Mwanasheria Mkuu wa Serikali ajiuzulu, ameshindwa kumshauri 'kisheria/kikatiba' Rais Samia S Hassan

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ajiuzulu, ameshindwa kumshauri 'kisheria/kikatiba' Rais Samia S Hassan

Kwanza, wakati Mama Samia anatangaza kifo cha Hayati JPM, alitangaza siku 14 za maombolezo ilihali kwenye katiba zinatajwa siku 21. Baadae Katibu Mwenezi CCM ndg Polepole akatangaza siku 21 kwa niaba ya chama 'MKANGANYIKO'. Wananchi walihoji kwanini Makam alitangaza siku 14 badala ya 21 'Mwanasheria' hakuliona hili.

Pili, mara tu baada ya kuapa na kutoa hotuba fupi, taarifa iliyotolewa ni kwamba Rais anaenda kuongoza kikao cha Baraza la Mawaziri.

Baadae TLS wakatoa mwongozo wa kikatiba na kisheria kuhusu Baraza hilo kuwa kwasasa 'halipo'. Mwanasheria Mkuu na wanasheria wengine wa serikali mlikuwa wapi? Mbona hamjasema chochote? Washauri wa Rais mnamsaidiaje Rais?

Pia soma

Wakati mwingine ndiyo maana tunaamini taarifa za mitandaoni kuliko za serikali

Fuatilia vizuri, viongozi wengi wa serikali huwa hawajui sheria wala katiba kwa upana wake,na wenye wajibu wa kisheria hufanya kuendana na mdundo wa kiongozi. wakati wa Magufuli ilikuwa ni rahisi sana kuongoza maana alikuwa hafuati sheria, bali alikuwa anatumia njia aliyooita nia njema ikiongozwa na uzalendo, hivyo mwanasheria Mkuu wa serikali, majaji, mahakimu na wengine walikuwa wanatekeleza sheria sio kama zilivyo, bali alivyokuwa anataka Magufuli. Sasa inaonekana bado mwanasheria Mkuu, Jaji Mkuu na wengineo bado wako kwenye hangover ya utawala wa Magufuli.
 
Pia Rais ali hutubia Baraza jana ukutani ku kiwa na Picha ya JPM. Ni kosa Kubwa!!
 
Wanachojua ni ilani ya sisiem,
Hizi nafasi za kupewa zina shida sana serikali ibadilishe namna ya kuwapata hawa watu,
Watume maombi usahili ufanyike serikali ishirikiane Tanganyika Law Society kutuletea mwanasheria wa ukweli si hawa makada wa CCM.
Umeongea ukweli mtupu, tatizo haya mambo ya uchamauchama haya wakishaona TL yuko pale wanaona kama wote ni Chadema
 
Rais ndio kanuni ya Katiba

Katiba haimwongozi rais ila rais anaingoza katiba

Katiba ni kitu ila Rais ni Nafsi

Punguza utoto, si ajabu ww ndio ulikuwa kwenye mpango wa kuchezea katiba kwa maslahi yenu, kuwa jiwe aongezewe muda ili muendelee kupiga huku mkipindisha sheria.
 
Hivi Mh Samia ataacha/atabadilisha wangapi?
Mbona hamsemi Mabeho au Siro nk nk. Wanafiki wa kubwa nyie na safari hii mnachokitafuta miaka nenda rudi msipokuwa makini mtakipa.

Nchi hii imedhalilishwa kwa miaka mingi na wanasiasa wanafiki, wachumia tumbo pangu pakafu tia mchuzi.
 
Hivi Mh Samia ataacha/atabadilisha wangapi?
Mbona hamsemi Mabeho au Siro nk nk. Wanafiki wa kubwa nyie na safari hii mnachokitafuta miaka nenda rudi msipokuwa makini mtakipa.

Nchi hii imedhalilishwa kwa miaka mingi na wanasiasa wanafiki, wachumia tumbo pangu pakafu tia mchuzi.
ahaha,wasukuma mwisho wenu kiutawala ushafika!!!!!
 
ahaha,wasukuma mwisho wenu kiutawala ushafika!!!!!

Wewe ni wa ajabu kabisa !Taifa la Tanzania lilipata Kiongozi Rais JPM ambaye alijitambua na akawa zaidi upande wa wananchi walio wengi na akajitofautisha na Watangulizi wake tukimuondoa Mwl JK Nyerere.

Ukombozi kamili wa Watanzania wengi utapatikana kama watanzania ambao pia ni wengi maskini walio katika vyombo vya ulinzi na Usalama/ Majeshi yetu watajitambua na kuacha kutumiwa na baadhi ya wanasiasa ndivyo sivyo.

Wanasiasa wanaringia hayo Majeshi hawana lolote lengine, pasipo kushikwa mkono na wajeda wa nyanja zote hawana jeuri yeyote.

Wànajeshi na vyombo vya ulinzi na usalama wakikataa kwa kumaanisha maadili ya hovyo ya baadhi ya wanasisa pasi shaka wanasiasa hao watafuata mstariiii nyookaaà.
 
Moja ya madhaifu makubwa ya Bw. Magufuli ilikuwa ni kuendekeza ukabila na ukanda, kwenye teuzi zake alipenda sana kufuata hayo mambo mawili.
 
Wewe ni wa ajabu kabisa !Taifa la Tanzania lilipata Kiongozi Rais JPM ambaye alijitambua na akawa zaidi upande wa wananchi walio wengi na akajitofautisha na Watangulizi wake tukimuondoa Mwl JK Nyerere.

Ukombozi kamili wa Watanzania wengi utapatikana kama watanzania ambao pia ni wengi maskini walio katika vyombo vya ulinzi na Usalama/ Majeshi yetu watajitambua na kuacha kutumiwa na baadhi ya wanasiasa ndivyo sivyo.

Wanasiasa wanaringia hayo Majeshi hawana lolote lengine, pasipo kushikwa mkono na wajeda wa nyanja zote hawana jeuri yeyote.

Wànajeshi na vyombo vya ulinzi na usalama wakikataa kwa kumaanisha maadili ya hovyo ya baadhi ya wanasisa pasi shaka wanasiasa hao watafuata mstariiii nyookaaà.
We jamaa unatumia ubongo upi kufikiria???? Shwain mkubwa
 
Kwanza, wakati Mama Samia anatangaza kifo cha Hayati JPM, alitangaza siku 14 za maombolezo ilihali kwenye katiba zinatajwa siku 21. Baadae Katibu Mwenezi CCM ndg Polepole akatangaza siku 21 kwa niaba ya chama 'MKANGANYIKO'. Wananchi walihoji kwanini Makam alitangaza siku 14 badala ya 21 'Mwanasheria' hakuliona hili.

Pili, mara tu baada ya kuapa na kutoa hotuba fupi, taarifa iliyotolewa ni kwamba Rais anaenda kuongoza kikao cha Baraza la Mawaziri.

Baadae TLS wakatoa mwongozo wa kikatiba na kisheria kuhusu Baraza hilo kuwa kwasasa 'halipo'. Mwanasheria Mkuu na wanasheria wengine wa serikali mlikuwa wapi? Mbona hamjasema chochote? Washauri wa Rais mnamsaidiaje Rais?

Pia soma

Wakati mwingine ndiyo maana tunaamini taarifa za mitandaoni kuliko za serikali
Hili neno kujiuzulu limelua fasheni sana.
 
Mwigulu Nchemba Wajibu TLS:
Nimesoma andiko la TLS, kwa heshima zote kwa chombo chetu hiki kilichopewa mamlaka kisheria, Nimeshtuka sana, I wish to say,

Kwanza KATIBA HAIJAVUNJWA KWA MHE RAIS SAMIA SULUHU kuapa, na wala hakuna Mkanganyiko wowote wa Kikatiba, kwa yeye kutoteua PM na Baraza jipya. Mmekaa wote kweli mkaona hivyo!
Kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 42(5) kuna watu wa aina mbili wanaweza kuwa Rais. Moja, Rais Mteule ambaye anatokana na Ibara ya 42(1). Mbili, Mtu anayeshika kiti cha Rais ambaye anatokana na ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ambaye ni Makamu wa Rais. Kwa Mazingira haya, Makamu wa Rais, baada ya kifo cha Rais, anakuwa Kaimu Rais baadae ndio ameapa na kuwa RAIS wa Nchi. Rais Mteule anapatikana kutokana na uchaguzi. Hivyo basi ibara ya 57(2)(f) ya Katiba haitumiki katika mazingira haya. Kwa mjibu wa Sheria, Mhe Rais alitakiwa kutoa taarifa hii kwenye Baraza la Mawaziri baada ya kuapa na alifanya hivyo, maana yake Baraza lipo.

Hata hivyo kwa tamaduni za Kiafrika, kitanzania na Misingi ya UTU, SIONI KAMA NI JAMBO JEMA SANA KUANZA KUJADILI MGAWANYO WA MADARAKA TUNGALI HATA HATUJAMZIKA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU. HUU SIO MSIBA MDOGO, JAMBO HILI ZITO LIKO MIKONONI MWA RAIS WETU MAMA SAMIA SULUHU, HALAFU SISI TUANZE KUMPATIA MAMBO YA MARA TEUA PM, MARA VUNJA BARAZA, KATIBA INAELEKEZA RAIS KUAPA NA NAMNA YA KUMPATA MAKAMU WA RAIS.

KWA MJIBU WA KATIBA RAIS ANARUHUSIWA KUVUNJA BARAZA MUDA WOWOTE NA KUPANGA ATAKAVYO HATA SIO KWA MAZINGIRA KUAPA KWAKE,

KWANINI HATUIONI HEKIMA YAKE YA KUSHUGHULIKIA MSIBA KUMSITIRI KWANZA ALIYEKUWA KIONGOZI WETU? TUNAANZA NA MAZISHI AU MIRATHI? 😭😭😭😭
 
Baadae TLS wakatoa mwongozo wa kikatiba na kisheria kuhusu Baraza hilo kuwa kwasasa 'halipo'. Mwanasheria Mkuu na wanasheria wengine wa serikali mlikuwa wapi? Mbona hamjasema chochote? Washauri wa Rais mnamsaidiaje Rais?
Professor Kilangi hawezi kukosea kwa vitu Kama hivyo
Hao TLS walitakiwa pia waseme hakuna AG Kama kweli hoja yao Ina mashimo,Rais anapaswa kuteua AG kwanza
Tatizo wanasheria wengi wakishapata mihuri hawajisomei,Kama karume,kila siku kutoa vifungu vilivyofutwa
 
Hatufai kabisa ni bomu tu
Watu watatu 3 hawa;

1. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, nafikili anaitwa Kilangi

2. DPP

3. Solicitor General - Gabriel Malata.

Hawa watu walichangia sana kuminya haki za Watanzania.
 
Back
Top Bottom