingekuwepo kati ya hizo options.

Mimi ni mmoja wa watu tutakaopenda tusome 'kitabu' ili kupata mwanga zaidi. Kwani ili chapisho liitwe kitabu linakuwa na features zipi? Tena kitabu ndio kizuri zaidi kwani tutaona na references au bibliographies zaidi ambazo zitatusaidia tuone hoja zao kamili.
Safi sana well said
 
Hili ni andiko la Dr Adelardus Kilangi,mkurugenzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine tawi la Arusha,mwanasheria kitaaluma aliyebobea kwenye sheria za madini,na mwenyekiti wa bodi ya Petrol Tanzania!

............................................
Wandugu,

1. Nitaomba tuvumiliane. Niliombwa kusema kitu. Nitaandika kwa kirefu kidogo. Kwa kuwa ninaandika muda huu, nina advantage ya kuwa nimesoma maoni mengine yaliyotangulia. Nilicheka sana kaka yangu Ngwilimi aliposema halali hadi nimetoa maoni. Sipendi kumkosesha usingizi. Nitaandika kwa paragraphs ili kurahisisha rejea.

2. Nimeangalia maoni mbalimbali yaliyotolewa humu. Yanagusa maeneo yafuatayo:

i)Statement ya Acacia.

ii)Suala la sovereignty over natural resources na tatizo la 'state capture'.

ii) Suala la smelting na mchanga wa makinikia.

iv)Nini tunaweza kufanya kwenye mikataba:
- kuvunja mikataba?
- kushitaki kwa kutuibia?
- ku-review mikataba?
- au kuweka mikataba wazi?

vi) Sheria za kimataifa.

3. Haya ni mambo mengi na mazito. Sio rahisi kuya-summarize kwenye text ya simu. Pia ni vema kukubaliana kuwa kwenye mjadala kama huu itikadi, vyama na mihemuko iwekwe pembeni. Hoja zitawale.

4. Sitaingia kwenye mtego wa kulaumu au kutetea mtu. Nitajikita kwenye masuala ya msingi yanayotengeneza chimbuko la tatizo. Matatizo katika sekta yetu ya Madini, kama ilivyo ktk nchi nyingi zinazoendelea, nyingi zikiwa Africa, na Tanzania ikiwemo, yana chanzo chake ktk maeneo matatu:

i) Falsafa inayotuongoza,
ii) Sheria inayotuongoza.
iii) Mfumo wa utawala.

FALSAFA INAYOTUONGOZA

5. Malalamiko kuwa nchi zinazoendelea na zenye kumiliki resources zinapunjwa hayakuanza leo. Yalianza miaka ya 1950. Haya yalipelea kuibuka kwa falsafa mbili: resource nationalism na resource liberalism. Kila moja ina implications kwenye sheria na kwenye namna nchi itasimamia raslimali zake.

6. Wale wa resource nationalism walitaka nchi iwe na mamlaka kamili kwa resources zao na ziwasaidie na wakatengeneza principle ya permanent sovereignty over natural resources. Walitaka mambo haya yasimamiwe zaidi na sheria za nchi.

7. Wale wa resource liberalism wanataka raslimali ziwe wazi kwa dunia nzima maana mgawanyo wake duniani hauna usawa (japokuwa wao wamelinda teknolojia yao).

8. Katika vision ya nchi, nchi inachagua falsafa ya kufuata. Falsafa inayofuatwa huathiri sera na sheria.

9. Baada ya Uhuru Tanzania ilifuata falsafa ya resource nationalism hadi 1979. Kuanzia 1979 Tanzania ikaanza kufuata resource liberalism baada ya shinikizo la World Bank na IMF chini ya kitu kinaitwa Washington Consensus. Falsafa hii ilifikia kilele miaka ya 1990 mwishoni. Kwa hiyo ikaathiri sera na sheria.

10. Kuanzia mwishoni mwa miaka ya 2000 nchi imejaribu kurudi kwenye resource nationalism lakini inakwama. Sasa hivi resource nationalism sentiments ziko very high.

SHERIA INAYOTUONGOZA

11. Kama nilivyosema, falsafa huja kuathiri Sera na Sheria. Sheria muhimu hapa ni (nitachanganya lugha kidogo hapa):

i) investment law
ii) mining/petroleum law
iii) tax law.

Investment Law

12. Hiki ni chanzo kikubwa cha ugomvi. Nchi zilizoendelea zimeshinikiza uwepo wa mfumo wa sheria wenye kugandamiza nchi zinazoendelea. Mfumo huu unagawanyika kama ifuatavyo na kila kipande kina matatizo makubwa na mengi.

i) customary international law. Humu kuna principles nyingi ambazo nchi inaweza kuambiwa kuwa imezivunja. Nchi zilizoendelea na zinazoendelea zinagombana juu ya principles hizi.

ii) multilateral framework. Hapa kuna mikataba ya mataifa mengi. Tanzania ni mwanachama Wa mikataba miwili yaani unaoanzisha Multilateral Investment Guarantee Agency (MIGA) na unaoanzisha International Centre for the Settlement of Investment Disputes (ICSID).

iii) bilateral framework. Hii ni mikataba kati ya nchi na nchi (bilateral investment treaties - BITs. Ila inawalinda wawekezaji toka nchi hizo mbili. Nchi inaweza kushindwa kesi sio sababu ya mikataba ila kwa sababu ya BITs.

iv) national framework
(mining and petroleum acts) - hizi zina certain aspect fulani za investment.

v) state-investor agreements (tunayoita mikataba na wawekezaji).

Wengi tunaangalia hii tu. Hatuangalii hizo frameworks zingine ambazo baadaye zinatukandamiza.

Pia, framework No. i, ii, na iii ziko chini ya himaya ya sheria za kimataifa.

Mining/petroleum law

12. Mining and petroleum law hutengenezwa na nchi yenye resources. Lakini nchi zilizoendelea huwa zina-influence mno zoezi la utngenezaji sheria hizi, maana hizo ndio hutoa mineral or petroleum rights. Wako tayari hata kuidanganya nchi kwa misaada wanayojua tunahitaji sana. Wanaweza kutudanganya kuwa wanatupatia technical support. Kumbe wanatutengenezea sheria itakayowezesha kutuibia.

Tax Law

13. Tax law ni Eneo jingine ambalo linatumika sana kutuibia. Mnapokuwa mnatengeneza sheria zenu za kodi hawa jamaa hawaachi kuwazungukieni na kuwa-influence.
MFUMO WA UTAWALA

14. Kuna tatizo kubwa sana linalozikumba hasa nchi za Africa na baadhi ya zinazoendelea zilizo nje ya Africa. Hili ni tatizo la 'state capture'. Kama ilivyo concept ya 'river capture' kwenye geography, basi state capture means influence by the elite or business people or investors such that the state (led by its government) fails to think on its own and it follows the thinking of the group that has captured it.

15. Wakati wa kufuata falsafa ya resource liberalism, Tanzania iliingia kwenye total 'state capture'. Ndio kusema tuliondoa kichwa chetu tukaweka kichwa kingine. Tukawa tunafikiri kwa mfumo wa hicho kichwa kingine. Sasa tumeanza kurudisha kichwa chetu.
SUALA LA MCHANGA WA MADINI

Utangulizi

16. Suala hili wote tunajua background yake. Kamati ya Pili natumaini itafanya kazi ya na uchambuzi Wa kutosha.

Mchanga kwenye Madini ni Mali ya nani?

17. Principle ya 'permanent sovereignty over natural resources inasema huu ni Mali ya nchi. Article 27 of the Constitution of the URT inachukua mwelekeo huo huo. Hata Section 5 of the Mining Act says the same. And the same position was in Mining Acts za 1998 na 1979. Zile za kabla ya Hapo ziikuwa zinazungumzia mwingereza.

18. Hata hivyo kuna ubishi kuwa pale nchi inaposaini state-investor agreement (Mineral Development Agreement) na kutoa mineral rights je nchi inakabidhi sovereignty yote kwa companies. Makampuni yatasema 'ndiyo'. Nchi zinatakiwa ziseme 'hapana'.

19. Mineral rights means rights to extract minerals and sell them. Does it include transporting them outside the country in order to extract minerals? I don't think if contracts say so. And if they do, that defeats the principle of permanent sovereignty over natural resources!

Nini Tunaweza kufanya kuhusu mikataba?

20. Kuivunja? Hatuwezi kuivunja. Tumesaini mkataba wa MIGA na wa ICSID. Tutashtakiwa kwa kuvunja customary law principle ya 'fair and equitable treatment', na 'state responsibility' na ya 'respect for acquired rights'. Tutapelekwa mbele ya ICSID na kuhukumiwa, kisha tutaminywa na MIGA itakayokamata mali zetu popote zilipo.

21. Kuwashtaki makampuni kwa kutudanganya? Tunaweza, na tutatumia argument kuwa wamevunja customary law principle ya 'good faith and prohibition of abuse of rights'. Lakini wakisema uchunguzi wa mchanga tumeufanya kwa upande mmoja wanaweza kushinda.

22. Ku-review mikataba? Lazima tuwe tume -incorporate kwenye mkataba kipengele kinachohusiana na doctrine ya 'clausula rebus sic stantibus'. Hii ni doctrine inayoruhusu ku-review mkataba kama conditions Fulani zikibadirika. Lazima kifungu hiki kiwe kwenye mikataba. Hawa jamaa walihakikisha hakimo kwenye mikataba yetu. Kwa hiyo ukianza process ya ku-review unilaterally watasema umevunja principle ya 'fair and equitable treatment'.

23. Kuiweka wazi mikataba ili watu wote waione? Investors wataegemea kwenye principle of confidentiality of investment agreements. Hii principle IPO katika international law. Ingawa sasa kuna mabishano makubwa. Wengine wanaipinga. Ndio maana japokuwa tuna sheria mpya ya uwazi na uwajibikaji - Extractive Industries (Transparency and Accountability) Act, 2015, ambayo inasema mikataba yote iwekwe wazi, makampuni yamekataa kwa kusema kuwa wakati wanasaini mikataba hiyo sheria hiyo haikuwepo. Mnavyojua sheria hairudi kinyume. Kumbe watadai bado canal in sea na principle hiyo.

24. Kwa hiyo kumbe tunaweza kufanya nini sasa? KAMA ALIVYOSEMA MHESHIMIWA RAIS, HII VITA, NA HII NILIYOTOA HAPA NDIO PICHA HALISI YA VITA HII.

Basi wandugu siku nyingine msinitafute ili nitoe Maoni yangu. Vinginevyo mjiandae kusoma kitabu.
Thanks Dr kwa ufafanuzi huo Ubarikiwe sana
 
Amenifungua ubongo, just why tangu mabishano haya yaanze, sija comment chochote. Mwanzo niliona Kama Raisi amefanya vizuri, lakini kadri Siku zinavyokwenda naaza kukata tamaa. Tuendako nathani kuna kiza kinene.
Usikate tamaa Major,huwezi amin ukichagua side sasa hivi utakua unabetia mawazo yako,acha kubeti kwenye hii issue,hata kesi iwe vipi mawakili wanakuwepo pande mbili na hapo ndipo panabeba maana ya neno "usikubali kubeti" tuache wanaojua sheria waumane tusijipe pressure Major trust me kesi ni kesi tu,atakayekuwa na wakili makini atashinda,we stay tune ITAFAHAMIKA
 
Agent of imperialist at work. Ahadi mojawapo Ya mwana Tanu ilikuwa ikisema nitajiellimisha kwa kadri Ya uwezo wangu kwa faida Ya watanzania walio wengi .mleta maada kajielimisha sana kwa faida ya imperialists. Very sad.Yeye na tundu lisu wamejielimisha sana kwa faida ya imperialists

Na wewe toa elimu yako
 
Uchunguzi wa upande mmoja hauwezi kukubalika katika mahakama za kimataifa na hili ndio kosa kubwa tulilolifanya.

Kingine cha kushangaza ni kwanini serikali haitaki kukubali hoja ya ACASIA ya kuunda Tume Huru kuchunguza jambo hili?
Naomba unijibu kulingana na nilivyo uliza,,,SWALI,.

1.Ukihisi unaibiwa,utamwambia unaemhisi aje mthibitishe kwa pamoja kabla ya wewe kuwa na uhakika kuwa umeibiwa!!!?

2.Naomba unithibitishie hii kauli yako,, "Serikali haitaki" ili nielewe kwa nini unashangaa

Kuelimishana ni vizuri ila kueleweshana ni vizuri zaidi,nna imani utanielimisha nnapokosea na nitaelewa nisipopaelewa
 
Binadam sisi ni watu wa ajabu sana. Kwa mfano JPM asingezuia hayo makontena, haya tunayoyaongea tungejuaje. Tungeelewaje undani wa hizi asasi za kimataifa tulipojifunga? JPM did the best ever, nani mwingne angeweza kufanya hayo? Kama umemuelewa mtoa mada kuna kitu kakieleza kinaitwa state capture, kuna ma tycoon na watu wazito waliokuwa na influence kwenye kuridhia hizo sheria kandamizi ila JPM hakujali hlo amejali nchi kwanza. Tusimlaumu JPM, ametufunilia ni jinsi gani tulikuwa tunaibiwa.. Maana kila mwenye akili timam anaona kuwa mikataba hyo na ya kilaghai na kinyonyaji. Tuchambue tuwezavyo ila tusimtafute mchawi.

[HASHTAG]#tutalivuka[/HASHTAG] [HASHTAG]#daraja[/HASHTAG] [HASHTAG]#tukilifikia[/HASHTAG].
 
Hivi karibuni kumetokea varanganti la aina yake kuhusu taarifa ya kamati ya makinikia. Kumejitokeza kuvutana kati ya Setikali na wawekezaji na pia baadhi ya Wananchi amegawanyika pia na inavyoonekana kila siku zinavyokwenda mbele ndivyo mzozo unazidi. Natoa mapendekezo kwa Serikali na wawekezaji kusafirisha hayo makinika mpaka yanapochambuliwa, yasimamiwe na pande zote mbili wakati wa kuchambuliwa na ukweli upatikane na hicho ndicho kiwe kigezo cha wawekezaji kulipa kodi kwa kila makinika yatakayokuwa yanapelekwa huko kabla hatujanunua mashine yetu.
N.B. Mod tafadharini msiuunganishe uzi huu na nyuzi nyingi kupindukia zilizomo humu. Napenda serikali iupitie ushauri huu ili kumaliza mzozo huu kistaarabu.
 
Hakuna kitu kaandika mtetezi wa wahuni tu huyo. Atuachie wazalendo tupambane yeye abaki na vifungu koko vya sheria alivyokariri kutetea mabeberu management ya Accacia.

Msomi Gani koko huyo asiyejua kuwa kilichokuwa kikifanywa na management ya accacia hakikuwa na baraka ya wanahisa wa Accacia? Ndio maana namuona kibaraka tu wa management ya accacia sio wanahisa wa accacia.

Management ya Acacia wamewaibia sana wana hisa wao subiri na ripoti ya makontaina waliyosafirisha miaka yote itoke wanahisa wapate taarifa yake. Huyu mwanasheria koko na wenzie akina lisu watatafuta shimo la kujificha. Mleta mada ni kati ya wanasheria finyu wasioangalia swala kwa upana wake.

Kabeba cv kubwa hewa. Kwa sasa wanahisa wako busy kuhakiki je kilichotoka Tanzania kiliwafikia kama kilivyo? Na je makontaina yaliyoondoka nchini yote yalienda kule kiwanda walichokubaliana au kuna yaliyochepushwa kwenda smelters zingine? Macho Ya wanahisa yote yako kwa magufuli wako naye asilimia 100 kwani wanataka ukweli ujulikane kujua kama management imewaibia au la.

Wakati wanahisa wako na magufuli wasomi sheria koko kama mleta maada wako na management ya accacia na wanapiga filimbi Ya hamelini kuitetea management. Mleta mada ona aibu nakala mpelekee tundu lisu na chadema. Hii vita tuachieni wazalendo nyie kaeni na mavyeti yenu koko ya sheria
Haya mwenye mbwa kamteua mtetezi wa wahuni kuwa AG..ngoja tuone mbwa mzalendo ataendelea kubweka au!
 
Back
Top Bottom